Rais Kikwete aahirisha kuongea na 'Wazee wa Dar'; sasa kuongea nao Jumatatu wiki ijayo

Wagalatia7 walijipanga long time kuhakikisha kuwa Wanamdondosha! Walipanga mipango yao ikakamilika, watu wao wakatoa mzigo (Wote Wagalatia), wakapitishia kwenye bank yao, wakahakikisha kila mgalatia aliehusika hata siku za nyuma wanapata gawio kutokana na roles n responsibilities zao! wengine wakaenda mbali Zaidi baada kutoa mzigo waka-inform wahisani (WB,IMF) kuwa mtego umekamilika! Kibinyo kikaanza, Mgalatia mmoja akajitoa kafara eti yeye ndo hakueleweka, wagalatia wagalani wakampongeza kwa hatua yake huku wakimtumia JK kushukuru!!! Wagalatia wamegoma kuachia ngazi, wanatishia kuwa kuliko wao waachie ngazi bora Serikali yote iwajibike!!! Wanajua kuwa JK ndo ataonekana zoba !!!... Nasema tu, Lakini Jambo hili si zito sana ila Mwenyewe anaruhusu kupandiwa mabegani!!! Dawa ni kuchinja wagalatia wengi awezavyo hadi Heshma ipatikane!!! I stand to be corrected

NB: Wagalatia7 haihusiani na Imani bali kikundi cha EHT wenye kupenya kwenye Imani tofauti tofauti...

Watanzania mmemtukana sana mzee wenu ila j3 anaenda kuwapa zawadi ya x-mas na mwaka mpya anaenda kuwaacha watu wote midomo wazi, idara zote za usalama wametoka watu very faithful pamoja na wazee kuminambili wamejifungia mahali wanatengeneza sura mpya yakitaifa. Singasinga atajuta kutafuna fedha za wa Tz. Serikali imeomba msaada toka idara za nchi washirika zenye nguvu kwenda rudisha fedha za watanzania. Huu ndio mwisho wa ufisadi, mambo yote ni siri tena siri kubwa watu wameapa kiapo chakuto kutoa siri. No phn no anya connection only ikulu cable used. Hao walio toka nakuwautubia wa Tz kwamba niwasafi wanaenda kufa kisiasa maana uwenda asubuh ya j3 itakuwa mwisho wa kuwa mawaziri na hawatotakiwa kuongea chochote ktk media! Stay tune Tz
 
Rais JK ambaye alikuwa ahutubie taifa kwa kuongea na wazee wa DSM ameahirisha, kisa yupo nje ya DSM. Kitendo alichokifanya Rais huyu wa nchi ni ubaguzi wa kutenga maeneo ndani ya nchi moja. Kwani Rais anahutubia wazee wa DSM tu na si wananchi wote?

Kama suala ni kufikisha meseji kwa wananchi wote kwa kuwahutubia wazee wa mkoa fulani, ni kwanini Rais asihutubie wananchi kupitia wazee wa Arusha kule alipo sasahivi? Kitendo cha kuacha kuhutubia taifa ambapo wananchi wengi walikuwa wameahirisha shughuli zao kwa kupangua ratiba ili wasikie mwongozo wa nchi inapoelekea hakikubaliki, na huu ni mwendelezo wa udhaifu ambao umekuwa ukitajwa mara kwa mara.

laiti kama Rais angekuwa nje ya nchi hapo angeeleweka, lakini tunaambiwa Rais yupo Arusha ambapo bado ni Tanzania. Rais anaweza kuhutubia hata akiwa Tandahimba ama Nyamikoma ili mradi tu ujumbe ufike kwa wananchi wote.

Iwapo hajaahirisha kwa suala la ubaguzi basi, rais amekariri kila hotuba lazima aitolee DSM, ama kuna hakuwa amejiandaa tayari na kuna waliokurupuka kutoa ratiba mapema.

Tusishangae kuahirishwa kwa matukio mbalimbali nchini yawe ya michezo, ratiba za mitihani ama jambo lolote, hii ni inadhihirishia ulimwengu jinsi Tanzania tunavyo ongozwa kizembezembe.

Kuhutubia taifa si Jambo dogo wala la mzaha, ndio maana wimbo wa Taifa hupigwa. Hapa JK lazima aje na sababu za msingi kwanini ameahirisha hotuba yake na kuacha watu wengi katika sintofahamu.
 
nyerere ndo alikuwa hafai ndo maana wlikosakosa kumpindua safari tatu

Hakupendwa na aina ya watu jamii ya escrow tunahitaji Rais Tough asiyependwa na mafisi kuliko asiyependwa na umma . Kama Raisi wa leo angekuwa tough kwenye issue Za umma basi tungetegemea misukosuko ya kufanana na Nyerere RIP siyo kupiga cheers na kila aina ya jambazi .lazima tupambane kuirudisha hadhi ya ikulu yetu takatifu
 
Hana cha kuzungumza na watanzania, hasira zetu ni kwenye box la kura.
 
JK%2BMWISHO%2BMWEZI.JPG


Rais Kikwete ameahirisha kulihutubia bunge na 'Wazee wa Dar'; ambapo sasa ataongea nao Jumatatu wiki ijayo(Disemba 22, 2014),Ikulu imethibitisha kuwa na kusema muda utatangazwa.


Rais kikwete leo alitarajiwa kulihutubia taifa kupitia wazee wa mkoa wa Dar es salaam katika mkutano wake ambao ulikuwa ufanyike katika ukumbi wa Hotel ya Blue Pearl,ubungo jijini Dar es salaam.

Katika mkutano wake huo Rais Kikwete alitazamia kuzungumzia mustakabali wa nchini sambamba na kuweka wazi juu ya sakata la utekelezaji wa maazimio nane likiwamo la bunge la kuwawajibisha viongozi waliotajwa katika sakata la uchotwaji wa fedha bilioni 360 katika akaunti ya Tegeta Escrow Pamoja na mambo mengine.

Katika maazimio nane ya bunge yaliyopendekezwa yalitaka viongozi waliotajwa katika ripoti hiyo kwa tuhuma za uchotwaji wa fedha kuchukuliwa hatua za kinidhamu na hata wanapo bainika kufilisiwa mali zao na kushitakiwa katika viombo husika kwa kuonekana kulihujumu taifa katika sakata hilo la uchotwaji wa fedha akaunti ya Escrow.

Rais pia alipanga kuzungumzia juu ya Sekta ya Elimu pamoja na agizo lake la ujenzi wa maabara kwa shule za sekondari nchini,Upigaji kura za maoni kuhusu katiba Mpya utakao fanyika Aprili 30 pamoja na daftari la wapiga kura.

Hata hivyo Katika Hotuba hiyo Rais aliazimia kuelezea uchaguzi wa serikali za Mitaa ulivyo fanyika ambao ulionekana kukumba na dosari kadhaa katika vituo vya kupigia kura katika sehemu mbali mbali za nchi ulipo kuwa ukifanyika uchaguzi huo ambao uliweza kugharimu maisha ya watu kwa kupoteza maisha.

Usije shangaa sura mpya ikawa na singangasinga akirithi mikona ya prof Muhongo make Kama taifa la Tanzania linachezeshwa sindimba hapa timedikia chorus
 
Yeye anaongea na watanzania na sio wazee wa Dar. Kwahiyo hata kama yupo Arusha anaweza akaongea na watanzania tu. Asilete mbwembwe hapa
 
Daaah.. Ninakumbuka ile stori ya Mwalimu kuhusu yule raia wa kigiriki aliekuwa anatangaza kwamba serikali yote ya Tanzania ameiweka mfukoni mwake..

JK ataingia kwenye rekodi ya raisi dhaifu kuliko wote Afrika asipochukua hatua zozote kwa sababu hii ya watu kwenda mahakamani..

Huyu ni zaidi ya dhaifu....ni dhaifuest...goigoi ambaye hawezi mshinda mbio farasi.
 
Ni vizuri ukatumia lugha ya staha kufikisha ujumbe lugha kama hizo unazotumia si nzuri kwa mwendo huo tutakuwa tunajenga taifa la watu wasiyokuwa na adabu kuheshimiana miongoni mwa jamii yetu kutapotea na hiyo inaweza pelekea machafuko nchini kwetu kila kukicha

Toka hapa na wewe mwalimu wa nidhamu na ujenzu wa taifa. Hivi unaongelea nidhamu kwa wapuuzi...sheikh anapoingia na mbwa wake msikitini sie waumini kuonyesha tumemuelewa tunatia maguu na nguruwe ili sheikh azidi kutuheshimu waumini wake.
Acha nidhamu ya woga mkubwa sasa wewe unawaambukiza wanao ujinga kuwaheshimu wapuuzi na majizi.
 
Back
Top Bottom