Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Rais Kibaki amjibu Odinga
Monday, 31 January 2011 19:41 newsroom
NAIROBI, Kenya
RAIS Mwai Kibaki amemjibu Waziri Mkuu Raila Odinga, kuhusiana na madai yake kuwa hakuhusishwa kwenye mchakato wa uteuzi wa nafasi nne za kikatiba. Odinga amemlalamikia Rais Kibaki kwamba hakumshirikisha katika uteuzi wa nafasi nne za Jaji Mkuu, Mwanasheria Mkuu, Mkurugenzi wa Mashitaka na Mkurugenzi wa Bajeti.
Rais Kibaki hivi karibuni alitangaza kuwateua Jaji Alnashir Visram kuwa Jaji Mkuu, Profesa Githu Muigai kuwa Mwanasheria Mkuu, Kioko Kilukumi kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka na William Kirwa kuwa Mkurugenzi wa Bajeti. Hata hivyo akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Makongeni, Nairobi, Odinga alisema; Mimi sitaki kupigana na Kibaki hadharani, nataka kusuluhisha haya maneno kiungwana."
Mawaziri Profesa George Saitoti (Usalama wa Ndani) na Yusuf Haji (Ulinzi), walimjibu Odinga wakidai wamewasiliana na Rais Kibaki ambaye aliwathibitishia kuwa kulikuwa na mazungumzo ya kushauriana kabla ya majina hayo kutangazwa.
Profesa Saitoti pia ni Mwenyekiti wa chama cha PNU ambacho Rais Kibaki ni mwanachama wake na Haji anatoka chama cha Kanu ambacho ni mshirika wa PNU.
Katiba mpya inamtaka Rais kushauriana na Waziri Mkuu kabla ya kufanya uteuzi wa masuala yanayohusu katiba hiyo.
Hata hivyo majina hayo yaliyotangazwa na Rais Kibaki yanatakiwa kupelekwa bungeni kwa ajili ya kupitishwa.
Uteuzi huo umeligawa bunge ambapo wabunge wa PNU na wale wa Kanu wameunga mkono uteuzi wa Rais Kibaki, wakisisitiza kuwa Odinga alishirikishwa, ambapo chama cha ODM kinachoongozwa na Odinga kimepinga uteuzi wa Kibaki.
Monday, 31 January 2011 19:41 newsroom
NAIROBI, Kenya
RAIS Mwai Kibaki amemjibu Waziri Mkuu Raila Odinga, kuhusiana na madai yake kuwa hakuhusishwa kwenye mchakato wa uteuzi wa nafasi nne za kikatiba. Odinga amemlalamikia Rais Kibaki kwamba hakumshirikisha katika uteuzi wa nafasi nne za Jaji Mkuu, Mwanasheria Mkuu, Mkurugenzi wa Mashitaka na Mkurugenzi wa Bajeti.
Rais Kibaki hivi karibuni alitangaza kuwateua Jaji Alnashir Visram kuwa Jaji Mkuu, Profesa Githu Muigai kuwa Mwanasheria Mkuu, Kioko Kilukumi kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka na William Kirwa kuwa Mkurugenzi wa Bajeti. Hata hivyo akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Makongeni, Nairobi, Odinga alisema; Mimi sitaki kupigana na Kibaki hadharani, nataka kusuluhisha haya maneno kiungwana."
Mawaziri Profesa George Saitoti (Usalama wa Ndani) na Yusuf Haji (Ulinzi), walimjibu Odinga wakidai wamewasiliana na Rais Kibaki ambaye aliwathibitishia kuwa kulikuwa na mazungumzo ya kushauriana kabla ya majina hayo kutangazwa.
Profesa Saitoti pia ni Mwenyekiti wa chama cha PNU ambacho Rais Kibaki ni mwanachama wake na Haji anatoka chama cha Kanu ambacho ni mshirika wa PNU.
Katiba mpya inamtaka Rais kushauriana na Waziri Mkuu kabla ya kufanya uteuzi wa masuala yanayohusu katiba hiyo.
Hata hivyo majina hayo yaliyotangazwa na Rais Kibaki yanatakiwa kupelekwa bungeni kwa ajili ya kupitishwa.
Uteuzi huo umeligawa bunge ambapo wabunge wa PNU na wale wa Kanu wameunga mkono uteuzi wa Rais Kibaki, wakisisitiza kuwa Odinga alishirikishwa, ambapo chama cha ODM kinachoongozwa na Odinga kimepinga uteuzi wa Kibaki.