Rais Kagame Kamteua Mtanzania kuwa waziri

Muonekano wake ni mtusi bila shaka yoyote huyo karudi nyumbani mana kazi aliyotumwa kuifanya Bongo alishaimaliza!
 
Kwa style hii, sidhani kama kuna siku tutaruhusu wageni waje kufanya kazi bila kupewa majungu na wenyeweji!! Lakini ndiyo kawaida ya wenyeji, nenda nchi yeyote utakutana na aina hii hii ya malalamiko.
 
Nadhani siye tuliyopo Mipakani hapa wilaya ya kyerwa twawajuwa wengi sana waliokuwa huku kwetu sasa ni wakubwa Rwanda, Nadhani kuna Tatizo la msingi la nchi yetu majungu,kujuana ,kubebana, kulindana n.k, awe na maisha mema huko aliko
 
Hao jamaa wako wengi hapa bongo na kujiita watanzania lakini kiukweli huko ndio kwao. Mmatumbi hawezi kuwa waziri Rwanda kamwe na huo ni mtego tu kuna wengine wamebadili mpaka majina wapo hapa bongo.
 
Profesa huyu ni Mnyarwanda ambaye alisomea huku Tanzania na kuajiriwa pale Chuo Kikuu si huyu tu tuliwahi kuwa na kina Prof Wamba Dia Wamba. Huyu ana makazi yake wilaya ya Missenye katika mji wa BUNAZI na nyumba yake ipo karibu na njia panda ya kwenda Kagera Sugar kwenye barabara ya Bukoba Mutukula.
 
RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.

Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.

Sura nyingine mpya katika Baraza hilo ambalo liliapishwa juzi Ikulu ya Rwanda ni pamoja na Seraphine Mukantabana (Wakimbizi na Menejimenti ya Maafa) na Oda Gasinzigwa (Ofisi ya Waziri Mkuu- Familia na Jinsia).

Akizungumza kwa simu na mwandishi wetu jana, mdogo wa Profesa Rwakabamba, Timothy Rwamushaija anayeishi Dar es Salaam, alisema ndugu yake alizaliwa katika Kijiji cha Bushagara, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

Alisema Profesa Rwakabamba alikuwa Mtanzania aliyeamua kuchukua uraia wa Rwanda na wote baba yao ni Mzee Titus Rwamushaija... “Huyu ni kaka yangu wa tumbo moja na kwa kweli tumefurahi sana kwa mafanikio yake sisi kama wanafamilia.”

Naibu Makamu Mkuu - Taaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), Profesa Makenya Maboko alisema Profesa Rwakabamba alifanya kazi katika chuo hicho na aliondoka akiwa Mkuu wa Kitivo cha Uhandisi.

“Aliondoka wakati Kagame alipoingia madarakani na alikwenda kuongoza Taasisi ya Teknolojia ya Kigali (KIST) kabla ya kwenda katika Chuo Kikuu cha Kigali,” alisema Profesa Maboko.

Msomi huyo alikwenda Rwanda mwaka 1997, baada ya kuombwa na Rais Kagame ambaye alikwenda UDSM kuwaomba baadhi ya wahadhiri kwenda Kigali kufungua chuo kikuu katika taifa lake baada ya kumalizika vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 1994.

Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa kwanza wa KIST na kukifanya kuwa miongoni mwa vyuo bora barani Afrika kwa masuala ya teknolojia jambo lililomfurahisha Rais Kagame.

Baada ya mafanikio hayo, Rais Kagame alimteua kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda, Butare ambako pia alijizolea sifa baada ya kusimamia vyema ujenzi wa mabweni kwa wingi na kiongozi huyo alimtunukia uraia wa nchi hiyo kama zawadi.

Hata hivyo, Profesa Rwakabamba atakuwa amelazimika kuukana uraia wa Tanzania kwa kuwa katiba ya nchi hairuhusu uraia wa nchi mbili.

Profesa Rwakabamba alipata elimu ya msingi huko Muleba na akajiunga na Shule ya Sekondari ya Ihungo.

Baada ya hapo, alijiunga na Chuo Kikuu cha Leeds, Uingereza na kupata Shahada ya Uhandisi mwaka 1971 na 1975 alipata Shahada ya Uzamivu katika fani hiyohiyo.

--------
Hapa JF, kuliwahi kuwa na mjadala juu ya mwanazuoni huyu hapa ---> https://www.jamiiforums.com/celebri...nia-mwanzilishi-wa-kigali-institute-kist.html

Mnamuitaje Mtanzania wakati alishachukua unraia wa Rwanda? Au Tz siku hizi imeridhia uraia pacha? Afer all he looks like a Rwandise guy rather than a Tanzanian.
 
Kamachumu na Muleba kuna watanzania wengi wenye asili hiyo ambao naona mkoa uliisha wapa urai,walikuja siku nyingi kama wafugaji wanitwa Wahima[mwenye kumbukumbu na issue ya Jenerali Ulimwengu]wengi wao walirudi Rwanda baada ya Kagame kuchukua nchi wakiwemo wakina Rwakibamba,bado wapo wengi tu wana mashamba ,mifugo na ni matajiri na wanakubalika kama wenyeji wa Mkoa wa Kagera
 
Wana JF,kule Kagera hasa wilaya ya Muleba na Karagwe kuna muingiliano mkubwa sana wa jamii za wanyarwanda,kwa hiyo kusema hati huyu jamaa ni mtusi,halina mashiko.Ukielekea Bukoba huko utawaona wenye sura za kiganda wapo kibao.Huyu jamaa kweli ni mtanzania wa kweli.Kwani kuukana utanzania ni dhambi? Mwacheni ale BATA WA KIGARI.
 
Mawazo yako si sahihi kabisa ingawa watu wengi wanazo fikra hizo. Ninakuhakikishia kuwa wewe ukitua tu Rwanda kuna watu unafanana nao ambao ni WAHUTU... je kwa kufanana na hao tutasema tutasema wewe ni muhutu??? Naomba nitoe elimu kdg kwa ninalo fahamu:

1. Watu wengi sana wanadhani kuwa mtu mwenye Kufananana na Profesa ni mtusi na wengine kukosea zaidi kwa kusema ni Mnyarwanda. Ukweli ni kuwa kuna watu ambao ni Watanzania kabisa hasa wanaotoka Kagera na baadhi ya sehemu za Kigoma wanafanana na watusi wa Rwanda na Burundi....wengine hata kufanana na Baadhi ya makabila ya Ethiopia nilipokuwa kwa some years. Kufanana huko hatuwezi kusema hao ni watu wa Rwanda au Watusi.

2. Sio wote wenye kufanana na Prof ni Wanyarwanda, Kwakuwa Rwanda kuna makabila makuu mawili ambao ni watusi na Wahutu.... Pia Watusi si kwamba wapo Rwanda tu bali na Burundi. Mfano mwingine ni kwa Masai wa Kenya na Tanzania.

3. WaTZ wengine huwa rahisi kunyosha vidole kwa watu kama hao kuwa ni watusi lakini wengine hata tafsiri ya urai watu hawaijui kabisa. Mimi nina Mdogo wangu alizaliwa nchi ambayo ukizaliwa tu automatically unakuwa raia.... alivyokuja bongo akawa yupo tu na kuendelea na shughuri zake kama raia wa TZ kwa kuwa wazazi wake ni waTZ, lakini baadae ilibidi tumwambie alitakiwa aukane urai wa ile nchi ya magharibi alipofika 18yrs otherwise atakuwa ana uraia wa nchi mbili na bongo haikubaliki.

4. Mbona Wahindi kibao wako Bongo na wengine hata wanauraia wa nchi zingine hatuwanyoshei vidole. Mbaya zaidi walio wengi wanapola mali zenu na kuendelea kuwa maskini kwa kubaki vibarua...

Kwa mazingira ya kibongo na siasa zetu ambazo hazifai, hadi sasa kuna watu kibao nchi zingine na kuomba uraia..... Ukienda hasa Botswana na Rwanda, doctors na Engineers wako kibao wanapiga pesa.
 
ni mtusi aliesoma hapa tanzania.
Ndugu zangu msidanganyike, huyo Prof. Silas Rwakabamba, ni Mtanzania na wala hatuhitaji kujiuliza kama ni Mtusi au nini, maana kwa wabantu na hasa ukifuatilia historia za migration za wananchi wetu, na hasa wa mipakani, utakuta Ancestral origin ni moja. Hivyo si ajabu Mchaga kufanana na Mkikuyu, Mha kufanana na Mrundi na mengine, maana walipodecent kuja huku walikaa maeneo yanayofanana. Maeneo ya Bukoba wana koo za Kitemi mathalani, koo hizi za akina Kasusura, Ruhinda, Rumanyika and so forth, wana origin inayofanana, na hawa hawa akina Bahinda ndio pia wako Rwanda, Burundi na Uganda, but that does not make them Baganda, Barundi or Banyarwanda. Ni vema kuelewa hiyo misingi ya Historia ili kuwaza vema. Hata majina yana aina fulani ya kufanana. Watoro, Wachiga na Wanyankole toka Uganda wanazungumuza sawia na Wahaya na Wanyambo, toka Tanzania, lakini hii haiwafanyi kutokuwa Waganda au Watanzania. Litafakari hilo.
 
Mbona sura yake full mnyarwanda? Nileteeni huyo mdogo wake nimhoji

Supu ya Jiwe: Mawazo yako si sahihi kabisa ingawa watu wengi wanazo fikra hizo. Ninakuhakikishia kuwa wewe ukitua tu Rwanda kuna watu unafanana nao ambao ni WAHUTU... je kwa kufanana na hao tutasema tutasema wewe ni muhutu??? Naomba nitoe elimu kdg kwa ninalo fahamu:

1. Watu wengi sana wanadhani kuwa mtu mwenye Kufananana na Profesa ni mtusi na wengine kukosea zaidi kwa kusema ni Mnyarwanda. Ukweli ni kuwa kuna watu ambao ni Watanzania kabisa hasa wanaotoka Kagera na baadhi ya sehemu za Kigoma wanafanana na watusi wa Rwanda na Burundi....wengine hata kufanana na Baadhi ya makabila ya Ethiopia nilipokuwa kwa some years. Kufanana huko hatuwezi kusema hao ni watu wa Rwanda au Watusi.

2. Sio wote wenye kufanana na Prof ni Wanyarwanda, Kwakuwa Rwanda kuna makabila makuu mawili ambao ni watusi na Wahutu.... Pia Watusi si kwamba wapo Rwanda tu bali na Burundi. Mfano mwingine ni kwa Masai wa Kenya na Tanzania.

3. WaTZ wengine huwa rahisi kunyosha vidole kwa watu kama hao kuwa ni watusi lakini wengine hata tafsiri ya urai watu hawaijui kabisa. Mimi nina Mdogo wangu alizaliwa nchi ambayo ukizaliwa tu automatically unakuwa raia.... alivyokuja bongo akawa yupo tu na kuendelea na shughuri zake kama raia wa TZ kwa kuwa wazazi wake ni waTZ, lakini baadae ilibidi tumwambie alitakiwa aukane urai wa ile nchi ya magharibi alipofika 18yrs otherwise atakuwa ana uraia wa nchi mbili na bongo haikubaliki.

4. Mbona Wahindi kibao wako Bongo na wengine hata wanauraia wa nchi zingine hatuwanyoshei vidole. Mbaya zaidi walio wengi wanapola mali zenu na kuendelea kuwa maskini kwa kubaki vibarua...

Kwa mazingira ya kibongo na siasa zetu ambazo hazifai, hadi sasa kuna watu kibao nchi zingine na kuomba uraia..... Ukienda hasa Botswana na Rwanda, doctors na Engineers wako kibao wanapiga pesa.
 
kuna mwalimu alikuwa anatufundisha geography pale sengerema secondary,huyu mwalimu ni wale wanyarwanda waliokimbilia karagwe miaka ya 50,baada ya vita ya mwaka 94 kuisha alirudi kwao rwanda akapewa ualimu na uraia juu..we are sorrounded,kuna siku kitatokea cha kutokea
 
Back
Top Bottom