Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 741
- 479
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amekutana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Tanzania Bw. Shigeki Komatsubara aliyefika kujitambulisha Ikulu Zanzibar tarehe: 14 Desemba, 2023.
Katika mazungumzo yao wamegusia uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Zanzibar na UNDP pamoja na kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo, uchumi wa buluu, utalii, Mahakama, kujenga uwezo kwa Taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Taasisi ya Afisi ya Rais Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini (PDB) na nyinginezo.
Katika mazungumzo yao wamegusia uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Zanzibar na UNDP pamoja na kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo, uchumi wa buluu, utalii, Mahakama, kujenga uwezo kwa Taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Taasisi ya Afisi ya Rais Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini (PDB) na nyinginezo.