Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Raia waliouawa na polisi si majambazi-RC
2009-04-19 21:39:24
Na Charles Ole Ngereza, Arusha
Sasa imefahamika rasmi kwamba raia wawili waliouawa na polisi kwa risasi wakituhumiwa kuvamia kituo cha mafuta cha Mount Meru mkoani hapa na kupora Sh. 100,000, hawakuwa majambazi.
Hiyo imebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isidori Shirika alipotangaza rasmi jana matokeo ya kamati ya uchunguzi wa mauaji hayo yaliyofanywa na polisi dhidi ya raia wawili mwezi Machi mwaka huu.
Katika tukio hilo, Shedrack Motika (22) na Ewald Mtui (36), waliuawa kwa risasi na polisi waliodaiwa kupigiwa simu kuwa kulikuwa na tukio la ujambazi katika kituo hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Mkoa alisema kuwa tume hiyo imebaini kuwa hakukuwa na tukio la ujambazi lilotokea katika kituo hicho cha mafuta kilichopo katika eneo la Kijenge.
Aidha, Shirima alisema kuwa katika uchunguzi huo, Tume ilipokea maelezo ya wananchi 51 kati yao 33 ni wale waliojitokeza kwa hiari yao kukutana na kamati huku 18 wakiwa ni wale walioitwa mbele ya kamati hiyo.
Shirima alisema katika mkutano na wandishi wa habari kuwa kamati hiyo imeridhika kwamba kuna utata mkubwa katika utoaji na usahihi wa taarifa kuhusiana na tukio hilo.
Alifafanua kuwa kutokana na matokeo ya uchunguzi wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Arusha baada ya kupitia na kuzingatia taarifa ya uchunguzi, imeridhika kuwa taarifa ya uchunguzi huo iwasilishwe katika vyombo vya sheria ili kufanya upelelezi wa kina kwa mujibu wa sheria.
``Tumeona kuwa tukabidhi kwa ofisi ya mwanasheria wa serikali kwa uchunguzi na hatua kuchukuliwa kwa watakaobainika kuwa na makosa,`` alisema Shirima.
Akijibu maswali ya waandishi waliohoji wahusika wa mauaji hayo wako wapi na hatua zipi zitachukuliwa, Shirima alisema kuwa hatma yao itajulikana baada ya ofisi ya Mwanasheria wa Serikali na vyombo vingine vitakapokamilisha uchunguzi.
Aidha Mkuu huyo wa mkoa hakueleza uchunguzi huo utaanza lini kuchunguza ripoti ya kamati na kumaliza lini.
Pia taarifa hiyo ya Mkuu wa Mkoa iliyokuwa na aya nne tu haikueleza kama kulikuwa na utoaji wa taarifa za uongo na ni hatua zipi zitachukuliwa dhidi ya waliobainika kuidanganya kamati hiyo.
Wakati taarifa hiyo ikitolewa jana, ndugu wa marehemu walikuwa nje ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakisubiri nini kitasemwa lakini hata hivyo baada ya kupata fununu walidai kuwa watatoa maoni yao kesho (Jumatatu).
Kamati hiyo iliyotoa matokeo hayo iliundwa na wajumbe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa, ofisi ya mwanasheria wa serikali, mwakilishi wa jamii na jeshi la polisi.
Mauaji ya vijana hao yaliyodaiwa kuwa ya kinyama yalidaiwa kufanywa na polisi yaliyotokea Machi mosi, mwaka huu baada ya mhudumu wa kituo cha mafuta cha Mount Meru kuzozana na marehemu hao.
Katika mzozo huo ambao mhudumu huyo alidaiwa kumtaarifu tajiri yake ambaye naye aliwapigia polisi ambao baadaye waliwaua vijana hao.
SOURCE: Nipashe
2009-04-19 21:39:24
Na Charles Ole Ngereza, Arusha
Sasa imefahamika rasmi kwamba raia wawili waliouawa na polisi kwa risasi wakituhumiwa kuvamia kituo cha mafuta cha Mount Meru mkoani hapa na kupora Sh. 100,000, hawakuwa majambazi.
Hiyo imebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isidori Shirika alipotangaza rasmi jana matokeo ya kamati ya uchunguzi wa mauaji hayo yaliyofanywa na polisi dhidi ya raia wawili mwezi Machi mwaka huu.
Katika tukio hilo, Shedrack Motika (22) na Ewald Mtui (36), waliuawa kwa risasi na polisi waliodaiwa kupigiwa simu kuwa kulikuwa na tukio la ujambazi katika kituo hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Mkoa alisema kuwa tume hiyo imebaini kuwa hakukuwa na tukio la ujambazi lilotokea katika kituo hicho cha mafuta kilichopo katika eneo la Kijenge.
Aidha, Shirima alisema kuwa katika uchunguzi huo, Tume ilipokea maelezo ya wananchi 51 kati yao 33 ni wale waliojitokeza kwa hiari yao kukutana na kamati huku 18 wakiwa ni wale walioitwa mbele ya kamati hiyo.
Shirima alisema katika mkutano na wandishi wa habari kuwa kamati hiyo imeridhika kwamba kuna utata mkubwa katika utoaji na usahihi wa taarifa kuhusiana na tukio hilo.
Alifafanua kuwa kutokana na matokeo ya uchunguzi wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Arusha baada ya kupitia na kuzingatia taarifa ya uchunguzi, imeridhika kuwa taarifa ya uchunguzi huo iwasilishwe katika vyombo vya sheria ili kufanya upelelezi wa kina kwa mujibu wa sheria.
``Tumeona kuwa tukabidhi kwa ofisi ya mwanasheria wa serikali kwa uchunguzi na hatua kuchukuliwa kwa watakaobainika kuwa na makosa,`` alisema Shirima.
Akijibu maswali ya waandishi waliohoji wahusika wa mauaji hayo wako wapi na hatua zipi zitachukuliwa, Shirima alisema kuwa hatma yao itajulikana baada ya ofisi ya Mwanasheria wa Serikali na vyombo vingine vitakapokamilisha uchunguzi.
Aidha Mkuu huyo wa mkoa hakueleza uchunguzi huo utaanza lini kuchunguza ripoti ya kamati na kumaliza lini.
Pia taarifa hiyo ya Mkuu wa Mkoa iliyokuwa na aya nne tu haikueleza kama kulikuwa na utoaji wa taarifa za uongo na ni hatua zipi zitachukuliwa dhidi ya waliobainika kuidanganya kamati hiyo.
Wakati taarifa hiyo ikitolewa jana, ndugu wa marehemu walikuwa nje ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakisubiri nini kitasemwa lakini hata hivyo baada ya kupata fununu walidai kuwa watatoa maoni yao kesho (Jumatatu).
Kamati hiyo iliyotoa matokeo hayo iliundwa na wajumbe kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa, ofisi ya mwanasheria wa serikali, mwakilishi wa jamii na jeshi la polisi.
Mauaji ya vijana hao yaliyodaiwa kuwa ya kinyama yalidaiwa kufanywa na polisi yaliyotokea Machi mosi, mwaka huu baada ya mhudumu wa kituo cha mafuta cha Mount Meru kuzozana na marehemu hao.
Katika mzozo huo ambao mhudumu huyo alidaiwa kumtaarifu tajiri yake ambaye naye aliwapigia polisi ambao baadaye waliwaua vijana hao.
SOURCE: Nipashe