Mgombea Ubunge Jimbo la Kawe kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Halima James Mdee hana usingizi, akitafakari rafu za mapema ambazo inadaiwa anapigwa na wapinzani wake.
Habari zilitua kwenye dawati la Risasi Jumamosi na baadaye kupata
uthibitisho kwa Halima mwenyewe kuwa kuna michezo michafu anafanyiwa
lakini unaomuumiza kichwa ni ule wa kupandikiza wapigakura feki jimboni
kwake.
Habari zinasema kuwa kuna watu feki kutoka maeneo tofauti na Jimbo la
Kawe ambao wanaandaliwa mazingira ya kupiga kura kinyume na utaratibu
uliowekwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) pamoja na muongozo wa
Daftari la Kudumu la Wapigakura.
Akilizungumzia hilo, Halima alisema taarifa za watu kusambazwa ili
kupiga kura kinyume na utaratibu amezipata muda mrefu na anazifanyia
kazi kikamilifu kwa sababu anahisi ni mpango maalum wa kummaliza
kisiasa.
Unajua huu mchezo hauwezi kufanikiwa bila kupata baraka za NEC, hili
nalifuatilia na ndiyo maana nahoji mbona mpaka sasa daftari halijawekwa
hadharani, hii
chelewachelewa inaweza kuambatana na hujuma, alisema Halima na kuongeza:
Siwezi kupuuza taarifa ninazopewa, nafuatilia kuona ukweli wa kile
kinachosemwa. Nitafika mpaka tume kuhakikisha hili halifanikiwi,
kitendo cha kuchukua wananchi Mbagala ili wampigie kura mgombea fulani
ni uhuni na siyo siasa.
Wananchi pia wajue, kama mgombea anataka kushinda uchaguzi kwa kutumia
faulo huyo hawezi kuwa kiongozi bora baadaye. Uadilifu wa mtu lazima
uonekane kuanzia mwanzo hadi mwisho. Na ninasisitiza, hao watu wa
Mbagala na Tandika hawatapiga kura Kawe.
Jimbo la Kawe, ni kati ya majimbo ambayo yameonesha kuwa na upinzani
mkubwa kutokana na kushirikisha wagombea watatu wenye nguvu, Halima,
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Angela Kizigha wa CCM.
Habari zilitua kwenye dawati la Risasi Jumamosi na baadaye kupata
uthibitisho kwa Halima mwenyewe kuwa kuna michezo michafu anafanyiwa
lakini unaomuumiza kichwa ni ule wa kupandikiza wapigakura feki jimboni
kwake.
Habari zinasema kuwa kuna watu feki kutoka maeneo tofauti na Jimbo la
Kawe ambao wanaandaliwa mazingira ya kupiga kura kinyume na utaratibu
uliowekwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) pamoja na muongozo wa
Daftari la Kudumu la Wapigakura.
Akilizungumzia hilo, Halima alisema taarifa za watu kusambazwa ili
kupiga kura kinyume na utaratibu amezipata muda mrefu na anazifanyia
kazi kikamilifu kwa sababu anahisi ni mpango maalum wa kummaliza
kisiasa.
Unajua huu mchezo hauwezi kufanikiwa bila kupata baraka za NEC, hili
nalifuatilia na ndiyo maana nahoji mbona mpaka sasa daftari halijawekwa
hadharani, hii
chelewachelewa inaweza kuambatana na hujuma, alisema Halima na kuongeza:
Siwezi kupuuza taarifa ninazopewa, nafuatilia kuona ukweli wa kile
kinachosemwa. Nitafika mpaka tume kuhakikisha hili halifanikiwi,
kitendo cha kuchukua wananchi Mbagala ili wampigie kura mgombea fulani
ni uhuni na siyo siasa.
Wananchi pia wajue, kama mgombea anataka kushinda uchaguzi kwa kutumia
faulo huyo hawezi kuwa kiongozi bora baadaye. Uadilifu wa mtu lazima
uonekane kuanzia mwanzo hadi mwisho. Na ninasisitiza, hao watu wa
Mbagala na Tandika hawatapiga kura Kawe.
Jimbo la Kawe, ni kati ya majimbo ambayo yameonesha kuwa na upinzani
mkubwa kutokana na kushirikisha wagombea watatu wenye nguvu, Halima,
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Angela Kizigha wa CCM.