Radio Imani, Kwa Neema FM zafungiwa... Clouds FM yatozwa faini!

Status
Not open for further replies.
Inamaana kufungiwa effective midnight today au vipi?

simple hlo la lin itafungwa litakuwa ni moja ya kitu cha kukizungumzia mckilize tu leo kwa makin ikiwezekana mrekod la kujiulza ni kwa nn clauds haikulimwa miez 6 ina maana hzi radio nyingine ni za kimackin au usikose leo saa moja na nusu jion
 
Radio hizi mbili zimefungiwa miezi sita, na Clouds FM kupigwa faini ya milion 7

KWA NEEMA FM Mwanza: Sababu ni kushabikia maswala ya uchinjaji Mwanza

Radio Iman FM Morogoro: Kushabikia watu kutoshiriki Sensa 2012

Clouds FM:
~ Kuendesha/kusabikia masuala ya ushoga wakati wa uchaguzi wa Marekani, kuendesha kipindi cha uchochez wakati wa uchaguzi wa Marekani
~ Kuendesha kipengere cha 'Jicho la ng'ombe' kisichofata maadili

TCRA kitego cha mahudhui ndio kimefanya kazi hii leo

SOURCE: EA radio
Mbona kama likes zimepungua? zilikuwa zaidi ya 15 sasa zimepungua
 
MUNGU hana Mama, Osokoni hebu ondoa upuuzi wako hapa !

Kwahiyo MUNGU aliwaacha watu waliomuumba mwenyewee awauwee kwa kutundikwa msalabani ?

Holly ---- !

Imani yake inamwambia hivyo na yako inakuambia hivyo. Katika ulimwengu wa roho tutaokolewa na imani zetu kila mmoja na aheshimu imani ya mwenzie
 
Neema FM eti nayo wamefungiwa...ha haa haaa. Radio Iman ndiyo walikuwa wanatafutwa.

Kweli siku zote si sawa, Hivi maneno haya umesemewa au ndio wewe Ritz?

Kwa leo tu naungana na wewe 100% na kuweka msisitizo kuwa watu waliohusika na watakaojihusisha huko mbeleni wachukuliwe hatua kama Individuals kama vile waandishi wale wa Genocide Rwanda walivyoshitakiwa kwa uchochezi kupitia taaluma zao, hili jambo la uchochezi lipo wazi siku hizi na sio Radio, Magazeti tu, hili linaonekana sana kwenye mihadhara ya kidini na si polisi wala serikali inayokemea, jipu lilianza taratibu na sasa tayari mgonjwa hapati usingizi sijui itakuwa vipi litakapopasuka
 
Mimi nadhani serikali isiishie kufunga radio moja moja. Waziri wa mambo ya ndani apeleke muswada bungeni - haraka- ili itungwe sheria inayokataza mtu/kikundi cha watu kuhubiri dini isiyo mhusu, kukashfu dini nyingine, mahali popote na kupitia chombo chochote.

Kama mtu ni mkristo aingie kanisani na amazie sala zake huko. Hivyo hivyo kama mtu ni muislam aingie msikitini na kumalizia ibada yake huko. Huku nje tuwe ni watanzania ,chini ya dini moja iitwayo Tanzania ikiongozwa na katiba isiyo na specific dini.

Kwenye sheria, pia iwe ni marufuku kwa mwanasiasa yoyote kuhubiri dini. Kama mtu anaona kuna chama kimekaa kidini apeleke malalamiko yake kwa msajili wa vyama vya siasa, ili naye afanye uchunguzi kwa mujibu wa sheria na kuchukua hatua stahiki pale inapothibitika. Wanasiasa waliofikilisika hoja ni hatari kuliko hata hizi radio zilizofungiwa.

Ni lazima kuwe na sheria inayotuongoza vinginevyo baada ya muda tutajikuta kwenye mtafaruku mwingine tena kama huu. Tuwe na sheria.

Sasa kwani hapo CHADEMA kitasalimika ? Katibu wa Chama - Padri !

Kitafutiliwa mbalii na issue ya kwenda Magogoni msahau tu, hamuwezi
 
Mimi nadhani serikali isiishie kufunga radio moja moja. Waziri wa mambo ya ndani apeleke muswada bungeni - haraka- ili itungwe sheria inayokataza mtu/kikundi cha watu kuhubiri dini isiyo mhusu, kukashfu dini nyingine, mahali popote na kupitia chombo chochote.

Kama mtu ni mkristo aingie kanisani na amazie sala zake huko. Hivyo hivyo kama mtu ni muislam aingie msikitini na kumalizia ibada yake huko. Huku nje tuwe ni watanzania ,chini ya dini moja iitwayo Tanzania ikiongozwa na katiba isiyo na specific dini.

Kwenye sheria, pia iwe ni marufuku kwa mwanasiasa yoyote kuhubiri dini. Kama mtu anaona kuna chama kimekaa kidini apeleke malalamiko yake kwa msajili wa vyama vya siasa, ili naye afanye uchunguzi kwa mujibu wa sheria na kuchukua hatua stahiki pale inapothibitika. Wanasiasa waliofikilisika hoja ni hatari kuliko hata hizi radio zilizofungiwa.

Ni lazima kuwe na sheria inayotuongoza vinginevyo baada ya muda tutajikuta kwenye mtafaruku mwingine tena kama huu. Tuwe na sheria.

hiyo haitowezekana,lazima pawepo na uhuru wa kutoa mawazo na huwezi ukamwekea mtu vikwazo nini aamini na nini asiaamini.
Mfano leo naweza anzisha dini yangu inayoamini chochote ni haki yangu kuhubiri nachokiamini hata kama kitakwenda kinyume na imani ya mwingine.
 
Neema metolewa kafara tuu ili kubalance mambo Radio Imani sio kufungiwa kwa miezi sita walitakiwa kufutwa kabisa!na kwa nn wasifungiwe wakati uleule wanahamasisha watu kutohudhuria sensa wanafungiwa leo??

Wiki ijayo Tanzania Daima sijui utasemaje.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom