pushy parents...

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,845
...wadau,

imekaaje hili la mzazi/wazazi kumchagulia/kumpangia mtoto masomo ya kusoma ili huko mbeleni aje kufanya kazi/taaluma iliyokusudiwa na wazazi?

Nini experience yako katika hili, manufaa/hasara zake?
Nini mtizamo wako kwenye ulezi/malezi hayo?
 
Sometimes mtoto anahitaji mwongozo toka kwa wazazi/walezi. Utakuta wengine wanao uwezo darasani lakini hawana uelewa wa masomo gani wachukue. Hapo walezi wana nafasi ya kuongea nae na kumwelekeza. Mazingira pia yanachangia. Mfano mtoto wa kijijini ukimwambia unataka uwe nani? majibu yake lazima yatatofautiana na mtoto wa mjini,kwahiyo mlezi/mzazi hana budi kumwelekeza kama yeye mwenyewe pia kasoma na kupitia life tofuatitofauti. Anaweza kumpa experience yake kuhusu masuala ya masomo na career development. Lakini sio ile mtoto hawezi hesabu wewe unamlazimisha asome hesabu ili aje kua Computer geek...hiyo sio,utachemsha tu.!
 
Sometimes mtoto anahitaji mwongozo toka kwa wazazi/walezi. Utakuta wengine wanao uwezo darasani lakini hawana uelewa wa masomo gani wachukue. Hapo walezi wana nafasi ya kuongea nae na kumwelekeza. Mazingira pia yanachangia. Mfano mtoto wa kijijini ukimwambia unataka uwe nani? majibu yake lazima yatatofautiana na mtoto wa mjini,kwahiyo mlezi/mzazi hana budi kumwelekeza kama yeye mwenyewe pia kasoma na kupitia life tofuatitofauti. Anaweza kumpa experience yake kuhusu masuala ya masomo na career development. Lakini sio ile mtoto hawezi hesabu wewe unamlazimisha asome hesabu ili aje kua Computer geek...hiyo sio,utachemsha tu.!

...naaam, naaam!

Mtoto wa Kijijini huenda akataka kuwa Mwalimu, kwani ndiye pekee anayeonekana ana hadhi ya kujivunia kwenye jamii...

Lakini cha ajabu, mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi, na Mabalozi wetu na wengineo wengi walizaliwa huko mikoani, wengine vijijini kabisa miaka hiyo.... wengi wao baada ya Tabora school enzi hizo nk... walipitia Makerere na kuendelea kwenye vyuo vikuu nchi mbali mbali duniani na kuishia kufanya kazi za kimataifa i.e Udakitari, nk...

Who pushed them? Mkoloni? jamii ilomzunguka? au juhudi binafsi?

Leo hii unamgharamikia mwanao kuanzia Chekechea, unamlipia primary na secondary education kwenye Academies, lengo lako ni kumpa elimu tu bila matarajio yeyote akishamaliza?

au, Una experience gani binafsi wazazi wako walivyokusukuma kielimu kufikia malengo yao?

Binafsi, ningesikiliza matakwa ya jamii ilokuwa inanizunguka, huenda ningekuwa Dakitari kama ilivyo asilimia kubwa ya ukoo wangu.
 
Mkuu on my side actually mdingi alitaka nisomee udaktari wa binadamu na uwezo nilikuwa nao, lakini deep in my heart sikuona kuwa nina wito, courage na passion wanayotakiwa kuwa nayo madaktari. Mi naogopa hospitali let alone kuattend wagonjwa. So nikaishia nilikoishia
 
Lakini kwa upande mwingine mzazi anaweza tu kushauri na sio kuwa pushy....jukumu langu kwa mfano ni kumpa the best education I can and I hope in the process ataona ni wapi angependa zaidi,, kuna watu wamekuwa maarufu na wametoa michango katika jamii kwa kudefy maagizo ya wazazi wao.
 
Back
Top Bottom