FrankMakange
Member
- Jul 7, 2012
- 9
- 3
Nimejaribu kupitia mada kadhaa kuhusu video inayodaiwa kumuonyesha Mkurugenzi wa Usalama na Ulinzi wa CHADEMA Bw. Wilfred Lwakatare akitoa maelekezo ya kumdhuru mwandishi wa habari - na kuona kuwa waanzishaji/wachangiaji karibu wote waliojaribu kutoa hoja kuhusu video hii imerokodiwa lini wamekuwa na jibu moja tu, Desemba 28, 2012. Nafikiri jibu hili limetokana na jina la video hiyo katika YouTube ambalo ni "VID-20121228-00005"
Bila kujali uhalali wa video husika, ENDAPO jina la video hiyo (VID-20121228-00005) ndio sababu/uthibitisho pekee kuwa video hii imerekodiwa tarehe 28-12-2012, basi nafikiri kuna haja ya kuiangalia upya hoja hii kwani jina la video linaweza kuwa lolote lile kutegemea aliyeiweka hadharani video hiyo anataka iwe na jina gani.
Tunaweza kujenga hoja kuwa jina hili limetokana na jinsi kamera inavyotunza na kuzipa data majina, na mhusika amejisahau lakini pia tukumbuke kuwa inawezekana aliyeiweka video hiyo ameamua kubadilisha sehemu ya jina hilo kwa makusudi kabisa.
Hivyo basi (assuming kila kitu katika video hii ni cha kweli) kimantiki nionavyo mimi ni kuwa; Kama aliyerekodi/ajuaye ukweli wa video hii hatasema ukweli kuwa imerekodiwa lini, basi ni vema na ni sahihi kufikiri kuwa video hii imerekodiwa katika kipindi KATI ya "Bw. Lwakatare alipoingia CHADEMA na kuwa na madaraka yamuwezeshayo kuweka mikakati kama ile AU Mwandishi husika alipoanza kuwa tatizo kwa CHADEMA" NA "Siku video ile ilipowekwa hadharani"
IN SHORT: JINA VID-20121228-00005 SIO UTHIBITISHO KUWA VIDEO IMEREKODIWA TAREHE 28-12-2012
Bila kujali uhalali wa video husika, ENDAPO jina la video hiyo (VID-20121228-00005) ndio sababu/uthibitisho pekee kuwa video hii imerekodiwa tarehe 28-12-2012, basi nafikiri kuna haja ya kuiangalia upya hoja hii kwani jina la video linaweza kuwa lolote lile kutegemea aliyeiweka hadharani video hiyo anataka iwe na jina gani.
Tunaweza kujenga hoja kuwa jina hili limetokana na jinsi kamera inavyotunza na kuzipa data majina, na mhusika amejisahau lakini pia tukumbuke kuwa inawezekana aliyeiweka video hiyo ameamua kubadilisha sehemu ya jina hilo kwa makusudi kabisa.
Hivyo basi (assuming kila kitu katika video hii ni cha kweli) kimantiki nionavyo mimi ni kuwa; Kama aliyerekodi/ajuaye ukweli wa video hii hatasema ukweli kuwa imerekodiwa lini, basi ni vema na ni sahihi kufikiri kuwa video hii imerekodiwa katika kipindi KATI ya "Bw. Lwakatare alipoingia CHADEMA na kuwa na madaraka yamuwezeshayo kuweka mikakati kama ile AU Mwandishi husika alipoanza kuwa tatizo kwa CHADEMA" NA "Siku video ile ilipowekwa hadharani"
IN SHORT: JINA VID-20121228-00005 SIO UTHIBITISHO KUWA VIDEO IMEREKODIWA TAREHE 28-12-2012