Profesa Lipumba kugombea tena urais 2015

mustafa ommy

JF-Expert Member
Feb 8, 2013
221
127
Na Ashton Balaigwa


Lipumba%2830%29%282%29.jpg

Mwenyekiti wa chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba


Makamu wa kwanza wa rais wa Serikali ya Umoja wa kitaifa ya Zanzibar, Seif Shariff Hamad, amemtangaza Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mgombea wa kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu ujao.

Aidha CUF imewatangazia neema Watanzania kuwa endapo itachukua madaraka katika uchaguzi huo itawajaza fedha mifukoni ikiwa ni njia mojawapo ya kuwaondolea umasikini.

Makamu huyo wa kwanza wa rais alisema hayo katika mkutano wa uzinduzi wa oparesheni ya mkachamchaka kuelekea mwaka 2015 (V4C), uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kiwanja cha Ndege, manispaa ya Morogoro.

Alisema Profesa Lipumba bado ni kiongozi shupavu anayestahili kugombea wadhifa huo kupitia CUF katika uchaguzi ujao kwakuwa anakubalika ndani ya chama hicho pamoja na kwa wananchi.

Alisema kuwa operesheni za V4C zilizoanza Mei mwaka jana zitaendelea nchi nzima kwa viongozi wakiongozwa na mwenyekiti wa chama hicho na wafuasi wake kupita kila kata na wilaya mbalimbali wakihamasisha wananchi kukiunga mkono chama hicho.

Makamu huyo wa Serikali ya umoja wa kitaifa alisema kuwa malengo ya CUF ni kujenga umoja wa kitaifa na kuhakikisha kuwa wananchi wote pasipokujali mwenye nacho na asiyekuwanacho wanapata haki sawa na hizo ndiyo sera za CUF.

Kwa upande wake, Profesa Lipumba, akizungumza katika mkutano huo alisema utatifi uliofanywa katika baadhi ya nchi duniani zikiwamo nchi za Brazil na Mexico umebaini kuwa njia nyepesi ya kumuondolea mwananchi umasikini ni kumpatia fedha taslimu.

Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa masuala ya uchumi, alisema jambo hilo linawezekana kufanyika nchini kwa kutumia teknolojia ya simu za mikononi na kuwapo kwa vitambulisho vya taifa vinavyotumia alama za vidole kama alama za ulinzi.

Alisema chama chake kikipewa ridhaa na watanzania ya kuongoza nchi kitatumia raslimali zilizopo nchini za madini, gesi, mafuta, mbuga za hifadhi na maeneo ya utalii kuboresha miundombinu lakini kuwapatia fedha taslimu wananchi ikiwa ni njia rahisi ya kupambana na umasikini.

Ikiwa Profesa Lipumba atagombea tena mwaka ujao, itakuwa ni mara ya tano kwake kwa kuwa amekuwa akiwania nafasi hiyo tangu mwaka 1995 lakini hajawahi kushinda.
 

SIASA

Na Venance George, Morogoro



Posted Jumatatu, Februari 18 2013 saa 10:47 AM

KWA UFUPI

Awali kabla ya kufanyika kwa mkutano huo uliopambwa na shamra shamra za ngoma zilizoanza siku mbili kabla ya uzinduzi huo zikiambatana na baadhi ya wafuasi na wapenzi wa chama hicho kupita katika mitaa mbalimbali ya mji wa Morogoro wakiperusha bendera, uliingia dosari baada ya kutanguliwa na mvua kubwa iliyokwamisha baadhi ya shughuli na kuchelewa kuanza kwa mkutano huo.


CHAMA cha Wananchi (CUF), kimemnadi Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba kugombea kwa mara nyingine kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015, huku yeye binafsi akitangaza neema kwa Watanzania ya kuwajaza fedha mifukoni.

Katika mkutano wa uzinduzi wa operesheni ya mchakamchaka kuelekea mwaka 2015 uliofanyika juzi katika Viwanja vya Shule ya Msingi Kiwanga cha Ndege Morogoro, viongozi wengi wa chama hicho akiwamo Katibu Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, walimnadi Prof Lipumba jukwaani wakidai kuwa bado ni kiongozi anayestahili kugombea wadhifa huo kupitia CUF.

Awali kabla ya kufanyika kwa mkutano huo uliopambwa na shamra shamra za ngoma zilizoanza siku mbili kabla ya uzinduzi huo zikiambatana na baadhi ya wafuasi na wapenzi wa chama hicho kupita katika mitaa mbalimbali ya mji wa Morogoro wakiperusha bendera, uliingia dosari baada ya kutanguliwa na mvua kubwa iliyokwamisha baadhi ya shughuli na kuchelewa kuanza kwa mkutano huo.

Mvua hiyo ilianza kunyesha Saa 9.40 jioni mara baada ya mabasi madogo takriban 15 yaliyowabeba wanachama, wafuasi na viongozi wa CUF kutoka Dar es Salaam kuwasili katika viwanja vya mkutano,hali ambayo iliwalazimu viongozi wa juu kuanza na zoezi la kufungua matawi ya jumuiya za vijana na jumuiya ya akinamama kabla ya kwenda kuhutubia.

Akizungumza katika mkutano huo, Profesa Lipumba alisema utatifi uliofanywa katika baadhi ya nchi duniani zikiwamo nchi za Brazil na Mexico umebaini kuwa njia nyepesi ya kumuondolea mwananchi umasikini ni kumpatia fedha taslimu.

Prof Lipumba ambaye ni mtaalamu wa masuala ya uchumi,alisema kuwa jambo hilo linawezekana kufanyika nchini kwa kutumia teknolojia ya simu za mikononi na kuwapo kwa vitambulisho vya taifa vinavyotumia alama za vidole kama alama za ulinzi.

Alisema India yenye watu zaidi ya bilioni 1.2 imefanikiwa kutumia vitambulisho vya taifa katika masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na uhifadhi na usalama wa fedha zao na hivyo kuwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kuchukua vitambulisho hivyo vinavyotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Mwenyekiti huyo wa CUF alisema chama chake kikipewa ridhaa na Watanzania ya kuongoza nchi kitatumia rasilimali zilizopo nchini za madini, gesi, mafuta, mbuga za hifadhi na maeneo ya utalii kuweza kuboresha miundombinu, lakini kuwapatia fedha taslimu wananchi ikiwa ni njia rahisi ya kupambana na umasikini.

NISHATI YA GESI
Mwenyekiti wa CUF alisema nchi nyingi duniani zilizopata nishati ya gesi na mafuta zimejikuta katika mgogoro mkubwa ikiwa usimamizi wa raslimali hiyo utawanufaisha wachache na kutolea mfano wa Nigeria. Profesa Lipumba alidai kuwa watafiti wamegundua kuwa gesi iliyogunduliwa Mtwara inafuti za ujazo trioni 33, kiwango ambacho kinaweza kuvunwa kwa zaidi ya miaka 10 na kina uwezo wa kuingizia serikali wastani wa pato la Sh 6.5 bilioni (USD 4 milioni) mpaka Sh 8.1 bilioni (USD5 milioni) kwa mwaka.


 
Mgombea wa MAISHA sio wa kudumu. Ni mpaka atakapokufa. Kumbe ndio maana juzi nimewaona kwenye Coaster makabwela wanakwenda upande huo, kumbe walikuwa wanakwenda kujaza mkutano.

Mtatiro atakuwa Waziri Mkuu..tehe tehe tehe!
Duh!wanasafirishana kwa maloli,ili mikutano yao ionekane ina watu wengi,jamaa wamechoka sana!
 
Acha agombee kwani nje ya Lipumba CUF wana nani mwingine anayestahili kugombea cheo hicho?
 
Again??? Bila MPINZANI??? Raha kweli kuwa CUF...
Sasa HIVI wana MACHIMBO ya DHAHABU huko TANGA nadhani watashinda!!!!
 
hahaha!! Lipumba mwanauchumi kweli kweli... tujazie hela babaa.... sitaki ata kujua how! nakuaminia
 
Na Ashton Balaigwa


Lipumba%2830%29%282%29.jpg

Mwenyekiti wa chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba


Makamu wa kwanza wa rais wa Serikali ya Umoja wa kitaifa ya Zanzibar, Seif Shariff Hamad, amemtangaza Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mgombea wa kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uchaguzi mkuu ujao.

Aidha CUF imewatangazia neema Watanzania kuwa endapo itachukua madaraka katika uchaguzi huo itawajaza fedha mifukoni ikiwa ni njia mojawapo ya kuwaondolea umasikini.

Makamu huyo wa kwanza wa rais alisema hayo katika mkutano wa uzinduzi wa oparesheni ya mkachamchaka kuelekea mwaka 2015 (V4C), uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Kiwanja cha Ndege, manispaa ya Morogoro.

Alisema Profesa Lipumba bado ni kiongozi shupavu anayestahili kugombea wadhifa huo kupitia CUF katika uchaguzi ujao kwakuwa anakubalika ndani ya chama hicho pamoja na kwa wananchi.

Alisema kuwa operesheni za V4C zilizoanza Mei mwaka jana zitaendelea nchi nzima kwa viongozi wakiongozwa na mwenyekiti wa chama hicho na wafuasi wake kupita kila kata na wilaya mbalimbali wakihamasisha wananchi kukiunga mkono chama hicho.

Makamu huyo wa Serikali ya umoja wa kitaifa alisema kuwa malengo ya CUF ni kujenga umoja wa kitaifa na kuhakikisha kuwa wananchi wote pasipokujali mwenye nacho na asiyekuwanacho wanapata haki sawa na hizo ndiyo sera za CUF.

Kwa upande wake, Profesa Lipumba, akizungumza katika mkutano huo alisema utatifi uliofanywa katika baadhi ya nchi duniani zikiwamo nchi za Brazil na Mexico umebaini kuwa njia nyepesi ya kumuondolea mwananchi umasikini ni kumpatia fedha taslimu.

Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa masuala ya uchumi, alisema jambo hilo linawezekana kufanyika nchini kwa kutumia teknolojia ya simu za mikononi na kuwapo kwa vitambulisho vya taifa vinavyotumia alama za vidole kama alama za ulinzi.

Alisema chama chake kikipewa ridhaa na watanzania ya kuongoza nchi kitatumia raslimali zilizopo nchini za madini, gesi, mafuta, mbuga za hifadhi na maeneo ya utalii kuboresha miundombinu lakini kuwapatia fedha taslimu wananchi ikiwa ni njia rahisi ya kupambana na umasikini.

Ikiwa Profesa Lipumba atagombea tena mwaka ujao, itakuwa ni mara ya tano kwake kwa kuwa amekuwa akiwania nafasi hiyo tangu mwaka 1995 lakini hajawahi kushinda.

NANI KING'ANG'ANIZI Proffessor LIPUMBA au Maalim SEIF SHARIF HAMAD?
 
Rais! Rais! Rais! Rais! WANADI UHURU WAPO GADO. CHADEMA NA CCM HAWALI HATA WANAWE.
 
Back
Top Bottom