Prof. Shivji aukosoa Mchakato wa Katiba Mpya, aliponda Bunge la Katiba

Mie naona katika hili Shivji hayuko objective,kwanza anaonyesha kuwa ana hofu ya serikali 3, lakini pia anajikanganya anaposema muungano usiangaliwe kwa kigezo cha idadi ya serikali papo hapo anasema alipoombwa kutoa ushauri kwenye Baraza la Wawakilishi alipendekeza muundo wa serikali 2.

Hoja yangu hapo ni kwamba kama muungano hautakiwi kujadiliwa kwa idadi ya serikali mbona na yeye aliuingia mtego huo huo ?
 
Ndio sababu hawakumuweka kwenye tume ya katiba maana angemkosoa live hata Warioba na ToR alizopewa azishikilie!!kile kichwa ni balaa!!!
Mkuu Lambardi, nilitumai, jina la Prof. Shivji baada ya kukosekana kwenye tume, lingeibukia kwenye bunge la katiba!.
Pasco
 
nakubaliana na "Shivji"tulikosea tangu mwanzo,kuna mambo makuu mawili tulitakiwa kuanza nayo, na kupata muafaka wa kitaifa kabla ya kuipa kazi tume ya kukusanya maoni,

1. tulitakiwa kwanza tuwe na referendum juu ya muundo wa muungano.

wananchi wangeulizwa wanataka muundo upi wachague watakaoshinda ndo katiba iandikwe kufuata matakwa ya wananchi

2.tuwe tukubaliane kwenye dira, itakayo tuongoza kutafsri siasa, uchumi

hapa tulitakiwa tuwe makini, kwa sababu nyakati tulizomo zimebadilka sana, na si rahisi kupata majibu ya moja kwa moja kutoka kwa wananchi juu ya mfumo gani unafaa kuendesha uchumi na siasa zetu, hivyo basi baada ya tume ya warioba kukusanya maoni ya wananchi nchi nzima walitakiwa waje na mapendekezo ya "dira"

kwa kifupi, ni hivi kwanza tungepiga kura ya maoni, kuchagua muundo wa muungano, na dira ya taifa
baadaye ndo tungelianza kazi ya kukusanya maoni ya wananchi ni kipi kiingizwe kwenye katiba ya Muundo "A" na dira "B"

au tungelianza na muundo wa muungano, tukafuatiwa na maoni ya wannchi baadaye tukakubaliana juu dira kazi ya kuandika katba mpya ingekuwa rahisi mno.
Amesisitiza dira inatengezwa kwa mjadala wa kitaifa, ili dira hiyo iwe imetokana na wananchi. Kabla ya kuandaa katiba kwanza ni lazima watu waulizwe wanataka kujenga taifa la namna gani, baada ya kujua tunataka nini, ndipo tunaunda tume, kuandaa katiba ya kuitekeza hiyo dira!.

Amesema amemuuliza M/Kiti wa Tume, hayo maoni tunayoyakusanya, ni maoni ya kutengeneza katiba ya kutekeleza nini?, Warioba hana jibu, hivyo tunatengeneza katiba mpya kwa kufuata dira na misingi ya katiba ya zamani kwa sababu Tanzania kama taifa, hatujawahi kukaa chini na kujitafakari, tunataka nini?.

No wonder kuna kiongozi aliulizwa "chanzo cha umasikini wa Tanzania ni nini", akasema "hajui kwa nini Tanzania ni masikini!.

Katiba yetu bado inasema Tanzania ni nchi ya wakulima na wafanyakazi inayofuata misingi ya siasa ya ujamaa na kujitegemea, huku in reality, Tanzania ya leo sio ya wakulima na wafanyakazi na tunafuata misingi ya upapari na soko huria!.
P.
 
Too Late Prof. Shivji you can not change anything now. Watu wako busy na safari ya Dodoma. huyu hakuwa na kigezo cha kushirikishwa kwenye bunge hili? naona angeweza kuleta tofauti.
 
Too Late Prof. Shivji you can not change anything now. Watu wako busy na safari ya Dodoma. huyu hakuwa na kigezo cha kushirikishwa kwenye bunge hili? naona angeweza kuleta tofauti.
Tunaweza kumwingiza kupitia kundi lenye malengo yanayofanana : Wachawi, Wanga, Waganga wa Kienyeji labda.
 
Mie naona katika hili Shivji hayuko objective,kwanza anaonyesha kuwa ana hofu ya serikali 3, lakini pia anajikanganya anaposema muungano usiangaliwe kwa kigezo cha idadi ya serikali papo hapo anasema alipoombwa kutoa ushauri kwenye Baraza la Wawakilishi alipendekeza muundo wa serikali 2.

Hoja yangu hapo ni kwamba kama muungano hautakiwi kujadiliwa kwa idadi ya serikali mbona na yeye aliuingia mtego huo huo ?
Kwa level ya huyu profesa hakustahili kabisa kuujadili muungano bila ya kupata walau kopi ya hati ya mkataba wa muungano.

Kwangu mimi profesa Shivji alitakiwa kuiheshimu taaluma yake.
 
Kufuatia Prof. Shivji kuzungumza tena leo akibonda, kuponda na kuisagasaga tume ya Warioba, nimeona afadhali niwakumbushe tuu kuwa Shivji kubonda na kuponda hakuanza leo!,

Hebu msomeni humu na kumlinganisha na alichosema leo!.

Pasco
 
Salaam,

Kwa wenye access na ITV, Watch ITV now, Prof. Issa Shivji, anashusha mhadhara kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya.

Kwa wale ambao mtakikosa kipindi hiki, angalieni TBC-1 saa 1:30 usiku huu.

Please Watch.

Pasco.

NB. Vipindi hivi vitakujia kila siku saa 1:30 TBC-1 na ITV siku za Alhamisi na Ijumaa saa 1: 00 usiku.

UP DATE
Sehemu ya pili ya mada ya Prof. Shiji na Mchakato wa Katiba Mpya kinaendelea ITV saa hizi na kitakuwepo TBC-1 saa 1:30. Leo Prof. Shivji anajibu maswali ya washiriki.
Karibuni tuendelee.

Shivji anasema msingi mkuu wa katiba ni "dira", huwezi kuingia kwenye mchakato wa katiba mpya bila dira. Mchakato wa kukusanya maoni ulitakiwa utanguliwe na "mjadala wa kitaifa kuweke dira", ndipo sasa tutengeneza katiba inayoendana na hiyo dira!.

Amesema, pamoja na mchakato kuanza bila dira rasmi, lakini wajumbe wa kamati hiyo wana mitazamo, hivyo japo hatuna dira, lakini pia tunaweza kupata katiba nzuri!

Ameitaja misingi mikuu minne ya katiba nzuri, ikianzia na uhuru, haki, usawa, udugu na ujamaa.

Uhuru: Huu ni uhuru wa mtu binafsi, lengo zima la uhuru limejengwa kwenye misingi ya haki za binaadamu, maada ya dhana ya uhuru, pia ni uhuru wa nchi, uhuru wa taifa, uhuru wa jamii!. Kama nchi haiko huru, then watu wake hawawezi kuwa huru!. Japo taifa limepata uhuru wa nchi, yaa independence, lakini taifa hilo likawa halijajikomboa "libarated", huwezi kujidai eti una uhuru!. Zaidi ya nchi kupata uhuru, ili mchi iwe na uhuru wa kweli lazima wawe libarated!. Huwezi kudai uko huru huku unanyonywa na mapepari.

Nchi zinataka uhuru
Mataifa yanataka ukombozi
Watu wanataka mapinduzi!.

Amnezungumzia haki, nimemkosa, sasa anazungumzia usawa "equality before law", watu wote ni sawa, tajiri, masikini, mwanamke mwanaume, mkubwa mdogo, walala heri na walala hoi wote wako sawa mbele ya sheria.

Anatoa hadithi ya kesi ya Martha Wejja, uswa huo unategemea, dira ndio ilitakiwa iamue kuhusu hii misingi

Katiba bora ni ile katiba ambayo chimbuko lake litatoka chini kwa wananchi kwenda juu kwa watawala, katiba hii tuyaitengeneza sasa, misingi imetoka juu kwa watawala na kuletwa chini kwa wananchi!.

Amesisitiza dira inatengezwa kwa mjadala wa kitaifa, ili dira hiyo iwe imetokana na wananchi. Kabla ya kuandaa katiba kwanza ni lazima watu waulizwe wanataka kujenga taifa la namna gani, baada ya kujua tunataka nini, ndipo tunaunda tume, kuandaa katiba ya kuitekeza hiyo dira!.

Amesema amemuuliza M/Kiti wa Tume, hayo maoni tunayoyakusanya, ni maoni ya kutengeneza katiba ya kutekeleza nini?, Warioba hana jibu, hivyo tunatengeneza katiba mpya kwa kufuata dira na misingi ya katiba ya zamani kwa sababu Tanzania kama taifa, hatujawahi kukaa chini na kujitafakari, tunataka nini?.

No wonder kuna kiongozi aliulizwa "chanzo cha umasikini wa Tanzania ni nini", akasema "hajui kwa nini Tanzania ni masikini!.

Katiba yetu bado inasema Tanzania ni nchi ya wakulima na wafanyakazi inayofuata misingi ya siasa ya ujamaa na kujitegemea, huku in reality, Tanzania ya leo sio ya wakulima na wafanyakazi na tunafuata misingi ya upapari na soko huria!.

UP DATE
Sehemu ya pili ya mada ya Prof. Shiji na Mchakato wa Katiba Mpya kinaendelea ITV saa hizi na kitakuwepo TBC-1 saa 1:30. Leo Prof. Shivji anajibu maswali ya washiriki.
Karibuni tuendelee.

Prof. Shivji ameanza na ukosoaji wa Tume ya Katiba, akasema Tume za katiba ziko supposed to be a "professional body" hazikuhitaji uwakilishi, kwenye kukusanya maoni, uwakilishi wa nini?. Amesema, uwakilishi, anahitajika kwenye Bunge la Katiba. Pia ameuliza kwa nchi masikini kama Tanzania, wajumbe 30 wa tume ya kukusanya maoni, "wote hao wa nini?.

Prof. Shivji pia amekosoa bunge la katiba litakaloitishwa, amesema sheria iliyopo inawataja wabunge wote bunge la JMT, na wajumbe wote wa BLW automatically wanakuwa ni wajumbe wa bunge la katiba, akasema "wabunge hawa ni wawakilishi wa wananchi kwa mujibu wa katiba iliyopo, sasa nani kawatuma wajumbe hawa kuwa wawakilishi wa wananchi katika bunge la katiba?. Waunge wote na wawakilishi wote wamechaguliwa kutoka vyama vya siasa. Jee Watanzania wasio wanachama wa chama chochote cha siasa, watawakilishwa na nani?,

Prof. Shivji amesema Bunge la Katiba ni bunge maalum kwa kazi maalum!, Wabunge wa bunge la sasa, hawakupaswa kuwa wajumbe wa bunge la katiba automatically.

Kwa msiojua Katika uundaji wa katiba ya Tanzania ya mwaka 1977, wabunge wa bunge la Tanzania ndio walijitransform na kujigeuza wajumbe wa Constituent assembly, na bunge likajiuza bunge la katiba, likaipitisha katiba ile within 45 minutes!.

Akatoa angalizo, ukujumlisha wabunge wote na wajumbe wote wa BLW katika ujumla wao, wabunge wa chama kimoja peke yao, wanafikia theluthi mbili za kupitisha katiba mpya!.

Prof. Shivji amesema this is a good chance kwa Watanzania kupata katiba bora, ila tusiharakishe, bora tuchelewe lakini tupate katiba yenye uhalali wa kikatiba na uhalali wa kisheria.
We not only need a good constitution, but a constitution which has the constitutionality of a good constitution!-Prof. Shivji.
Pasco

daa huyu professor shivji ni kiboko
 
Salaam,

Kwa wenye access na ITV, Watch ITV now, Prof. Issa Shivji, anashusha mhadhara kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya.

Kwa wale ambao mtakikosa kipindi hiki leo saa hizi hapa ITV, angalieni TBC-1 kesho saa 1:30 usiku.

Please Watch.

Pasco.

NB. Vipindi hivi vitakujia kila siku saa 1:30 TBC-1 na ITV siku za Alhamisi na Ijumaa saa 1: 00 usiku.

UP DATE
Sehemu ya pili ya mada ya Prof. Shiji na Mchakato wa Katiba Mpya kinaendelea ITV saa hizi na kitakuwepo TBC-1 saa 1:30. Leo Prof. Shivji anajibu maswali ya washiriki.
Karibuni tuendelee.

Prof. Shivji anasema msingi mkuu wa katiba ni "dira ya kitaifa ". Anasema huwezi kuingia kwenye mchakato wa katiba mpya bila kuwa na dira ya kitaifa. Mchakato wa kukusanya maoni ulitakiwa utanguliwe kwanza na "mjadala wa kitaifa kuweke dira", ndipo sasa tutengeneza katiba inayoweka dhima ya kuitekeleza hiyo dira!.

Amesema, pamoja na mchakato huu wa katiba kuanza bila dira rasmi, lakini kwa vile baadhi wajumbe wa kamati hiyo ni watu we mitazamo tofauti tofauti na kuna wenye misimamo thabiti, hivyo japo tumeanza bila dira, lakini bado tunaweza kupata katiba nzuri kama mbele ya safari tutajadili dira ya taifa na ikaingizwa!.


Amesisitiza dira inatengezwa kwa mjadala wa kitaifa, ili dira hiyo iwe imetokana na wananchi watu muhimu kabisa wa kwanza ni wananchi na sio viongozi. Kabla ya kuandaa katiba kwanza ni lazima watu waulizwe wanataka kujenga taifa la namna gani, baada ya kujua tunataka nini, ndipo tunaunda tume, kuandaa katiba ya kuitekeza dhima ya hiyo dira!.


Prof. Shivji amesema this is a good chance kwa Watanzania kupata katiba bora, ila tusiharakishe, bora tuchelewe mchakato lakini tupate katiba bora yenye uhalali wa kikatiba na uhalali wa kisheria.

We not only need a good constitution, but a constitution which has the constitutionality of a good constitution!-Prof. Shivji.
Pasco
Wanabodi, msikilize Askofu Gwajima Bungeni Jana

Hicho alichokisema kuhusu Dira, ndicho alichokisema Prof. Shivji hapa,

Hivyo japo kwenye baadhi ya issues Askofu Gwajima anaonekana kama kiazi fulani, Lakini kwenye hoja hii,he is very right.
P
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom