Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,149
Waandishi wa habari 13 wa vyombo mbalimbali, wametangaza kumpeleka mahakamani Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi, huku wakidai anahujumu vyombo vya habari vichanga visijiendeshe.
Wanahabari hao ambao Mengi alitangaza hivi karibuni kuwafungulia mashitaka akidai wanamchafua, wao pia waliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam, kwamba watafungua kesi Machi 23 mwaka huu, ambayo pamoja na mambo mengine, wanataka athibitishe kama wao ni mafisadi kama alivyodai kwenye magazeti yake.
Mwenyekiti wa Kamati ya Waandishi hao, Prince Bagenda, alisema nia ya Mengi kuwaburuta mahakamani ni kutaka kuwadidimiza kimauzo. Pia walisema watamshitaki Mwanasheria Michael Ngalo wa Kampuni ya Uwakili ya Ngalo &Company kwa kuwaita mafisadi wakati akitangaza azma ya mteja wake (Mengi).
Alisema hivi sasa wanashindwa kupata matangazo kutoka kwa watu mbalimbali baada ya magazeti yao kutajwa kuwa yanamilikiwa na mafisadi, jambo ambalo alisema si kweli. Hii ni vita ya kibiashara, soko linaingiliwa na hatupendi vyombo vya habari vichanga viingiliwe, hivyo tunamtaka athibitishe kama kweli sisi ni mafisadi.
Kama ilivyokuwa awali, ingawa ametushitaki kwa kumchafua na sisi tunamshitaki kwa kutuita mafisadi nasi pia atulipe fidia, alisema Bagenda. Bagenda alikishutumu Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT) kuwa hakiwafai wao kama wamiliki wa vyombo vidogo vya habari na hivyo wameamua kuanzisha chao.
Kwa mujibu wa waandishi hao, katika kesi ambayo wanaendelea kushughulikia mchakato wake, wanataka walipwe Sh bilioni 100 kwa maana ya Sh bilioni 50 kwa magazeti matano kila moja Sh bilioni 10. Lakini pia Sh bilioni 50 zingine kwa waandishi, wahariri na wamiliki ambao wanamlalamikia. Magazeti hayo ni Tazama, Taifa Tanzania, Nyundo, Sauti Huru na Umma Tanzania.
Wanahabari hao ambao Mengi alitangaza hivi karibuni kuwafungulia mashitaka akidai wanamchafua, wao pia waliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam, kwamba watafungua kesi Machi 23 mwaka huu, ambayo pamoja na mambo mengine, wanataka athibitishe kama wao ni mafisadi kama alivyodai kwenye magazeti yake.
Mwenyekiti wa Kamati ya Waandishi hao, Prince Bagenda, alisema nia ya Mengi kuwaburuta mahakamani ni kutaka kuwadidimiza kimauzo. Pia walisema watamshitaki Mwanasheria Michael Ngalo wa Kampuni ya Uwakili ya Ngalo &Company kwa kuwaita mafisadi wakati akitangaza azma ya mteja wake (Mengi).
Alisema hivi sasa wanashindwa kupata matangazo kutoka kwa watu mbalimbali baada ya magazeti yao kutajwa kuwa yanamilikiwa na mafisadi, jambo ambalo alisema si kweli. Hii ni vita ya kibiashara, soko linaingiliwa na hatupendi vyombo vya habari vichanga viingiliwe, hivyo tunamtaka athibitishe kama kweli sisi ni mafisadi.
Kama ilivyokuwa awali, ingawa ametushitaki kwa kumchafua na sisi tunamshitaki kwa kutuita mafisadi nasi pia atulipe fidia, alisema Bagenda. Bagenda alikishutumu Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari (MOAT) kuwa hakiwafai wao kama wamiliki wa vyombo vidogo vya habari na hivyo wameamua kuanzisha chao.
Kwa mujibu wa waandishi hao, katika kesi ambayo wanaendelea kushughulikia mchakato wake, wanataka walipwe Sh bilioni 100 kwa maana ya Sh bilioni 50 kwa magazeti matano kila moja Sh bilioni 10. Lakini pia Sh bilioni 50 zingine kwa waandishi, wahariri na wamiliki ambao wanamlalamikia. Magazeti hayo ni Tazama, Taifa Tanzania, Nyundo, Sauti Huru na Umma Tanzania.