Monstgala
JF-Expert Member
- Aug 25, 2009
- 1,079
- 1,034
Mimi ni mmoja wa abiria tuliokuwa tunaelekea kanda ya ziwa leo hii kwa usafiri wa hawa ndugu zetu waliopata kujitengezea reputation nzuri hapa Tz. Katika hali ya kushangaza tumesimamishwa kwenye queue masaa mawili bila ya huduma huku tukiambia hamna network. Baada ya hapo tumecheck-in alafu tumekaa masaa mengine mawili tukiambiwa ndege imechelewa. Alafu ghafla dada mmoja mhusika katukusanya na kutuambia twende lunch kwa sababu hawana uhakika na ndege hiyo tunayoisubiri.
Wakati tukiwa tunaburuzwa kwenda "lunch" dada yule kaingiza habari nyingine kuwa abiria wa Musoma safari leo hamna. Wakati abiria tukiambizana kulikoni mwenzetu mmoja katudokeza kwamba haka kamchezo kapya sasa kana wiki.
Hitimisho: mpaka sasa tupo hapa (masaa matano) tunasubiri hatma yetu na sio siri PrecisionAir wakiendelea hivi reputation waliyoitengeneza kwa muda mrefu itayeyuka na yale ya Air Tanzania yatajirudia.
Wakati tukiwa tunaburuzwa kwenda "lunch" dada yule kaingiza habari nyingine kuwa abiria wa Musoma safari leo hamna. Wakati abiria tukiambizana kulikoni mwenzetu mmoja katudokeza kwamba haka kamchezo kapya sasa kana wiki.
Hitimisho: mpaka sasa tupo hapa (masaa matano) tunasubiri hatma yetu na sio siri PrecisionAir wakiendelea hivi reputation waliyoitengeneza kwa muda mrefu itayeyuka na yale ya Air Tanzania yatajirudia.