Pongezi Kwa Ndege ya Uchumi

Masanilo

Platinum Member
Oct 2, 2007
22,286
4,493
Mkuu napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa ndugu yetu na rafiki yetu kwenye JF, kwa kuweza kufaulu viva voce examination na kutunukiwa shahada ya juu (Doctor of Philosophy) PhD. Najua umehangaika kwa muda mrefu na machapisho yako yamesimama. Hongera sana kamanda, walau wewe umehangaika si kama kilaza Kikwete aliyepewa bila kuhangaika. Hongera Dr Ndege ya uchumi taifa linakuhitaji

Rev Masa K
 
Hongera sana Ndege ya uchumi
Ndo maana naona sasa jina lako limebadilika na kuwa Dr Ndege ya Uchumi am happy fo you man
 
Asanteni sana Mch Masa na FirstLady1, naomba tuendelee kuombeana katika jukumu hili la kulitoa Taifa Mahala hapa na Kulipeleka mahala Pengine

Mungu Awabariki sana
 
Hongera sana Dr wa kweli Ndege ya uchumi kwa kazi nzuri iliyokuwezesha kukamata kitu hiyo. Sasa usisahau kutimiza wajibu wako October 31 na pia kufanya kampeni za mwisho dhidi ya thithiem.

Hongera sana :peace:
 
Hao ndio madokta tunaowataka... sio wa kuchakachuliwa... HONGERA SANA MPIGANAJI, NINA IMANI UTARUDI KULE TUFUFUE LILE JUKWAA LETU LA ELIMU...

HONGERA NDEGE YA UCHUMI
 
hongera sana Dr!Mungu akupe hekima na busara ktk kuchambua na kuchanganua mambo kwa faida ya wana jf na Tz kwa ujumla,Mungu ibariki Tz,mungu ibariki Jf ,mungu mbariki Dr ndege ya uchumi.:peace::peace::peace:
 
Hawa ndo madaktari nchi inayowahitaji si wale jamaa Kamala, Nchimbi, Matayo, Nagu, Makongoro, Kikwete list ni ndefu sana!
 
Back
Top Bottom