Pombe kali zinaongeza sana uzito, ajabu wengi wanafikiri kinyume chake

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,243
12,770
Tanzania ukiifuatilia sana utaona watu wengi wanaangalia mambo kinyumenyume sana. Sijui huwa sababu ni nini?

Pombe(Ethanol) ni sukari iliyogeuzwa kwa fermentation. Pombe ina nguvu kama tu chakula chenye wanga.

Inasemwa kuwa mtu anapokunywa pombe, mwili unaacha kutumia mafuta na wanga kama chanzo cha nguvu na kuanza kutumia pombe. Kwa hiyo mtu akinywa pombe mafuta yanazidi kutunzwa mwilini mwake.

Mahitaji ya nguvu ya mwili wa binadamu kwa siku ni 2,500 kilocalories kwa mwanaume na 2,000 kilocalories kwa mwanamke. Na wastani wa nguvu zilizopo kwenye 100mls za pombe kali(40ABV) ni kama 200kilocalories. Kwa hiyo mtu anayemaliza mzinga wa konyagi anaweza kupata kilocalories 1,000. Karibu nusu ya mahitaji yake ya siku ya nguvu. Hiyo inamaanisha kuwa kiasi kama hicho cha mafuta kitaenda kujijaza mwilini mwake na kuleta unene.

Pia pombe huwa ina tabia ya kuleta hamu ya kula. Ukipiga konyagi na nyama choma au kitimoto au hata ugali maharage, kitambi njenje.

Kwa upande mwingine. Bia hizi lite, moja kwa wastani ina kilocalories 110. Nazo si za kufakamia. Maana ili kuepuka unene mbovu inatakiwa kutozidisha kilocalories 2,500 kwa siku. Sasa ukipiga lite 10 tayari una 1,100Kcal. Bado hujanywa chai, ugali mchana na nyama choma usiku.

So, si kweli kuwa pombe kali zinapunguza unene. Ukweli ni kuwa ni chanzo kikubwa cha unene.
 
Wanaongezeka mwili ni wale wanaokumbuka kula vizuri wakiwa kwenye hzo pombe au kesho yake asubuhi

Lakin ukifatilia wengi wanaokunywa pombe kali hawali vizur,wengine hawali kabisa sasa huko kuongezeka mwili kutatoka wapi
 
Wanaongezeka mwili ni wale wanaokumbuka kula vizuri wakiwa kwenye hzo pombe au kesho yake asubuhi

Lakin ukifatilia wengi wanaokunywa pombe kali hawali vizur,wengine hawali kabisa sasa huko kuongezeka mwili kutatoka wapi
Hao ambao hawali vizuri ni wale walevi choka mbaya. Kama wanywa pombe wangekuwa hawali vizuri usingeona vile vyakula ya mafuta, nyama choma, mishikaki, kitimoto, supu nk vikiuzwa sehemu za pombe.
 
Mtoa mada umeeleza vizuri kabisa, lakini mtazamo wangu ni huu kuhusu ili jambo.

Watu uchagua pombe kali ili wapunguze kiwango cha calories kitachoingia, maana kwa kawaida mtu anayeweza kumaliza konyagi kubwa pekeake huyu anaweza hata kufuta kreti ya s.lite.

Sasa hesabu zako zinasema kwamba konyagi 1 ina 1,000 kcal, akitumia s.lite atakunywa hata 20 ambazo ni 2200 kcal

Bia sukari iliyopo kwenye bia ni nyingi kuliko iliyopo kwenye pombe kali.
 
Mtoa mada umeeleza vizuri kabisa, lakini mtazamo wangu ni huu kuhusu ili jambo.

Watu uchagua pombe kali ili wapunguze kiwango cha calories kitachoingia, maana kwa kawaida mtu anayeweza kumaliza konyagi kubwa pekeake huyu anaweza hata kufuta kreti ya s.lite.

Sasa hesabu zako zinasema kwamba konyagi 1 ina 1,000 kcal, akitumia s.lite atakunywa hata 20 ambazo ni 2200 kcal

Bia sukari iliyopo kwenye bia ni nyingi kuliko iliyopo kwenye pombe kali.
Kuna ukweli, japo unaweza ukifanya hesabu za uwiano, kwamba konyagi kiasi gani ni sawa na lite ngapi utakuta unaingiza kiasi sawa cha calories mwilini. Tofauti itakuwa bei na kasi ya kulewa. Japo hili kwa wanywaji siyo practical.
 
Kila mtu anamalengo yake kimaisha..haiwezekani kuacha kuenjoy vitu uvipendavyo kisa umeme..
 
Back
Top Bottom