Polisi wengi wana utu kuliko raia wengi wanavyowachukulia

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2023
4,974
6,744
Siikatai kuwa kuna Askari Polisi wasio waadilifu! Karibia kila taaluma kuna watu wasiozingatia maadili ya kazi/taaluma zao

Kule nchini Marekani, Polisi mmoja alibaini kuwa leseni ya udereva wa kijana aliyemsimamisha ilikuwa imeisha wakati wake. Alipomwuliza sababu za kuendesha gari huku leseni ikiwa imeshaisha wakati wake, alijitetea kuwa anatokea jimbo jingine nchini Marekani na kilichomfanya awepo hapo ni kusoma chuo. Alikuwa ameachishwa kazi siku chache zilizopita hivyo hakuwa na hela ya kulipia leseni.

Alimjulisha huyo Polisi kuwa alikuwa anaelekea kwenye usaili wa kazi.

Askari Polisi aliuona utetezi wa huyo kijana kuwa una mashiko. Alijikuta njia panda kama amwathibu kwa mujibu wa Sheria au amwache aendelee na safari kinyume cha Sheria.

Baada ya kutafakari kwa muda, aliamua kulipaki pembeni gari lake na kukamata usukani wa gari la huyo kijana na kumpeleka alikokuwa akienda, kwenye usaili.

Walifika eneo la tukio kwa kuchelewa kidogo, kwa hiyo aliamua kuwafuata viongozi wa hiyo Kampuni na kuwaomba radhi kwa kumchekewesha huyo kijana kufika kwenye usaili. Aliwaeleza kilichompelekea kumchekewesha na akaeleweka.

Huyo kijana alifanikiwa kufanya "interview" na kufaulu. Alipata kazi, na pia, alifanyiwa mpango wa kupata leseni ya ya muda wakati akikusanya hela ya kukatia ya kudumu.

Hii habari nimeisoma kwenye mtandao wa Quora.

Ingawa tukio hilo lilitokea Marekani, naamini hata hapa nchini kwetu kuna Askari wengi wema wa kupigiwa mfano.

Ninasema hivyo nikijua ninachomaanisha. Nimeshakutana na wa aina hiyo zaidi ya mara moja.

Tujizoeshe kuyasema mema ya Askari wetu kwa kadiri wanavyojitajidi kutenda kiusahihi.
 
Siikatai kuwa kuna Askari Polisi wasio waadilifu! Karibia kila taaluma kuna watu wasiozingatia maadili ya kazi/taaluma zao

Kule nchini Marekani, Polisi mmoja alibaini kuwa leseni ya udereva wa kijana aliyemsimamisha ilikuwa imeisha wakati wake. Alipomwuliza sababu za kuendesha gari huku leseni ikiwa imeshaisha wakati wake, alijitetea kuwa anatokea jimbo jingine nchini Marekani na kilichomfanya awepo hapo ni kusoma chuo. Alikuwa ameachishwa kazi siku chache zilizopita hivyo hakuwa na hela ya kulipia leseni.

Alimjulisha huyo Polisi kuwa alikuwa anaelekea kwenye usaili wa kazi.

Askari Polisi aliuona utetezi wa huyo kijana kuwa una mashiko. Alijikuta njia panda kama amwathibu kwa mujibu wa Sheria au amwache aendelee na safari kinyume cha Sheria.

Baada ya kutafakari kwa muda, aliamua kulipaki pembeni gari lake na kukamata usukani wa gari la huyo kijana na kumpeleka alikokuwa akienda, kwenye usaili.

Walifika eneo la tukio kwa kuchelewa kidogo, kwa hiyo aliamua kuwafuata viongozi wa hiyo Kampuni na kuwaomba radhi kwa kumchekewesha huyo kijana kufika kwenye usaili. Aliwaeleza kilichompelekea kumchekewesha na akaeleweka.

Huyo kijana alifanikiwa kufanya "interview" na kufaulu. Alipata kazi, na pia, alifanyiwa mpango wa kupata leseni ya ya muda wakati akikusanya hela ya kukatia ya kudumu.

Hii habari nimeisoma kwenye mtandao wa Quora.

Ingawa tukio hilo lilitokea Marekani, naamini hata hapa nchini kwetu kuna Askari wengi wema wa kupigiwa mfano.

Ninasema hivyo nikijua ninachomaanisha. Nimeshakutana na wa aina hiyo zaidi ya mara moja.

Tujizoeshe kuyasema mema ya Askari wetu kwa kadiri wanavyojitajidi kutenda kiusahihi.
Mh! Polisi? Hapana. Mimi hata waliostaafu, huwa sitaki kujihusisha nao maana ni nyoka, ndumila kuwili,
 
Kinyesi ni kinyesi sawa lakini kinyesi cha mtu mzima na kinyesi cha mtoto mdogo ni vitu viwili tofauti kabisa 🤒😎
Amkakumeshakicha ndugu yangu. Unaota ndoto mbaya!
Nilidhani utatoa mfano wa jinsi polisi wetu hawa walivyo wakarimu na wema , kumbe unazungumza mambo ya marekani! 😳.Hawa wa kwetu hapa nia yao ya kuwepo barabarani Huwa ni ama kujipatia chochote kitu kutokana na makosa ya raia, ama kumfurahisha mkubwa furani ndani ya ccm.
 
Siikatai kuwa kuna Askari Polisi wasio waadilifu! Karibia kila taaluma kuna watu wasiozingatia maadili ya kazi/taaluma zao

Kule nchini Marekani, Polisi mmoja alibaini kuwa leseni ya udereva wa kijana aliyemsimamisha ilikuwa imeisha wakati wake. Alipomwuliza sababu za kuendesha gari huku leseni ikiwa imeshaisha wakati wake, alijitetea kuwa anatokea jimbo jingine nchini Marekani na kilichomfanya awepo hapo ni kusoma chuo. Alikuwa ameachishwa kazi siku chache zilizopita hivyo hakuwa na hela ya kulipia leseni.

Alimjulisha huyo Polisi kuwa alikuwa anaelekea kwenye usaili wa kazi.

Askari Polisi aliuona utetezi wa huyo kijana kuwa una mashiko. Alijikuta njia panda kama amwathibu kwa mujibu wa Sheria au amwache aendelee na safari kinyume cha Sheria.

Baada ya kutafakari kwa muda, aliamua kulipaki pembeni gari lake na kukamata usukani wa gari la huyo kijana na kumpeleka alikokuwa akienda, kwenye usaili.

Walifika eneo la tukio kwa kuchelewa kidogo, kwa hiyo aliamua kuwafuata viongozi wa hiyo Kampuni na kuwaomba radhi kwa kumchekewesha huyo kijana kufika kwenye usaili. Aliwaeleza kilichompelekea kumchekewesha na akaeleweka.

Huyo kijana alifanikiwa kufanya "interview" na kufaulu. Alipata kazi, na pia, alifanyiwa mpango wa kupata leseni ya ya muda wakati akikusanya hela ya kukatia ya kudumu.

Hii habari nimeisoma kwenye mtandao wa Quora.

Ingawa tukio hilo lilitokea Marekani, naamini hata hapa nchini kwetu kuna Askari wengi wema wa kupigiwa mfano.

Ninasema hivyo nikijua ninachomaanisha. Nimeshakutana na wa aina hiyo zaidi ya mara moja.

Tujizoeshe kuyasema mema ya Askari wetu kwa kadiri wanavyojitajidi kutenda kiusahihi.
Kuna walio very committed to their responsibilities hata hapa nchini. Mbaya ni pale wanapobanwa kimaslahi na wao kuona njia ya kujikwamua ni pale unapomkamata mvunja Sheria alafu kuna uwezekano wa kufaidika na huyo mvunja Sheria. Tuanzie wapi kuikataa rushwa na ishajenga mizizi ndani ya jamii yetu?
 
Amkakumeshakicha ndugu yangu. Unaota ndoto mbaya!
Nilidhani utatoa mfano wa jinsi polisi wetu hawa walivyo wakarimu na wema , kumbe unazungumza mambo ya marekani! 😳.Hawa wa kwetu hapa nia yao ya kuwepo barabarani Huwa ni ama kujipatia chochote kitu kutokana na makosa ya raia, ama kumfurahisha mkubwa furani ndani ya ccm.
Hii reply yako ilikuwa inamfaa mtoa mada siyo kwenye comment yangu,🤒😎
 
Sisi tunamifumo ya ukandamizaji na uonevu wenevu (huko mbele hakuna rushwa kuna haki kwa asilimia kubwa )

mifumo yetu ndio kipengele
 
Kichwa cha Habari ungesema askari polisi wengi wa marekani na ulaya wana utu kuliko raia wanavyowachukulia....


Sio unasema kwa jumla jumla tu mkuu
Hata hapa kwetu mkuu!

Kuna niliokutana nao sehemu tofauti kwa nyakati tofauti ambao nilitamani kuwapa "soda" kwa jinsi walivyonihudumia kiuadilifu. Walizingatia ucustomer care katika utoaj wa huduma. Wanajali sana kazi zao.
 
Wengi wana weledi na uwezo mkubwa wa kumsoma mtu mapema huwa ni watu sana ila ukiwa na kiburi majivuni ,mjinga au mpumbavu polisi akiliona hilo utaongia cha kike
Mfano mtu anakwambia nimeibiwa na msichana wa kazi ambaye nilimpata baada ya kutoroshwa mkoa fulani,sipajui kwao ,simjui nduguye yoyote afande nisaidie, hapa utamlamu polisi tu,
Mwingine umepata ajali umelewa tii, polisi watasudia utibiwe na utashitakiwa tu
Kifupi polisi wengi licha ya mapungufu mengine ya binadamu wote watu wadizaini hiyo hawatokaa wawavumilie
Hutii sheria unang'anga'na tu umetangaziwa "Jamhuri " inasema tawanyika unagoma kiukweli hapo watakuvunja taya
Huwezi ishi/,deal na polisi ukiwa mpumbavu, mwoga, hujui unajifanya unajua utajua hujui
 
Hata hapa kwetu mkuu!

Kuna niliokutana nao sehemu tofauti kwa nyakati tofauti ambao nilitamani kuwapa "soda" kwa jinsi walivyonihudumia kiuadilifu. Walizingatia ucustomer care katika utoaj wa huduma. Wanajali sana kazi zao.
Niliwahi kumtembelea david misime akiwa RPC DODOMA na kuzungumza nae maswala naweza kusema huyu jamaa ni askari aliyetukuka ingekuwa maamuzi yangu huyu alitakiwa kuwa IGP muda huu
 
Hata hapa kwetu mkuu!

Kuna niliokutana nao sehemu tofauti kwa nyakati tofauti ambao nilitamani kuwapa "soda" kwa jinsi walivyonihudumia kiuadilifu. Walizingatia ucustomer care katika utoaj wa huduma. Wanajali sana kazi zao.
Marekani umetoa mfano uliochukua asilimia 76 ya maandiko ya bandiko lako ila kwa Tz hutaki kabisa kutoa mfano. Unazunguka zunguka tu mkuu.

We ni askari polisi mkuu utakuwa.
 
Moja ya ishara kwamba umekua ni kutambua kwamba ubaya wa mtu hauwakilishi kundi lote alilotoka,wanaotukana polisi wengi wao hata hawajawahi kufanyiwa jambo baya nao.
Kwa sababu ktk kundi la polisi 3 wanaokufanyia ubaya,lazima kuna 1 au 2 watakuwa na msimamo tofauti kukutetea ama kukupunguzia madhira.
 
Sawa siku ifuatayo ,tofautisha police force na police service

ENDAPO marekani askari Huyo angekuwa Chini ya police force sidhani yangefanyika hayo
 
Back
Top Bottom