POLISI WANAMSAKA Abdallah Alila ARUSHA

i pad3

JF-Expert Member
Mar 16, 2012
1,518
378
Polisi wavamia hospitali

Wakati baadhi ya majeruhi wakidai kushuhudia polisi wakiwapiga risasi watu waliokuwa wakimkimbiza mtu aliyerusha bomu katika tukio la Jumamosi, askari hao juzi walifika katika Hospitali ya Seliani saa mbili usiku wakitaka kumchukua mmoja wa majeruhi kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo. Hata hivyo, hawakufanikiwa baada ya mgonjwa kutokomea kusikojulikana baada ya kupata taarifa za kutaka kuhusishwa na tukio hilo.

Ingawa si polisi wala Chadema waliokuwa tayari kumtaja mgonjwa huyo, inaelezwa kwamba majeruhi anayesakwa ni Abdallah Alila aliyekaririwa na vyombo vya habari jana na juzi akidai kumshuhudia aliyerusha boma akiondoka kwenye moja ya magari ya polisi.

Hata hivyo, Kamishna Chagonja jana alisema kwamba jeshi lake linapenda kushirikiana na raia kupata taarifa na si kutumia nguvu katika kukusanya ushahidi wake.


Mwananchi
 
nasikia wameshamchukua na kumpeleka kusikojulikana!

hatujampeleka kusikojulikana,tunaye hapa chumba maarum cha upererezi na mahojiano..Sema tu rituhumiwa hiri la ugaidi meno yake ni magumu mno..

imetolewa na kurugenzi ya habari na mawasiriano,makao makuu.
 
Akamatwe haraka sana kwa kuchafua jeshi la polisi .. kwa nini aongee uongo
 
Kama huyu jamaa kakamatwa atoe ushaidi.......ili isiendelee kuvuruga amani ya nchi kwa kuogea vitu amabavyo havina ushaidi wowote......
 
Tusishirikiane na polisi kabisaaaaaaaaaaaaaa,ni mwisho ,mwisho ,mwisho kabisaaaaaaaaaaaaa.polisi nendeni kwenye ofisi za ccm mkapate ushirikiano.hatuwataki tena tena tena tena tena.mpotee.tutajilinda wenyewe.
 
Ya Mwanahalisi;Ulimboka,Mwakyembe,Mwangosi,Kibanda,Mtwara,Rwakatare zimepita sasa inatamba ya Lema, na sasa tuna CD mpya ya ARUSHA

nchii hiii matukio hayaishi
 
Hiyo Video inayomuonyesha mrusha bomu...irudufiwe mara nyingi na iifadhiwe sehemu mbalimbali....ili isubiri muda muafaka kutolewa.
 
hivi mnajua FBI washakuja mpaka wamechoka, wamesepa zao juzi tu wamefika kwao hata hawapakua nguo kwenye mabegi wanasikia tena bomu jingine Tz Arusha...nahisi safari hii wamegoma kuja au kaka mkubwa awatumie airtz kwenda kuwachukua. :heh:
 
Back
Top Bottom