Polisi wanajua wanalofanya??

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
Napata raha sana kufuatilia kipindi cha Usalama Barabarani kinachorushwa na TBC-1 kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi..sijui kama kipindi hiki kinarekodiwa kwenye matukio la moja kwa moja (live) ambapo madereva wanakuwa hawajajiandaa ama lah, lakini raha nayopata ni pale ninapomwona Inspekta mzima wa Polisi Abel Swai anapojaribu kuelekeza maderva na Abiria Sheria za Barabarani ambazo hata yeye mwenyewe hazifahamu..leo ameniacha hoi anamwambia dereva..wewe unajua kuwa unmevunja sheria za SUMATRA za mwaka 2007 ambazo zinakuzuia usipite root isiyokuhusu?? anawauliza Abiria ..kwa nini mnapitishwa root tofauti *(dereva ametoka posta anapitia barabara ya Ohio kwenda Mwenge na gari yake mbele inasoma " Posta Mwenge ." anasisitiza tena kwa abiria mnaijua wajibu wenu ninyi kama abiria katika ile sheria ya Makosa ya Jinai .. sura ya 16 ya sheria Ya Mgambo inayowataka kutoa taarifa pale dereva anapokiuka sheria???..Sijaelewa hiyo sheria ya Mgambo ila nachujau ni kiuwa Sheria Sura Na. 16 ni Sheria Ya Kanuni za Adhabu (Penal Code). Napata shaka sana na uwezo wa Jeshi letu la Polisi kuhusu uelewa wao wa sheria na ndio maana wanafikia kumshtaki mtu kama
Samson Mwigamba na akina Bw. Absalom Kibanda kwa kuandika makala ya kuchochea askari kutotii sheria ..bila kufahamu kuwa watuhumiwa hao hawana nyazifa zozote nadni ya Serikali au Jeshi za kushawishi jeshi zima kufanya uasi ndani ya Jeshi..na wala pasipo kufahamu kuwa yaliandikwa ili kuwatetea wao wenyewe.
 
Back
Top Bottom