Elections 2010 Polisi wakabidhiwa mbinu za kuiangusha Chadema

Profesy

JF-Expert Member
Jun 24, 2009
385
13
Hii ndio title ya story iliokuepo jana kwenye Mwananchi ikawa inaelezea video moja inaonyesha vikao vya kisiri vinavyofanywa na CCM kupanga mikakati ya kushinda kwa njia yeyote hata kwa kumwaga damu pamoja na silaha walizoagiza na nyaraka za siri zilizochapishwa kwenye karatasi za mikakati hiyo ya ushindi. NOMA!!! :mmph: :ban:.

mwananchi delete.jpg
 
Hii ndio title ya story iliokuepo jana kwenye Mwananchi ikawa inaelezea video moja inaonyesha vikao vya kisiri vinavyofanywa na CCM kupanga mikakati ya kushinda kwa njia yeyote hata kwa kumwaga damu pamoja na silaha walizoagiza na nyaraka za siri zilizochapishwa kwenye karatasi za mikakati hiyo ya ushindi. NOMA!!! :mmph: :ban:.

Tunataka tupate ushahidi wa kina ili tuweze kukubaliana na hili. NO RESEARCH(DATA) NO RIGHT TO SPEAK
 
Tunataka tupate ushahidi wa kina ili tuweze kukubaliana na hili. NO RESEARCH(DATA) NO RIGHT TO SPEAK
If you are so concerned go read the paper. Nakuambia page 13 tena. Ndio nimetoka kuisoma kwa hio kama labda unataka nikuambie nani alikkua quoted ni Basil Lema wa cHADEMA, Stephen Kasidi wa CCM na story imeandikwa na Rehema Matowo kule Moshi.

Angalia mwenyewe if you need proof. I just post what I read sio kuropoka na porojo kama yule jama aliyefukuzwa kama mwalimu mkuu.:mmph:
 
If you are so concerned go read the paper. Nakuambia page 13 tena. Ndio nimetoka kuisoma kwa hio kama labda unataka nikuambie nani alikkua quoted ni Basil Lema wa cHADEMA, Stephen Kasidi wa CCM na story imeandikwa na Rehema Matowo kule Moshi.

Angalia mwenyewe if you need proof. I just post what I read sio kuropoka na porojo kama yule jama aliyefukuzwa kama mwalimu mkuu.:mmph:
tunaweza kupata link ya hii kitu
 
tunaweza kupata link ya hii kitu
Unfortunately website yao ndio aina labda niscan gazeti yenyewe mmuone lakini sio story kwenye site yao hata. Ni mpaka msome Mwananchi ya jana.
 
Sishangai. CCM haijaanza leo kutisha watu wakati wa uchaguzi. Mnayakumbuka mabomu ya machozi waliyomwagiwa wakazi wa Moshi waliofurika mitaani kumlaki Mrema (1995) kabla hajafulia kisiasa wakati huo?

Mimi nilikuwapo Moshi kabla ya siku hiyo, kama mwandishi wa habari. Tulienda kumwona Mkuu wa Mkoa (sikumbuki alikuwa nani wakati huo). Yeye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Mkoa ya Ulinzi na Usalama, kwa hiyo alipaswa kujua iwapo wananchi wangetupiwa mabomu ya machozi na polisi, au la. Kumbe hata yeye walimficha taarifa hizo. Alituambia kungekuwa shwari, lakini siku ya siku, watu walitupiwa mabomu, wengine wakaenda nyumbani kunawa, wengine walijikinga kwa khanga, vitenge na mashati yao.

Mapokezi yale yaliwatisha sana CCM, wakafanya kila hila kuhakikisha hapiti. HAKUPITA!

Kinachotokea leo hakistaajabishi. Ukizoea kula visivyo halali, utakula tu, hata ukiambiwa USILE! Utamwona akukatazaye kuwa adui yako mkubwa.

-> Mwana wa Haki
 
Sishangai. CCM haijaanza leo kutisha watu wakati wa uchaguzi. Mnayakumbuka mabomu ya machozi waliyomwagiwa wakazi wa Moshi waliofurika mitaani kumlaki Mrema (1995) kabla hajafulia kisiasa wakati huo?

Mimi nilikuwapo Moshi kabla ya siku hiyo, kama mwandishi wa habari. Tulienda kumwona Mkuu wa Mkoa (sikumbuki alikuwa nani wakati huo). Yeye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Mkoa ya Ulinzi na Usalama, kwa hiyo alipaswa kujua iwapo wananchi wangetupiwa mabomu ya machozi na polisi, au la. Kumbe hata yeye walimficha taarifa hizo. Alituambia kungekuwa shwari, lakini siku ya siku, watu walitupiwa mabomu, wengine wakaenda nyumbani kunawa, wengine walijikinga kwa khanga, vitenge na mashati yao.

Mapokezi yale yaliwatisha sana CCM, wakafanya kila hila kuhakikisha hapiti. HAKUPITA!

Kinachotokea leo hakistaajabishi. Ukizoea kula visivyo halali, utakula tu, hata ukiambiwa USILE! Utamwona akukatazaye kuwa adui yako mkubwa.

-> Mwana wa Haki
Kweli aise.
 
Sishangai. CCM haijaanza leo kutisha watu wakati wa uchaguzi. Mnayakumbuka mabomu ya machozi waliyomwagiwa wakazi wa Moshi waliofurika mitaani kumlaki Mrema (1995) kabla hajafulia kisiasa wakati huo?

Mimi nilikuwapo Moshi kabla ya siku hiyo, kama mwandishi wa habari. Tulienda kumwona Mkuu wa Mkoa (sikumbuki alikuwa nani wakati huo). Yeye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Mkoa ya Ulinzi na Usalama, kwa hiyo alipaswa kujua iwapo wananchi wangetupiwa mabomu ya machozi na polisi, au la. Kumbe hata yeye walimficha taarifa hizo. Alituambia kungekuwa shwari, lakini siku ya siku, watu walitupiwa mabomu, wengine wakaenda nyumbani kunawa, wengine walijikinga kwa khanga, vitenge na mashati yao.

Mapokezi yale yaliwatisha sana CCM, wakafanya kila hila kuhakikisha hapiti. HAKUPITA!

Kinachotokea leo hakistaajabishi. Ukizoea kula visivyo halali, utakula tu, hata ukiambiwa USILE! Utamwona akukatazaye kuwa adui yako mkubwa.

-> Mwana wa Haki

Rejea kwenye historia zote za hapa ulimwenguni na ujaribu kupata picha halisi ya mabadiliko jinsi yanavyotokea. Kifupi ni kuwa mabadiliko mengi yamemwagisha damu sana na machache tu ndio yamefanyika kiutulivu bila kumwaga au kuvujisha damu. Ni dhahiri kuwa uwizi wa kura utaendelea lakini una mwisho wake. Yawezekana ikawa sio generation yetu ila CCM ndio wanamalizia malizia uongozi wao. Ujio wa Afrika Mashariki nao utaamsha wananchi kwa kiasi kikubwa sana kwani hao wageni waingiao wanaweza shawishi watu sehemu mbali na hata kutoa mbinu kadhaa namna ya kufanya mabadiliko. Tarime wanatambua hili na ndio maana Chambiri hawezi kusimama kwao kabisa. Na sasa naona mwamko maeneo kama Busanda na Biharamulo pia Karatu na Kigoma Kaskazini. Sitashangaa kuskia mwamko maeneo mengine kede kede. Tatizo letu ni kuwa tunangojea hadi damu imwagike ndio tuweze kufanya mabadiliko, tunangojea hadi yatufikie kooni ndio tuanze kulipuka, hatuangalii nini tungependa watoto wetu au wadogo wetu au majirani zetu wajao au walio wadogo waweze kupitia. Kifupi na ukweli ni kuwa ELIMU ndio itatufikisha huko na hii si elimu ya kuingia darasani bali elimu ya ufahamu ambayo inatokana na sababu nyingi tu ikiwemo kukutana na watu toka nchi mbali mbali au mikoa tofauti tofauti. Ukifikiria kuhusu mwanano au mdogo wako nadhani utajua wapi pa kupeleka kura yako au nini cha kufanya. Tanzania sio masikini na hatuwezi kuwa masikini wakati utajiri tumeikalia na unaneemesha hao wachache ambapo mwanao, jirani yako na ndugu yako wananyimwa neema hiyo. Je, ndivyo unapenda iwe hivyo?
 
Back
Top Bottom