Polisi wa trafiki ndio wanaosababisha haya

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,570
19,448
Nimeona picha hii inayohusu ajali ya barabarani hapo Dar. Ingawa maelezo ya picha hayakueleza kama abiria wamepona au vipi, ila nimejiuliza tena chanzo cha ajali hizi na kujidhihirisha kuwa chanzo ni polisi wa trafiki. Askari hao wamekuwa hahangaiki na kuadhibu wavunja sheria za barabarani na mara zote wameng'ang'ania kupokea rushwa na kuwaacha waenedelee kuvunja sheria.

attachment.php
Untitled1.jpg
 
Nimeona picha hii inayohusu ajali ya barabarani hapo Dar. Ingawa maelezo ya picha hayakueleza kama abiria wamepona au vipi, ila nimejiuliza tena chanzo cha ajali hizi na kujidhihirisha kuwa chanzo ni polisi wa trafiki. Askari hao wamekuwa hahangaiki na kuadhibu wavunja sheria za barabarani na mara zote wameng'ang'ania kupokea rushwa na kuwaacha waenedelee kuvunja sheria.
Mwalimu Kichuguu, statement yako iko too definitive kukubalika kiujumla jumla. Ndiyo, ni kweli kwamba mojawapo ya sababu kubwa ya vyanzo vya ajali kwa hapa Tanzania ni rushwa na ukosefu wa maadili ya kikazi ya wanausalama wetu barabarani. Hata hivyo tatizo la ajali hapa kwetu kwa maoni yangu linasababishwa na mengi. Moja ya sababu ya kiujumla ni mmomonyoko wa maadili katika jamii. Sababu nyinginezo ni - ongezeko la magari na idadi ya watumia barabara, ufinyu na uduni wa miundombinu tuliyonayo, pamoja na kuongezeka kwa mwendokasi wa magari ya kisasa.

Picha uliyoiweka kwa hakika inaleta msisimko. Hata hivyo kwa kuwa hapajapatikana maelezo ya kutosha yaliyopelekea ajali hiyo kutokea, na kwamba hakuna maelezo ya majeruhi au maafa katika ajali hiyo; hakika mimi naona si haki kuwalaumu wanausalama wetu kwa kutumia mfano wa picha hiyo hadi pale maelezo ya kutosheleza kuhusiana na ajali yanapokuwepo. Maana picha kama hizi mara nyingi huwa zinaendana na hisia kubwa za majonzi au hasira kwa waliokumbwa. Kwani hatujui kama gari lilikuwa limeibiwa, hatujui kama gari lilifanyiwa service kizembe hivyo kukosa kufunga break, hatujui kama dereva alikuwa amelewa, hatujui kama dereva aliwekewa madawa, n.k. n.k...

Nimetoa mfano wa mmomonyoko wa maadili. Nitauelezea kifupi. Ni kwamba kwa hapa Tanzania na pahala pengi Afrika, maadili ya jamii yanateteleka kutokana na wanajamii kuona kuwa haki hazitendeki. Basi, chuki, visasi na watu kuamua kujifanyia mambo yao wajuavyo hutapakaa. Madereva wetu wanakuwa hawajali tena sheria mabarabarani, kutokana na rushwa au kujua kwamba hamna wafatiliaji wa kuwakamata na kuwaadhibu. Kichuguu, hili ni sawa kabisa na lile uliloelezea wewe hapo juu. Ila, hapo hapo linaweza likapingika, kwani hata kwa wenzetu kwenye nchi zilizoendelea na zenye miundombinu ya kisasa na wanausalama wanaojali maadili ya kazi yao ipasavyo bado ajali hutokea na zinaendelea kutokea.

Kwa mfano huu huu wa mmomonyoko wa maadili, huko kwa wenzetu ajali zinatokea haswa kwa magari yanayoendeshwa na vijana (teenagers). Zinatokea kwani wanakuwa na ile daring mentality. Ni aina ya utomvu wa nidhamu ambao kila jamii inakumbana nao na kila moja ina respond kivyake vyake. Kwao vijana wanakuwa wana test limit za vitu walivyobarikiwa kuwa navyo. Mfano mzuri ni ule unaopelekea hata kuwepo kwa vipindi kama vya jackass na jerry springer. Haya ni matatizo ya jamii na mojawapo ya uwanja wa mapambano ni mabarabarani, kukiwemo joyriding, road rage n.k.

Kwa mfano wa pili, ongezeko la watumiaji wa mabarabara na ongezeko la magari. Mfano huu nadhani unajielezea wenyewe, haswa pale jamii inayohusika inakuwa ile isiyokuwa na taratibu za kuelimisha watumia mabarabara ipasavyo. Hili swala linalenga wastani wa elimu ya jamii kwa ujumla na utumiaji mabarabara na vifaa vipitavyo mabarabarani.

Ufinyu na uduni wa miundombinu na ongezeko la mwendokasi wa magari ni sababu zinazoendana. Pale barabara zinapobakia kuwa zilezile zilizotumiwa na mkoloni, na kubakia zilezile zilizotumiwa na magari ambayo maximum speed ilikuwa 110km/hr. Basi pale panapokuwepo na ongezeko la magari yaendayo kasi zaidi na ongezeko la watumia mabarabara, lakini mabarabara hayo yanabakia kuwa yaleyale ya mwaka 47; lazima migongano itokee. Ajali na misongamano linakuwa jambo la mara kwa mara.

Steve Dii.
 
Nimeona picha hii inayohusu ajali ya barabarani hapo Dar. Ingawa maelezo ya picha hayakueleza kama abiria wamepona au vipi, ila nimejiuliza tena chanzo cha ajali hizi na kujidhihirisha kuwa chanzo ni polisi wa trafiki. Askari hao wamekuwa hahangaiki na kuadhibu wavunja sheria za barabarani na mara zote wameng'ang'ania kupokea rushwa na kuwaacha waenedelee kuvunja sheria.


ooh GOD.....kwa jinsi hii gari ilivyopondwa sidhani kama kuna mtu alitoka hai humo.
hii inaonyesha dhahiri gari ilikuwa katika mwendo mkali sana.
MKUU KICHUGUU,hata ukishusha traffic police kutoka mbinguni kama madereva HAWAKO SENSIBLE na RESPONSIBLE tutaendelea kuyaona haya hadi kesho......
 
lets pray that God was there to save the day when the accident occured and that no one was at least dead!
 
Back
Top Bottom