Polisi Chang'ombe wameanza kuuza "hisa"?

malimwengu

Member
Aug 29, 2011
21
12
Katika hali ya kushangaza polisi kituo cha Chang'ombe wameanza kuuza hisa kwa wahalifu ili nao wawe sehemu ya jeshi hilo.

Hii iko hivi, kuna watu wanatengeneza document feki za kuibia mizigo bandarini na kwenye ma godown mbalimbali. Wakifanya dili hii polisi huabarishwa lakini polisi humuachia mwenye mali. Akishtuka polisi hufanya nae kazi na kuwakamata wahalifu, huchukua pesa kutoka kwa mwenye mali na huchukua pesa kutoka kwa wahalifu na kuwaachia, wote waliowahi kukamatwa na kutoa pesa wameachiwa. Hivi karibuni kuna watu wamekodi gari na kubandika namba bandia kwenda kuiba mzigo, mwenye mali akashtuliwa, akawashtua polisi, jamaa wamekatwa na gari limekamatwa cha kushangaza mwenye gari hajakamatwa bali yupo uraiani ameambiwa atafute milioni tano waweze kumrudishia gari lake na pia akitaka kufanya shughuli zake hizo awaarifu kwanza polisi. Hii dili inapigwa na mtu ambaye namba za gari lake zilitumika anayejulikana kwa jina la Massawe anayeishi Arusha pamoja na OCS CID Chang'ombe.

Jamaa sasa anatafuta hizo milioni tano na ameshaanza kuchangisha ndugu zake ili kununua hisa za kushirikiana na polisi katika uhalifu.

Kumbe kazi ya jeshi la polisi sasa imebadilika kutoka kuwa usalama wa raia na mali zao mpaka kuwa uhakika wa majambazi na kazi zao. Mungu libariki sana jeshi la polisi
 
mh! Hivi kuna ukweli hapa? Kama ni kweli basi jeshi letu la polisi limeingiwa na kansa ya ajabu sana. Usalama wa taifa fanyeni kazi yenu kwa makini katika hili. Kweli taifa linawahitaji sana kuliko ccm inavyowahitaji.
 
mh! Hivi kuna ukweli hapa? Kama ni kweli basi jeshi letu la polisi limeingiwa na kansa ya ajabu sana. Usalama wa taifa fanyeni kazi yenu kwa makini katika hili. Kweli taifa linawahitaji sana kuliko ccm inavyowahitaji.
Kwa askariw a Chang'ombe kufanya hivi mimi wala hainishangazi, pale wapo kibiashara zaidi
 
Haha, hiyo ndo Tanzania zaidi unavyoijua.

Ila mimi nasema kila siku, na nitarudia kusema. Kuandika Jamii forum hapa haitoshi.

Tunatakiwa tuwe na chombo cha habari kisicho_chakachua habari... Mambo kama haya yawekwe hadharani (iTV na TBC hawawezi leta hii habari)...

Kuna siku hawa watawala wetu wataona hii Tanzania ni chungu...tumechoka manyanyaso wakati uko kwenu. Let's wait time will tell
 
Kwani si ndio kituo hiki ambacho mjane alikwenda kuripoti kesi na tajiri ya marehemu mumewe afisa mmoja wa kike akaungana na mshatakiwa kufuta message kwenye simu ya mlalamikaji!
 
ushauri tuanzishe kituo chetu cha Redio
JF REDIO
kazi yake kubwa itakuwa ni kutoa habari kama hizi pasi kutiwa chumvi
 
Hapa Mwanza kuna polisi hatari, wanavaa kiraia na kutumia gari lenye namba za kawaida, zamani wakifahamika kama TZR, ukikamatwa na hiyo mibaunsa usalama wako ni usiwe na pesa kama una japo mil.1 tu umekwisha.
Sasa hivi wanatumia defender ya rangi ya kitani yenye namba T 516 BJU. Hao jamaa nao ni sehemu ya ujambazi.
Tanzania hatuna polisi kabisa.
 
Back
Top Bottom