Penny
JF-Expert Member
- Sep 3, 2008
- 575
- 48
Leo nimekuja na ombi lingine. Hivi mwanamke (mama wa nyumbani)anastahili au hastahili kupewa pocket money ya kujinunulia vitu vyake vidogo mpaka aviorodheshe kwenye list ya vitu vya mwisho wa mwezi! Kwa kweli hili jambo linanishangaza sana kwa huyu bwana maana kupewa hio pesa ni mpaka uiombe kwa nguvu sana ikibidi na ugomvi juu yake. Sasa mume asimpompa mke pesa ategemee akapate wapi! ukiuliza kwa nini hakupi hiyo pocket money kila mwezi anakaa kimya tuu, ukimuuliza haujui kwamba anatakiwa kufanya hivyo anasema anajua. Sasa jamani mtu kama huyu aelewekeje! naombeni msaada tafadhali.