PM Majaliwa: Serikali ya Rais Samia Imetoa Zaidi ya Shilingi Bilioni 208 Kujenga Shule Mpya za Sekondari 184 Nchi Nzima

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,128
49,863
Waziri Mkuu akihutubia Wananchi huko Mtwara amewaambia kwamba Serikali ya Rais Samia Imetoa Zaidi ya Shilingi Bilioni 208 Kwa Ajili ya kujenga Shule Mpya za Sekondari Kwa Kila Halmashauri zote 184 Nchini..

Waziri Majaliwa amesema shule hizo Mpya ni maalumu Kwa Ajili ya kupokea Wanafunzi wa Kidato Cha kwanza mwaka 2024 na kwamba Kila shule Imepata kati ya sh.570mln na 600mln ambazo zinatolewa Kupitia mradi wa Sequip..
.........

SERIKALI imetoa zaidi ya Sh bilioni 208 ili zitumike kujenga shule mpya za sekondari kwenye Halmashauri zote hapa nchini ikiwa ni maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza mwakani.

Naibu Waziri (OR-TAMISEMI), Deogratius Ndejembi amesema wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa aliposimama kusalimia wananchi na watumishi wa Halmashauri ya Mtwara Vijijini kwenye kijiji cha Mkunwa, wilayani Mtwara, mkoani Mtwara.

"Halmashauri zote nchini, ziko 184 zimepatiwa kati ya Sh milioni 570 na milioni 600 za ujenzi wa shule mpya za sekondari. Tumewapa Wakurugenzi hadi Novemba, mwaka huu wawe wamekamilisha ujenzi huo ili waweze kupokea wanafunzi ifikapo Januari, 2024."

Akizungumza na wananchi hao na watumishi mara baada ya kuweka jiwe la msingi, Waziri Mkuu amesema Serikali inatambua kuwa Halmashauri hiyo ni changa na ndiyo maana inapeleka fedha ili kuwawezesha watumishi hao watimize majukumu yao.-Zaidi tembelea


My Take
Hivi Kuna Rais katika Historia ya Tanzania amewahi Jenga shule nyingi Kwa mpigo kama Rais Samia? Mwacheni Rais Samia awafundishe kazi.
 
Nawakumbusha hizo shule hapo Juu ni za O level,Kuna hizi shule Mpya za A level pia
 
Waziri Mkuu angekua na busara pamoja na hekima, basi muda mrefu sana angekua ameshaandika barua ya kujiuzulu Uwaziri Mkuu.

Spana za kichwani muda si mrefu zitaanza kumuangukia.

1) Swala la kuipa TRA budget kubwa kwa muda mfupi, ambayo ni sawa na budget ya Mwendazake kwa takriban miaka 6 alioshikilia Urais. Sio sifa, ni kashfa!

Cha ajabu watu wanajisifia kwamba unapigwa mwingi kwa kuipa TRA budget kubwa kiasi hicho kwa muda mfupi. Wakati ni matumizi na makadirio makubwa kupita kiasi hayo!!!

2) Muswaada wa DP World kuupeleka bungeni kichwa kichwa bila kuchukua maoni huru kutoka kwa wasomi huru (Ma Prof, Ma Dr, Mawakili, Tume Huru Ya kuchunguza Faida/Hasara/Madhara ya kuingia kwenye Mkataba Huo).

Potelea pote kama hawakutaka maoni ya wananchi, ila basi wangechukua ushauri wa Wasomi na wangeunda tume huru kuliangalia swala hilo kwa jicho la tatu.

3) Swala la kujenga shule kwa budget hio sio la kujisifia, hio ni kazi ya Serikali. Sio mpaka mambo ambayo ni lazima serikali kuyafanya kwa wananchi ni kuyatumia kisiasa!

4) Madudu ya budget ya mwaka huu wa fedha huko bungeni yalivyopitishwa, kwa kila Wizara na Serikali kwa ujumla. Budget na Makadirio ni makubwa vibaya mno. Wala Sio ya kujisifia kwa mtu mwenye akili timamu!
 
Hata ajenge maghorofa sisi tunachotaka ni kutuondolea mkataba wa kikoloni.

Yaani kila wakati tunafikiria Mangungo alivyouza nchi tunaona tumerudi kulekule. Ona 👇Mangungo alivyotupiga.
 

Attachments

  • Screenshot_20230702-200427.png
    Screenshot_20230702-200427.png
    187.9 KB · Views: 2
Back
Top Bottom