Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
2009-03-01 13:13:38
Na Mwandishi Maalum, Ireland
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema kuwa mgogoro wa kifedha duniani usiwe kisingizio cha nchi wafadhili kuacha kutimiza ahadi zao za kuzisaidia nchi zinazoendelea.
Katika mhadhara wake kwenye Chuo Kikuu cha Dublin juzi jioni, Waziri Mkuu, alisema kushindwa kutimiza ahadi hizo kutaongeza nyufa za maendeleo kati ya nchi tajiri na masikini.
Alitoa mfano kuwa kuna methali ya Kiswahili nchini Tanzania inayosema: Usipoziba ufa, utajenga ukuta.
Endelea... Mgogoro wa kifedha duniani usiwe kisingizio wafadhili kutusaidia-Pinda
------------------------------------
Hapa Pinda anawambia nini wafadhili ? ..Usipoziba ufa...! Je kuwaachia akina Lowasa na Karamagi na wengine ni kutwambia kuwa watakao kuja itabidi wajenge ukuta ? Maana mpaka leo ni miaka inakatika akina Pinda na wenziwe wanawaburuza waTanzania katika kuuziba ufa huu uliojitokeza maana hata kuuita ufa ni aibu tuliokuwa nao ni mpasuko kabisa ambao upasuko wake unaona mpaka upande wa pili bila ya kuhitaji kuchungulia.
Pinda wajibika hapa nyumbani kwanza ndio hata hao wanaokusaidia au wanaotusaidia wataona jitihada zenu ,msione mnawaburuza WaTanzania mkafikiri na hao wafadhili hawafuatilii ,itakuwa mnajidanganya ,maana wao ndio wanaofuatilia kwa ukaribu na kuyachunguza mambo na kuyajua kwa undani ,usiombe wakifika kutoa ushahidi ,utawala wetu huenda ukaumbuka.
Na Mwandishi Maalum, Ireland
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema kuwa mgogoro wa kifedha duniani usiwe kisingizio cha nchi wafadhili kuacha kutimiza ahadi zao za kuzisaidia nchi zinazoendelea.
Katika mhadhara wake kwenye Chuo Kikuu cha Dublin juzi jioni, Waziri Mkuu, alisema kushindwa kutimiza ahadi hizo kutaongeza nyufa za maendeleo kati ya nchi tajiri na masikini.
Alitoa mfano kuwa kuna methali ya Kiswahili nchini Tanzania inayosema: Usipoziba ufa, utajenga ukuta.
Naomba, mpaka sasa hivi, kuwa msukosuko wa fedha wa kimataifa usiifanye Ireland na nchi nyingine washirika wetu wa maendeleo kuacha kutimiza ahadi zao za misaada ya maendeleo kwa nchi zetu,
alisemaEndelea... Mgogoro wa kifedha duniani usiwe kisingizio wafadhili kutusaidia-Pinda
------------------------------------
Hapa Pinda anawambia nini wafadhili ? ..Usipoziba ufa...! Je kuwaachia akina Lowasa na Karamagi na wengine ni kutwambia kuwa watakao kuja itabidi wajenge ukuta ? Maana mpaka leo ni miaka inakatika akina Pinda na wenziwe wanawaburuza waTanzania katika kuuziba ufa huu uliojitokeza maana hata kuuita ufa ni aibu tuliokuwa nao ni mpasuko kabisa ambao upasuko wake unaona mpaka upande wa pili bila ya kuhitaji kuchungulia.
Pinda wajibika hapa nyumbani kwanza ndio hata hao wanaokusaidia au wanaotusaidia wataona jitihada zenu ,msione mnawaburuza WaTanzania mkafikiri na hao wafadhili hawafuatilii ,itakuwa mnajidanganya ,maana wao ndio wanaofuatilia kwa ukaribu na kuyachunguza mambo na kuyajua kwa undani ,usiombe wakifika kutoa ushahidi ,utawala wetu huenda ukaumbuka.