Peter Msechu: "Kwenye familia yetu mimi ndio model", aeleza kwanini anapenda kuwa kibonge

Primier

Member
Dec 16, 2015
86
14
Msechu-300x194.jpg

Peter-Msechu.jpg


Msechu ambaye ametoa video ya ‘Malava’ hivi karibuni inayoonekana kuwavutia wengi kutokana na jinsi alivyoutumia unene wake kufanya video ifurahishe, amesema kuwa watu inabidi wafahamu kwamba kwenye familia yao yeye ndiye mwembamba kuliko wote.

“Kuna kitu ambacho watu hawafahamu, watu wanaofahamu familia ya mzee Msechu, wajaribu kufatilia watawaambia yaani mimi ndio model,” alisema Msechu kupitia 255 ya XXL. “Yaani mimi na kitambi changu na mwili wangu nilivyo watu wanasema mimi mnene lakini katika familia yetu mimi ndio model, mimi ndio mtu ninayeangaliwa, yaani watu wananiangalia lini nitapungua hata kama Msechu. Sisi tuko hivyo marehemu mama yangu alikuwa yuko hivi, baba yangu amepungua tu kwasababu ya uzee lakini tuna miili.”

Msechu ambaye pia ana kipaji cha kuchekesha hakuacha kuongeza utani kuhusu unene wake kwa kumtania swahiba wake Baba Levo.

“Miili kama hii ni rahisi sana kupata mkopo, ukiwa na mwili kama huu ukiingia nao benki hawakuulizi…lakini sasa una mwili kama Baba Levo, ukienda sehemu kama Ubalozi wa Marekani ukitaka kwenda michongo yako ya nje…lazima upimwe kwasababu watu wanahisi unaweza ukawa na maebola, kwahiyo kidogo kuna sehemu zingine unapenya tunatereza kwasababu kidogo watu wanaona huyu jamaa ana afya ingawa ni wrong perception ya Waafrika wengi.” Alisema Msechu.
 
Huna tv kwako...

Wewe naye kwani unataka kuniazima?
Nitafurahia sana tena na inaitwaje ile DSTV ile naisikiaga kwa tangazo redio za jirani nikipita nayo usisahau kunitumia. Ndio kwanza namsikia leo mie na ushamba wangu wa huku udongo kuinama.
 
Wewe naye kwani unataka kuniazima?
Nitafurahia sana tena na inaitwaje ile DSTV ile naisikiaga kwa tangazo redio za jirani nikipita nayo usisahau kunitumia. Ndio kwanza namsikia leo mie na ushamba wangu wa huku udongo kuinama.
Hahah ntakuazima... mambo mazuri kama haya yasiwe yanakupita
 
Hahah ntakuazima... mambo mazuri kama haya yasiwe yanakupita

He he heeeeeeee yaani kweli unaniazima nilizani utasema unasaidia kutoa msaada. Haya kaabnayo kwanza sina namba ya sanduku la posta kupokelea mzigo mkubwa. Nitaendelea na kusikilizia kwa majirani
 
Duh..nimeona ile video utasema ni Hippopotamus anajaribu kujitikisa.

Muda si mrefu atalazimika kutembea na filimbi, maana akianguka atahitaji msaada wa kuinuliwa.
 
Duh..nimeona ile video utasema ni Hippopotamus anajaribu kujitikisa.

Muda si mrefu atalazimika kutembea na filimbi, maana akianguka atahitaji msaada wa kuinuliwa.
Ha ha ha. Filimbi tena? Nimeona ile video, wimbo ni mzuri na kajitahidi sana. Angejaribu walau arudie ule mwili wake wa kipindi alianza kufahamika kwenye ulimwengu wa muziki. Anakokwenda siko.
 
Huu ni uongo tuu...! Msechu ameshindwa kujicontrol alicho bakiza ni kujitetea kwa migongo ya ndugu zake..
 
Ha ha ha. Filimbi tena? Nimeona ile video, wimbo ni mzuri na kajitahidi sana. Angejaribu walau arudie ule mwili wake wa kipindi alianza kufahamika kwenye ulimwengu wa muziki. Anakokwenda siko.
Yes filimbi ili kama akianguka na hakuna mtu karibu apulize ndio waje kumuinua.....kwa wimbo, yes ni bonge la ngoma baada ya ile ya "Nyota na ing'ae......
 
Msechu-300x194.jpg

Peter-Msechu.jpg


Msechu ambaye ametoa video ya ‘Malava’ hivi karibuni inayoonekana kuwavutia wengi kutokana na jinsi alivyoutumia unene wake kufanya video ifurahishe, amesema kuwa watu inabidi wafahamu kwamba kwenye familia yao yeye ndiye mwembamba kuliko wote.

“Kuna kitu ambacho watu hawafahamu, watu wanaofahamu familia ya mzee Msechu, wajaribu kufatilia watawaambia yaani mimi ndio model,” alisema Msechu kupitia 255 ya XXL. “Yaani mimi na kitambi changu na mwili wangu nilivyo watu wanasema mimi mnene lakini katika familia yetu mimi ndio model, mimi ndio mtu ninayeangaliwa, yaani watu wananiangalia lini nitapungua hata kama Msechu. Sisi tuko hivyo marehemu mama yangu alikuwa yuko hivi, baba yangu amepungua tu kwasababu ya uzee lakini tuna miili.”

Msechu ambaye pia ana kipaji cha kuchekesha hakuacha kuongeza utani kuhusu unene wake kwa kumtania swahiba wake Baba Levo.

“Miili kama hii ni rahisi sana kupata mkopo, ukiwa na mwili kama huu ukiingia nao benki hawakuulizi…lakini sasa una mwili kama Baba Levo, ukienda sehemu kama Ubalozi wa Marekani ukitaka kwenda michongo yako ya nje…lazima upimwe kwasababu watu wanahisi unaweza ukawa na maebola, kwahiyo kidogo kuna sehemu zingine unapenya tunatereza kwasababu kidogo watu wanaona huyu jamaa ana afya ingawa ni wrong perception ya Waafrika wengi.” Alisema Msechu.
jamaa anaimba , Malava ni ngoma kali sana
 
Back
Top Bottom