Pengo: Nchi imeoza!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
Kulingana na gazeti la Majira la leo ASKOFU wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo ameibuka tena na kutangaza mapambano mapya dhidi ya mafisadi huku akidai nchi imeoza na kamwe kanisa halitakaa kimya na kulea hali hiyo.

  • Asema kamwe kanisa halitakubali kunyamaza.
  • Asema watapambana na ufisadi hadi mwisho.
  • Aapa kupambana na yeyote anayetetea uovu.
  • Asema Katoliki haliandai mgombea Urais mwaka 2010.
  • Adai anayeogopa waraka wa Kanisa ni Fisadi.
 
Kulingana na gazeti la Majira la leo ASKOFU wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo ameibuka tena na kutangaza mapambano mapya dhidi ya mafisadi huku akidai nchi imeoza na kamwe kanisa halitakaa kimya na kulea hali hiyo.

  • Asema kamwe kanisa halitakubali kunyamaza.
  • Asema watapambana na ufisadi hadi mwisho.
  • Aapa kupambana na yeyote anayetetea uovu.
  • Asema Katoliki haliandai mgombea Urais mwaka 2010.
  • Adai anayeogopa waraka wa Kanisa ni Fisadi.

Muadhama Cardinal Polycarp Pengo ... tuna separation of church and state ... remember?
 
Muadhama Cardinal Polycarp Pengo ... tuna separation of church and state ... remember?

Kwani unaelewa vipi dhana ya "Separation of Church and State"? Hebu fafanua maana one-liner uliyoposti haitoshelezi. Jee, kukemea Ufisadi Serikalini inahusika vipi na dhana uliyoitaja?
 
Muadhama Cardinal Polycarp Pengo ... tuna separation of church and state ... remember?

Mkuu ni kweli kuna separation ya politics na religious matters. Sina hakika kama maana yako ya Church and State, ina maana Mosque yenyewe haiwi separated na state matters, which in many cases it may seems so.

Lakini where do you draw that line. Mambo ya dini yanaishia wapi na ya siasa yanaingia wapi, ukiangalia kwa undani utaona kuwa ni mstari ambao umechorwa hewani tu. Sioni ubaya kwa kiongozi wa msikiti au kanisa kusema hatutaki viongozi wabovu, mtu akiwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa, diwani, mbunge,waziri au rais anaongoza watu wote bila kujali yeye ni mwanadini au la. Kwa hiyo kama uongozi wake haufai unamwathiri moja kwa moja hata mtu wa dini. Kama serikali inalinda na kupalilia maovu, misikiti na makanisa yatakuwa yanafanya kazi bure, yaani kufinidhs amorals wengine wanafanya tofauti. Wakati wao misikitini na makanisani wanapreach honesty, itakuwa ni upuuzi kama watachekelea ufisadi.

Makamba most of the time amekuwa akiquote Qoran na Biblia anapokuwa kwenye kazi za siasa. Alipokuwa RC hata alikuwa anakwenda misikitini kama RC, kumbuka mwembechai au pale kwa mtoro wakati wanachapana bakora ndani. Mbona yeye hakuwahi kukosolewa kuwa anachanganya siasa na dini?

Are we being hypocritical, or is our system hypocritical? Why should politicians mix politics and religion and why shouldn't clergymen mix religion and politics. Inawezekana Pengo hajui kama dini na siasa haviwezi kuchanganywa?
 
Kulingana na gazeti la Majira la leo ASKOFU wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo ameibuka tena na kutangaza mapambano mapya dhidi ya mafisadi huku akidai nchi imeoza na kamwe kanisa halitakaa kimya na kulea hali hiyo.

  • Asema kamwe kanisa halitakubali kunyamaza.
  • Asema watapambana na ufisadi hadi mwisho.
  • Aapa kupambana na yeyote anayetetea uovu.
  • Asema Katoliki haliandai mgombea Urais mwaka 2010.
  • Adai anayeogopa waraka wa Kanisa ni Fisadi.
Ni kweli nchi imeoza kiasi cha akinapengo kushindwa kuendesha ibada na kuingia katika ulingo wa kisiasa.mafisadi wamekuwa mbele wakidai kupambana na ufisadi ambao kimsingi hawaonekani wanaopambana nao.Inawezekana wanapambana na vivuli vyao.kwani kila tukiwauliza tajeni mafisani wananyamaza.ama kweli nchi imeoza
 
kama kuna separation ya dini na siasa ina maana kama kuna maovu katika siasa wanaotakiwa kupiga kelele ni wanasiasa tu hata wananchi hawatakiwi kulalamika ?nadhani mtu yoyote mwenye uchungu na rasilimali za nchi hii ana haki ya kujumuika katika harakati za ukombozi regardless wa yeye kuwa mtu baki,mchungaji,sheikh,profesa,mwanasheria,nk .tuangalie nini kinalalamikiwa sio nani au anatoka wapi analalamika.Aim ni kuokoa rasilimali za nchi.ni wakati wa kusahau tofauti za dini,kabila,jinsia ,nk na kufocus towards a common goal-kupigana na ufisadi
 
pengo amenena.........lakini wasiopinga sio tu mafisadi bali pia hata vyama ambavyo ni taasisi za dini kama cuf zinapinga waraka wa kanisa lakini zinaunga mkono mwongozo wa waislamu.
 
Muadhama Cardinal Polycarp Pengo ... tuna separation of church and state ... remember?
Yes but kumbuka Serikali haina dini ila walioko madarakani wana dini na wale wanaoongozwa nao wana dini zao. Na ndiyo maana kila mara baadhi ya viongozi wa kiserikali huwa wana"quote" vitabu vitakatifu. Hivi tatizo ni kilichosemwa AU aliyesema???? If we can not diferentiate the two, KILICHOSEMWA NA ALIYESEMA, we will be narrowing our minds. BY THE WAY, WHERE DO YOU DRAW THE church and state SEPARATION LINE???
 
pengo amenena.........lakini wasiopinga sio tu mafisadi bali pia hata vyama ambavyo ni taasisi za dini kama cuf zinapinga waraka wa kanisa lakini zinaunga mkono mwongozo wa waislamu.
Huo mwongozo una vipengere vimekaa vizuri lakini vile vile kuna vipengere vimeka vibaya. Hebu tazama kipengere kinachohimiza waislamu kuwachagua waislamu wenzao as if wanachagua IMAMU/SHEHE
 
Ni kweli nchi imeoza kiasi cha akinapengo kushindwa kuendesha ibada na kuingia katika ulingo wa kisiasa.mafisadi wamekuwa mbele wakidai kupambana na ufisadi ambao kimsingi hawaonekani wanaopambana nao.Inawezekana wanapambana na vivuli vyao.kwani kila tukiwauliza tajeni mafisani wananyamaza.ama kweli nchi imeoza

Na mtasema sana mwaka huu mpaka midomo iende upande.

Tatizo kubwa ktk Tz yetu ni watu kupenda free lunch na kutozishirikisha akili ktk mambo mbalimbali. Mojawapo ya wapenda free lunch wakubwa ktk nchi yetu ni baadhi ya ndugu zetu wasilamu..yes I said it. Na chuki yao kwa Pengo na kwa Kanisa Katoliki ni pale waraka wa Kanisa Katoliki ulipolonga wazi na bayana kuwa SERIKALI ISIGHARAMIKIE IBADA YA DINI MOJA TU HUSUSAN MAHAKAMA YA KADHI. Hili limewauma sana ndugu zetu wapenda free lunch, ila tumeshawajua kuwa ni ukosefu tu elimu na busara ndio mzizi wa matatizo yao yote. Wataendelea kutokwa na povu kwa husda na chuki isiyo na msingi lakini UKWELI UNAUMA na makelele yao yanadhihirisha ukweli kweli wachoma!

 
Huku tunakokwenda hakufai. Nitatoa mfano.

Mie kama mtoto wa kiislam sitakiwi kula nguruwe, dini inasema ni haramu. Kuacha kwangu kula nguruwe sio kwa sababu niko allergic nayo, au ninaumwa. The decision is completely based on on faith kwamba nikila kiti moto ninapata dhambi. I stopped reasoning about manufaa ya kiti moto like bei yake rahisi kuliko mbuzi, au ng'ombe, pia kiti moto kina protein za kutosha. Hizo zote faida za kiti moto sizifikirii kwa sababu naogopa Jehanamu. Essentially my faith has hijacked my own reasoning power.

My point is, hawa viongozi wa dini wakianza kuongelea siasa--they are subliminally imposing faith mandate for their waumini to follow what they are preaching, in this time sio Yohana mtakatifu tena bali ni siasa. Wakatoliki are soon going to give up their reasoning power and vote for whoever Kardinali Pengo is endorsing between those lines. Not because they want to, but because Pengo said that is what GOD and Jesus wants to. That is what Waraka is intentionally supposed to be interpreted na waumini.

It is a very dangerous trajectory for our country because once the debate is shifted to udini, the risks for conflict will increase and we are already masikini--the last thing we want is people to be voting in 2010 because of dini au ukabila. Unfortunately when shit hit the fan kardinali Pengo anakwenda zake Vatican kutulia na kutuachia msala nchini kwetu.

Ya Kaisari muachie Kaisari Kardinali Pengo, huko unakotupeleka hatutaki.
 
My point is, hawa viongozi wa dini wakianza kuongelea siasa--they are subliminally imposing faith mandate for their waumini to follow what they are preaching, in this time sio Yohana mtakatifu tena bali ni siasa. Wakatoliki are soon going to give up their reasoning power and vote for whoever Kardinali Pengo is endorsing between those lines. Not because they want to, but because Pengo said that is what GOD and Jesus wants to. That is what Waraka is intentionally supposed to be interpreted na waumini.

It is a very dangerous trajectory for our country because once the debate is shifted to udini, the risks for conflict will increase and we are already masikini--the last thing we want is people to be voting in 2010 because of dini au ukabila. Unfortunately when shit hit the fan kardinali Pengo anakwenda zake Vatican kutulia na kutuachia msala nchini kwetu.

Ya Kaisari muachie Kaisari Kardinali Pengo, huko unakotupeleka hatutaki.

Uliyoyasema yoote ni hisia tu..hivi unaweza kuonesha ni wapi Pengo amemu-endorse mtu yeyote kwenye nafasi yeyote ya kisiasa?
 
Nikweli unachosema Pengo naomba utupe mwongozo,ukizingatia chanzo chaufisadi,uwajue mafisadi ni nani,pia uanzie humo ndani ya kanisa kuwa fichua nautangaze kabisa.watu wamtanbue ndani ya kanisa,kama kanisa mpaka leo sijasikia mkimtenga muumini kwa kuwa fisadi inakuwa vipi unatangaza una pingana na ufisadi kwa maneno badala ya kwa vitendo.usizungumze ili kuonekana unazungumza jaribuni kutenda.
 
Kuna haja ya kuwa viongozi wa dini makini kama Wakina Pengo wansema bila ya kuogopa kabisa ni kweli kabisa kuwa Nchi imeoza
 
Kwani ni uongo nchi haijaoza???? na ni nani na nani anaeruhusiwa kuusema uovu huo, na nani haruhusiwi?? acheni udini hapa vitu vya kweli lzm visimame kwenye ukweli na vijadiliwe vitu visivyo faa pia vijadiliwe acheni kubagua kisa dini, kila mtu anatakiwa akemee ufisadi..sio mwislamu au mkristo wote tunatakiwa tuukemee..Desmond Tutu ange kataliwa kuongelea ubaguzi SA ingekuwa pale ilipo leo???
 
all in all...mie nafurahia hili vuguvugu la NYARAKA na MIONGOZO....natamani sana UDINI uote mizizi kisha TUPIGANE VITA vya udini au hata usiasa na ukabila ...KISHA MAENDELEO YA KWELI YAJE NCHINI MWETU KWA WATAKAOBAKI...kuliko kuendelea kuchekacheka na wapuuzi wachache wananufaika na rasilimali zetu.

NDIOOOO....kwani ni nchi gani iliyoendelea duniani ukianzia hiyo USA ambayo haikuwaua/kuuana/ kumwaga damu NDIPO IKAPATA MAENDELEO YA KWELI?

WATANZANIA acheni uoga wa kitoto...RWANDA NA BURUNDI WALITIANA ADABU NA WAMEANZA KUENDELEA KWA KASI...sie tunajivunia uhuru/amani na upendo ambavyo ki-halisia ni NIDHAMU YA WOGA NA KUOGOPANA...matokeo yake wapuuzi wachache aka MAFISADI wanatufanya watz wote wapumbafu na wapuuzi.

NO WAR...NO REAL PC N HARMONY..NO CIVILISATION/MAENDELEO YA KWELI at all.

nb:- ni maoni yangu na nasikitika kuwaambieni UKWELI na UKWELI TUPU watanzania wenzangu...EHEE MWENYEZI MUNGU NISAIDIE.
 
Back
Top Bottom