Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Pemba kwachafuka
Askari wapigwa mawe, Maalim Seif atuhumiwa
na Mwandishi Wetu, Pemba
HALI ya amani kisiwani Pemba si shwari, baada ya jana kuibuka vurugu kubwa zilizosababisha nyumba ya sheha kuchomwa moto, polisi kurushiwa mawe na watu saba kukamatwa, kwa madai ya kuwazuia watu kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Vurugu hizo zimetokea baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kuanza zoezi hilo ililolisimamisha mwezi uliopita kutokana na kuwapo kwa vurugu zilizosababishwa na baadhi ya watu wanaodai mizengwe kutawala katika uandikishaji wa watu kwenye daftari hilo.
Mamia ya watu walijitokeza katika vituo vya uandikishaji wapiga kura, lakini hawakusogea kwa makarani kuandikishwa, huku wengine wakipambana na polisi kwa matusi na kurushiana mawe walipotakiwa waondoke vituoni kama hawakuwa tayari kujiandikisha.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Yahya Rashid Hemed, alilazimika kufika katika kituo cha Kiuyu, Minungwini na askari wa ziada wapatao 20 wenye silaha na mabomu ya machozi kuungana na askari wapatao 50 wa polisi, KMKM, Magereza na Usalama wa Taifa, ambao walionekana kushindwa kuidhibiti hali.
Polisi walipojaribu kutumia nguvu na kutisha watu kwa mtutu wa bunduki, ndipo wananchi walipoanza kurusha mawe, ambapo Kamanda Yahya, alilazimika kufanya kazi ya ziada kutuliza jazba za wananchi.
Vurugu hizo kwa kiasi kikubwa zimetokana na baadhi ya wananchi kudai kuwa wengi wao hawana vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi, ambavyo ndivyo vinavyotumika kama kigezo cha kuandikishwa.
Hali ya vurugu ilianza kujitokeza katika vituo vya uandikishaji vya Kambini na Minungwini katika Jimbo la Ole, ambapo wanachama wa CCM walipokuwa wakijaribu kwenda katika vituo vya kuandikishwa, makundi ya watu yaliyokuwa karibu na vituo yalionekana kupinga na kusababisha zoezi hilo kutokwenda vizuri.
Askari polisi na wa Kikosi cha Kujenga Uchumi (JKU) walionekana kuimarisha ulinzi katika kituo cha uandikishaji Kambini, lakini ulinzi huo haukusaidia kitu, baada ya wananchi wenye jazba kuzuia kazi hiyo ya uandikishaji.
Kutokana na hali kuwa tete, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dadi Faki Dadi, alifika katika eneo hilo na kuwataka wananchi kuacha jazba ili watoe nafasi kwa wananchi wenye sifa kujitokeza kuandikishwa.
Akizungumza katika eneo hilo, Dadi aliwataka wananchi hao kuacha kuchukua sheria mikononi na kuwasihi wasio na vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi kufuatilia katika maeneo husika.
Kabla ya kuanza kwa vurugu hizo, usiku wa kuamkia jana nyumba ya Sheha wa Kangagani, Faki Omar Yusuf, imechomwa moto na watu wasiojulikana, huku yeye na familia yake wakinusurika baada ya kuwahi kutoka nje.
Mkuu wa Wilaya ya Wete, Omar Khamis Othman, aliyekuwapo katika kituo cha Minungwini, alisema vurugu hizo na watu kugoma zinatokana na uhamasishaji uliofanywa na viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF), hasa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad.
Alisema Maalim Seif anajua hawezi kushinda katika uchaguzi mkuu ujao na ule wa serikali za mitaa, kwa kuwa hana wafuasi wa kutosha visiwani Pemba, ndiyo maana amefanya mipango ya kuchafua zoezi la uandikishaji wapiga kura.
Katika vurugu hizo, Ali Makame, Makame Mcha, Ame Mtwana Juma, Ali Jafar Haji na Suluhu Ame, walikamatwa na askari wa Kutuliza Ghasia (FFU) katika vituo vya uandikishaji vya Fukuchani na Nungwi shuleni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mselem Masoud Mtuliya, alisema tatizo lililojitokeza linaonekana kukosekana elimu ya kutosha ya uraia kwa wananchi.
Alisema kwamba watu wengi walikuwa hawalifahamu zoezi hilo, kwa vile wengi waliojitokeza ni waliotaka kubadilisha vitambulisho vya kura, wakati walitakiwa ambao wametimiza umri wa kuandikishwa wa miaka 18.
Mzee Saleh Mohamed Salim (58) wa Kityu alisema mwaka huu Wapemba wameamua kukataa kutii amri zinazowakandamiza na kuwadhalilisha na wanataka ulimwengu utambue kuwa na wao ni watu wenye kuthamini utu wao na haki zao.
Siti Ali Hamad (83) , alisema wamekusudia kukomesha wizi wa kura, hila na mizengwe inayofanywa na serikali inayoongozwa na CCM kila unapofika wakati wa uchaguzi, hivyo safari hii wameamua kudai haki ya kupiga kura kwa gharama yoyote ile.
Mwaka 2001 tulizika watoto wetu walioandamana kudai haki, sasa tupo tayari kujitolea roho zetu ili wajukuu wetu wapate haki, lakini si kukubali kuendelea kuburutwa, alisema Siti.
Said Mbaruk, alisema yeye ni mtetezi wa haki za vijana, anasikitishwa kuona askari walijazwa vituoni kwa lengo la kuwatisha raia ili wasiweze kushiriki kikamilifu katika zoezi la uandikishwaji.
Nilikuwa ninapigania haki na nitaendelea kuwapo hapa kusisitiza vijana wapiganie haki mpaka zijulikane mbichi na mbivu, tumetishwa sana, tumepigwa sana na hakuna kinachotutisha katika kudai haki zetu, hatuui, tunachotaka ni kupewa haki ya kupiga kura, alisema Said.
Ole Saleh Mohammed Salim (58), alipinga kauli iliyotolewa na Mkurugenzi wa Vitambulisho, Mohammed Juma Ame, kuwa wametoa vitambulisho 155,561 kisiwani Pemba.
Labda vitambulisho hivyo vimegawiwa Giningi (makao makuu ya wanga vibwengo). Sisi hatuna na hawataki kutupa, lakini tutaendelea kuvidai, kwa vile ni haki yetu. Tunachotaka ni kupiga kura, alisema Salim.
Naye Mkurugenzi wa Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salum Bimani, alisema sakata hilo la wananchi kukosa vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi ni mpango maalumu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na CCM, wenye nia ya kuwanyima haki ya kikatiba wananchi ili kuwezesha CCM kushinda kwa ujanja ujanja.
Hivi karibuni Jumuiya ya Ulaya (EU), Marekani, Canada na Japan zilitoa tahadhari kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar juu ya kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika zoezi la uandishaji wa watu katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Tahadhari hiyo ilipingwa vikali na Umoja
Askari wapigwa mawe, Maalim Seif atuhumiwa
na Mwandishi Wetu, Pemba
HALI ya amani kisiwani Pemba si shwari, baada ya jana kuibuka vurugu kubwa zilizosababisha nyumba ya sheha kuchomwa moto, polisi kurushiwa mawe na watu saba kukamatwa, kwa madai ya kuwazuia watu kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Vurugu hizo zimetokea baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kuanza zoezi hilo ililolisimamisha mwezi uliopita kutokana na kuwapo kwa vurugu zilizosababishwa na baadhi ya watu wanaodai mizengwe kutawala katika uandikishaji wa watu kwenye daftari hilo.
Mamia ya watu walijitokeza katika vituo vya uandikishaji wapiga kura, lakini hawakusogea kwa makarani kuandikishwa, huku wengine wakipambana na polisi kwa matusi na kurushiana mawe walipotakiwa waondoke vituoni kama hawakuwa tayari kujiandikisha.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Yahya Rashid Hemed, alilazimika kufika katika kituo cha Kiuyu, Minungwini na askari wa ziada wapatao 20 wenye silaha na mabomu ya machozi kuungana na askari wapatao 50 wa polisi, KMKM, Magereza na Usalama wa Taifa, ambao walionekana kushindwa kuidhibiti hali.
Polisi walipojaribu kutumia nguvu na kutisha watu kwa mtutu wa bunduki, ndipo wananchi walipoanza kurusha mawe, ambapo Kamanda Yahya, alilazimika kufanya kazi ya ziada kutuliza jazba za wananchi.
Vurugu hizo kwa kiasi kikubwa zimetokana na baadhi ya wananchi kudai kuwa wengi wao hawana vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi, ambavyo ndivyo vinavyotumika kama kigezo cha kuandikishwa.
Hali ya vurugu ilianza kujitokeza katika vituo vya uandikishaji vya Kambini na Minungwini katika Jimbo la Ole, ambapo wanachama wa CCM walipokuwa wakijaribu kwenda katika vituo vya kuandikishwa, makundi ya watu yaliyokuwa karibu na vituo yalionekana kupinga na kusababisha zoezi hilo kutokwenda vizuri.
Askari polisi na wa Kikosi cha Kujenga Uchumi (JKU) walionekana kuimarisha ulinzi katika kituo cha uandikishaji Kambini, lakini ulinzi huo haukusaidia kitu, baada ya wananchi wenye jazba kuzuia kazi hiyo ya uandikishaji.
Kutokana na hali kuwa tete, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Dadi Faki Dadi, alifika katika eneo hilo na kuwataka wananchi kuacha jazba ili watoe nafasi kwa wananchi wenye sifa kujitokeza kuandikishwa.
Akizungumza katika eneo hilo, Dadi aliwataka wananchi hao kuacha kuchukua sheria mikononi na kuwasihi wasio na vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi kufuatilia katika maeneo husika.
Kabla ya kuanza kwa vurugu hizo, usiku wa kuamkia jana nyumba ya Sheha wa Kangagani, Faki Omar Yusuf, imechomwa moto na watu wasiojulikana, huku yeye na familia yake wakinusurika baada ya kuwahi kutoka nje.
Mkuu wa Wilaya ya Wete, Omar Khamis Othman, aliyekuwapo katika kituo cha Minungwini, alisema vurugu hizo na watu kugoma zinatokana na uhamasishaji uliofanywa na viongozi wa Chama cha Wananchi (CUF), hasa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad.
Alisema Maalim Seif anajua hawezi kushinda katika uchaguzi mkuu ujao na ule wa serikali za mitaa, kwa kuwa hana wafuasi wa kutosha visiwani Pemba, ndiyo maana amefanya mipango ya kuchafua zoezi la uandikishaji wapiga kura.
Katika vurugu hizo, Ali Makame, Makame Mcha, Ame Mtwana Juma, Ali Jafar Haji na Suluhu Ame, walikamatwa na askari wa Kutuliza Ghasia (FFU) katika vituo vya uandikishaji vya Fukuchani na Nungwi shuleni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mselem Masoud Mtuliya, alisema tatizo lililojitokeza linaonekana kukosekana elimu ya kutosha ya uraia kwa wananchi.
Alisema kwamba watu wengi walikuwa hawalifahamu zoezi hilo, kwa vile wengi waliojitokeza ni waliotaka kubadilisha vitambulisho vya kura, wakati walitakiwa ambao wametimiza umri wa kuandikishwa wa miaka 18.
Mzee Saleh Mohamed Salim (58) wa Kityu alisema mwaka huu Wapemba wameamua kukataa kutii amri zinazowakandamiza na kuwadhalilisha na wanataka ulimwengu utambue kuwa na wao ni watu wenye kuthamini utu wao na haki zao.
Siti Ali Hamad (83) , alisema wamekusudia kukomesha wizi wa kura, hila na mizengwe inayofanywa na serikali inayoongozwa na CCM kila unapofika wakati wa uchaguzi, hivyo safari hii wameamua kudai haki ya kupiga kura kwa gharama yoyote ile.
Mwaka 2001 tulizika watoto wetu walioandamana kudai haki, sasa tupo tayari kujitolea roho zetu ili wajukuu wetu wapate haki, lakini si kukubali kuendelea kuburutwa, alisema Siti.
Said Mbaruk, alisema yeye ni mtetezi wa haki za vijana, anasikitishwa kuona askari walijazwa vituoni kwa lengo la kuwatisha raia ili wasiweze kushiriki kikamilifu katika zoezi la uandikishwaji.
Nilikuwa ninapigania haki na nitaendelea kuwapo hapa kusisitiza vijana wapiganie haki mpaka zijulikane mbichi na mbivu, tumetishwa sana, tumepigwa sana na hakuna kinachotutisha katika kudai haki zetu, hatuui, tunachotaka ni kupewa haki ya kupiga kura, alisema Said.
Ole Saleh Mohammed Salim (58), alipinga kauli iliyotolewa na Mkurugenzi wa Vitambulisho, Mohammed Juma Ame, kuwa wametoa vitambulisho 155,561 kisiwani Pemba.
Labda vitambulisho hivyo vimegawiwa Giningi (makao makuu ya wanga vibwengo). Sisi hatuna na hawataki kutupa, lakini tutaendelea kuvidai, kwa vile ni haki yetu. Tunachotaka ni kupiga kura, alisema Salim.
Naye Mkurugenzi wa Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salum Bimani, alisema sakata hilo la wananchi kukosa vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi ni mpango maalumu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na CCM, wenye nia ya kuwanyima haki ya kikatiba wananchi ili kuwezesha CCM kushinda kwa ujanja ujanja.
Hivi karibuni Jumuiya ya Ulaya (EU), Marekani, Canada na Japan zilitoa tahadhari kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar juu ya kasoro mbalimbali zilizojitokeza katika zoezi la uandishaji wa watu katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Tahadhari hiyo ilipingwa vikali na Umoja