Chademakwanza
JF-Expert Member
- Jun 11, 2014
- 6,346
- 1,871
Nimekuwa nikimsikia tu Padre Baptist Mapunda.Leo nimeenda kanisani kwangu misa ya kwanza nikamkuta Padre mpya.Akajitambulisha anaitwa Baptist Mapunda Tunda la Kanisa.
Mahubiri yake:
*Amesema amepata maono kwamba Serikali ya CCM itaua watu wengi sana mwaka huu ili ibaki madarakani
*Akasema utawala huu ni wa shetani kwani watawala wamewageuka wananchi na kutenda kila aina ya uovu kwa raia wake
*Akasema anashangaa watu wanadanganywa na kanga na Tshirt za CCM ili kuichagua.Akadai mwenye shida amfuate atamnunulia Tshirt 10 bure kuliko kuvaa Tshirt ya CCM
*Akadai haogopi kufa kwa kusema ukweli.Akasema kama CCM wanamchukia akitoka nje wamkate shingo yake.
*Amewashangaa mafisadi waliopewa mabiliini ya Escrow na akadai yeye siyo kiongozi wa dini wa kuhongwa
*Akasema mtu ambaye mpaka leo anachagua CCM ni kipofu na amelaaniwa.Akasema haogopi kuchukiwa na CCM kwani yeye ni Nabii
*Akasema kuonyesha CCM ni watu waovu wameamua kwa makusudi kuwaapisha watu walioshindwa katika chaguzi.Huo ni ushetani wa kiwango cha mwisho kabisa.
*Amewashambulia viongozi wa dini wanafiki walamba viatu vya mafisadi ambao kila mwaka mpya wanaitisha kongamano wanalodai ni la kuombea amani.Amesema hawezi kushiriki upuuzi wa aina hiyo hata siku moja.Kwa sababu viongozi wa aina hiyo hawataki kuwaambia ukweli watawala kwamba matendo yao ndiyo yanavuruga amani.
--**Mwenye Masikio na asikie--**
Mahubiri yake:
*Amesema amepata maono kwamba Serikali ya CCM itaua watu wengi sana mwaka huu ili ibaki madarakani
*Akasema utawala huu ni wa shetani kwani watawala wamewageuka wananchi na kutenda kila aina ya uovu kwa raia wake
*Akasema anashangaa watu wanadanganywa na kanga na Tshirt za CCM ili kuichagua.Akadai mwenye shida amfuate atamnunulia Tshirt 10 bure kuliko kuvaa Tshirt ya CCM
*Akadai haogopi kufa kwa kusema ukweli.Akasema kama CCM wanamchukia akitoka nje wamkate shingo yake.
*Amewashangaa mafisadi waliopewa mabiliini ya Escrow na akadai yeye siyo kiongozi wa dini wa kuhongwa
*Akasema mtu ambaye mpaka leo anachagua CCM ni kipofu na amelaaniwa.Akasema haogopi kuchukiwa na CCM kwani yeye ni Nabii
*Akasema kuonyesha CCM ni watu waovu wameamua kwa makusudi kuwaapisha watu walioshindwa katika chaguzi.Huo ni ushetani wa kiwango cha mwisho kabisa.
*Amewashambulia viongozi wa dini wanafiki walamba viatu vya mafisadi ambao kila mwaka mpya wanaitisha kongamano wanalodai ni la kuombea amani.Amesema hawezi kushiriki upuuzi wa aina hiyo hata siku moja.Kwa sababu viongozi wa aina hiyo hawataki kuwaambia ukweli watawala kwamba matendo yao ndiyo yanavuruga amani.
--**Mwenye Masikio na asikie--**