Ni Kweli, matumizi ya pilipili yanamsulubu bacteria asizidishe uharibifu tumboni, hiyo Inaitwa, dawa ya moto ni moto.Anhaaa, sasa napata connection. Kuna dogo mmoja kule Buzuruga, Mwanza aliniambia kuwa yeye alikua anasumbuliwa na vidonda vya tumbo akawa akila pilipili anaumia sana lakini baadae anakuwa poa. Akawa anazila kwa fujo tumbo likiuma kisha linatulia.
Baadae akanipa habari ile hali ya tumbo kujaa gesi, kuunguruma, kuharisha imeisha. Anakula maharage, dagaa na kila kitu. Kiufupi alipona.
Mimi niliambiwa dawa hiyo na Mhindi nikapuuza, baadae nikatumia kidogo kidogo, ilisaidia sana.
Bt hatua muhimu ya kwanza ni kuzingatia kula Kwa wakati na kuepuka vyakula vyenye gas kama maharage nk nk
Pia hasira na kutunza visasi, kiufupi stress ni chanzo kikuu Cha madonda.
Pilipili, Kwa kuanzia, usile pilipili kichaa, Utaharibu,
Anza na pilipili zile zenye harufu nzuri zinazopikiwa kwenye mboga.
Unajua kama huna pesa, halafu uwe na madonda yanayokuzuia kutumia maharage ni taabu kubwa.
Mungu atusaidie.