Okoa Tanzania Bara: Saini Petition ya kuzuia ubinafsishwaji wa bandari zote za Tanzania Bara

Boss la DP World

JF-Expert Member
Dec 12, 2021
1,997
7,552
Hili jambo halijakaa sawa katika angle zote, na limelenga sehemu nyeti ambayo inaweza kudhoofisha nchi yetu hasa Tanzania bara na kufungua ukurasa mpya wa ukoloni mambo leo.
Saini petition kwenye website ya change kupaza sauti dhidi ya uhalifu huu uliopangwa kutokea mbele ya macho yetu.

 
Hili jambo halijakaa sawa katika angle zote, na limelenga sehemu nyeti ambayo inaweza kudhoofisha nchi yetu hasa Tanzania bara na kufungua ukurasa mpya wa ukoloni mambo leo.
Saini petition kwenye website ya change kupaza sauti dhidi ya uhalifu huu uliopangwa kutokea mbele ya macho yetu.

Mlishindwa kupinga bunge mbovu ndo mtaweza kupinga miswada yake.
 
Hili jambo halijakaa sawa katika angle zote, na limelenga sehemu nyeti ambayo inaweza kudhoofisha nchi yetu hasa Tanzania bara na kufungua ukurasa mpya wa ukoloni mambo leo.
Saini petition kwenye website ya change kupaza sauti dhidi ya uhalifu huu uliopangwa kutokea mbele ya macho yetu.

Wafuasi wa Marehemu poleni sana. Wakati lile shetani lenu la Chato linabaka uchaguzi na kutuwekea wabunge wa kumtawalisha milele si mlikuwa mnashangilia nyie!
Eti alikuwa Mzalendo. Sasa misukule yake njaa imewapanda vichwani ndo mnataka tushirikiane
 
Afadhali yule kuliko huyu anayetuuza huku anatuchekea.

Such an evil woman.
Hakuna afadhali wala nafuu, maana ndiye aliyetufikisha hapa.

Tena mbali ya uuaji na wizi, pia alifanya ufisadi wa kufuru i.e. Mwendazake.
 
Hakuna afadhali wala nafuu, maana ndiye aliyetufikisha hapa.

Tena mbali ya uuaji na wizi, pia alifanya ufisadi wa kufuru i.e. Mwendazake.
Huyu wa sasa anapora kwa kalamu tena anakomba vyote bila hata huruma.

Ni uovu uliopitiliza.
 
Nikatae maendeleo? Huo ni ujinga first class. Mkataba ni makubaliano.

Maza akimaliza hapo aende airports. Boma Liwanzaaa
 
Usalama, usiri na anonymity wa washiriki unahakikishwaje?

Sio kwamba tunasain ili tujuulikane?
 
Huyu wa sasa anapora kwa kalamu tena anakomba vyote bila hata huruma.

Ni uovu uliopitiliza.
Nakubali nawe mkuu Stroke, kwamba huyu wa sasa naye ni mwizi.

Nachopinga ni hilo neno afadhali.

Sisi kama Taifa hatuna unafuu wowote iwe kuibiwa kwa Siri au kalamu au tabasamu; iwe na Magu au Samia. Wizi ni wizi, ufisadi ni ufisadi - tuukemee na kuuchukia wazi wazi bila kuupaka rangi. Huo ndio msingi wa hoja yangu.
 
Kumbe mkataba wa milele wa TPA na DPW ulisainiwa na Magufuli
Ok sasa nimejua ukweli ndugu
Usipindishe maneno.

Pia ujue akiiba Samia aliyewekwa na Magufuli na kupata ridhaa ya wabunge wa Magufuli, au akiiba Magufuli (kama alivyoiba) au CCM (kwao ni utamaduni) matokea ni yale yale kwetu kama Taifa = HASARA!
 
Back
Top Bottom