Habari kutoka Morogoro zinaeleza kuwa "Watu mbalimbali wamefika ofisi za Chadema wilaya ya Morogoro mjini kutoa pole kutokana na msiba wa Mh. Regia Mtema, baadhi ya wakazi wa Morogoro walikuwa wakitoa michango ya rambirambi na wengine wakiulizia utaratibu wa usafiri wa kwenda Kilombero kuhudhuria mazishi.
Habari zimeendelea kudai kuwa Mh. Abood Aziz mbunge wa Morogoro mjini CCM amewaambia viongozi wa CHADEMA kuwa yuko tayari kutoa basi lake bure kusafirisha wanachama wa CHADEMA wataopenda kwenda kumzika marehemu Regia Mtema.
Habari zimeendelea kudai kuwa uamuzi wa mbunge huyo wa kujitolea basi uliibua mjadala mkubwa kwa wanachama wa CHADEMA kwani baadhi walionekana katakata kukataa msaaada huo kwa madai kuwa huenda ni mtego kwao wa kisiasa ili kuzima mashambulizi ya shutuma ambazo chama hicho kimekuwa kinatoa kwake kuwa amekuwa anatumia kutoa basi la kuzika wafu kila unapotokea msiba kama mtaji wa kisiasa badala ya kuibana serikali kuboresha huduma za afya ili kupunguza vifo".
Habari zimeendelea kudai kuwa Mh. Abood Aziz mbunge wa Morogoro mjini CCM amewaambia viongozi wa CHADEMA kuwa yuko tayari kutoa basi lake bure kusafirisha wanachama wa CHADEMA wataopenda kwenda kumzika marehemu Regia Mtema.
Habari zimeendelea kudai kuwa uamuzi wa mbunge huyo wa kujitolea basi uliibua mjadala mkubwa kwa wanachama wa CHADEMA kwani baadhi walionekana katakata kukataa msaaada huo kwa madai kuwa huenda ni mtego kwao wa kisiasa ili kuzima mashambulizi ya shutuma ambazo chama hicho kimekuwa kinatoa kwake kuwa amekuwa anatumia kutoa basi la kuzika wafu kila unapotokea msiba kama mtaji wa kisiasa badala ya kuibana serikali kuboresha huduma za afya ili kupunguza vifo".