Obama amemuumbua Rais Kikwete

Gudboy

JF-Expert Member
Aug 14, 2009
867
77
Julius Samwel Magodi

RAIS Barack Obama wa Marekani, wiki hii alifanya mazungumzo na baadhi ya viongozi wa nchi za Afrika, waliokuwa wakihudhuria mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN).

Katika mkutano huo pamoja na mambo mengine, aliwapasulia jibu linalowasumbua viongozi hao kwamba hakuna uwekezaji mzuri katika nchi inayokumbatia ufisadi.

Aliwataka viongozi hao akiwamo Rais Jakaya Kikwete, ambaye alihudhuria hafla hiyo kuondoa ufisadi katika nchi zao ndipo watakapoona manufaa ya uwekezaji.

Alisema mazingira yaliyopo sasa ni kuwa, uwekezaji umeshindwa kuzinufaisha nchi za kiafrika, kutokana na rushwa kutumika kuingiza wawekezaji feki.

Kwa hakika maneno haya ya Obama nilipoyasikia yalinikuna sana, nadhani Rais Kikwete alishtuka sana aliposikia kauli hiyo. Nasema atakuwa alishtuka kutokana na ukweli kwamba onyo hilo lilikuwa likiilenga serikali ya Tanzania.

Ingawa hakuwa akimanisha Tanzania pekee, lakini Obama kama vile mtabiri, kila alichokuwa akikizungumza kilikuwa kikiihusu serikali ya Kikwete.

Hakuna mtu asiyejua kwamba Tanzania sasa, imegeuzwa kuwa shamba la bibi na wawekezaji kutoka nje, ambao wamekuwa wakiingia nchini kuchuma na kuondoka na utajiri mkubwa.

Kuna wakati fulani mwekezaji mmoja kutoka nje aliwahi kusema kwamba,Tanzania ni nchi pekee duniani ambayo unaweza kuingia na kuwekeza ukiwa huna kitu, halafu ukatoka ukiwa miongoni mwa matajiri wakubwa duniani.

Obama alitukumbusha watanzania matatizo makubwa ya mikataba feki ya uwekezaji, ambayo sasa inatutesa na kutufanya tubaki watumwa katika nchi yetu.

Hotuba ya Obama itakuwa ilimkumbusha Rais Kikwete, uwekezaji mbaya ambao mpaka sasa umetutesa, kutokana na maafisa wa serikali kushirikiana na wawekezaji kuiibia nchi.

Mikataba hii ni ile ya Kampuni ya Rites na Shirika la Reli Tanzania (TRC), mikataba ya migodi ya madini, jinsi ambavyo wawekezaji wanachukua madini na kutuachia mashimo. Mgodi wa Mkaa ya mawe ya Kiwira, Richmond, TICTS na mingine mingi.

Hata hivyo Rais Kikwete ambaye kabla ya kuondoka kwenda Marekani, alikaririwa akisisitiza hakuna uchumi wa nchi yoyote duniani unaoweza kukua kwa uwekezaji wa serikali peke yake, bila wawekezaji binafsi.

Aliwataka maofisa wa serikali yake, kuchukua maamuzi ya haraka kutimiza mahitaji ya wawekezaji, mara zinapojitokeza nafasi za wawekezaji kutaka kuja nchini na sio kuwazuia.

Kwa hakika, kama Rais Kikwete anasema uwekezaji ndio njia muhimu ya kuleta maendeleo kwa wananchi, bila ya kutoa onyo kwa watendaji wake wa serikali, kuhusu kuingia mikataba feki ambayo imeipotezea nchi mabilioni ya shilingi, bado tuna matatizo makubwa.

Ni kweli kuwa maendeleo yanaweza kuchangiwa na wawekezaji wa nje. kwa vile wataingiza teknolojia mpya, kupanua ajira na kuongeza mapato ya nchi. Lakini kwa uwekezaji tuliona hapa nchini, wawekezaji kugeuka kuwa milija ya kunyonyea raslimali zetu, bado hawawezi kuwa ni suluhu ya matatizo yetu.

Kitu kibaya ambacho kimejengeka kwa viongozi wetu, ni kuugeuza uwekezaji kuwa miradi yao ya kujipatia utajiri na pengine kutafuatia fedha za CCM, kwa ajili ya uchaguzi mkuu.

Hii ni hatari sana kwa ustawi wa nchi, viongozi wetu wanachekelea kuendelea kuwepo kwa udhaifu wa sheria ya mikataba ya uwekezaji wakijua kwamba, wataendelea kujinufaisha wao au kundi lao.

Leo hii kila mwekezaji ambaye tumeingia naye mikataba feki, nyuma yake yupo kigogo wa serikali au aliyekuwepo katika uongozi wa serikali zilizopita.

Kwa mahesabu ya haraka haraka, mpaka sasa fedha ambazo zinadaiwa kukombwa serikalini kwa njia ya ufisadi, ama kupitia mikataba feki ya uwekezaji na wizi mwingine, ni zaidi ya shilingi trilioni moja, ambazo ni sawa na bajeti za wizara sita kubwa.

Kama viongozi wetu wangekuwa makini ambao hawana ubinafsi, wanaopenda nchi yao, leo fedha hizo zingekuwa ziko salama, zingeweza kujengea barabara na hospitali karibu nchi nzima na hivyo wanachi wakapata maisha bora, kama Rais Kikwete alivyoahidi wakati akiingia madarakani.

Hii ndio Tanzania yetu ambayo inatajwa kuwa moja ya nchi maskini kabisa duniani, ambayo inakosa uongozi madhubuti wa kulinda maliasili zake.

Mwandishi mashuhuri duniani Robin Sharma katika kitabu chake cha 'lead without title' anasema, "kila mtu anaweza kuonyesha tabia za kuwa kiongozi, lakini hiyo haimaanishi kuwa kila mtu anaweza kuwa kiongozi."

Tatizo letu hapa ni kwamba tunao viongozi wengi hususani maafisa waandamaizi na wanasiasa lakini hawana sifa za uongozi kutokana na kujiingiza katika kuifilisi nchi badala ya kulinda rasilimali zetu.

Tatizo tulinalo si wawekezaji, ni sisi wenyewe tunaowaruhusu hao wawekezaji kuchukua faida kubwa katika huo uwekezaji, kwa mikataba feki isiyo na manufaa kwa nchi. Kinachofanyika hapa nchini, ni uporaji wa mali ambao umebarikiwa na viongozi wetu.

Kinachotakiwa sasa tuwe na mapinduzi ya fikra, tutumie uchaguzi ujao kuchagua viongozi ambao wataiongoza nchi, kutufikisha katika nchi ya asali na maziwa badala ya kutupeleka na kutuacha jangwani.

Mwandishi wa safu hii anapatikana kupitia baruapepe; juliusmagodi@yahoo.com
Simu; 0754 304336

source: mwananchi
 
Tatizo tulinalo si wawekezaji, ni sisi wenyewe tunaowaruhusu hao wawekezaji kuchukua faida kubwa katika huo uwekezaji, kwa mikataba feki isiyo na manufaa kwa nchi. Kinachofanyika hapa nchini, ni uporaji wa mali ambao umebarikiwa na viongozi wetu.


Kinachotakiwa sasa tuwe na mapinduzi ya fikra, tutumie uchaguzi ujao kuchagua viongozi ambao wataiongoza nchi, kutufikisha katika nchi ya asali na maziwa badala ya kutupeleka na kutuacha jangwani.
Gody, hapo umenena tatizo si wawekezaji ni sisi wenyewe tuliopewa nafasi ya kutengeneza mikataba halafu tunaachia "grey areas" makusidi kabisa kwa manufaa ya sisi binafsi.

Halafu kingine ni kwamba pale tunapoachia wanasiasa kuwa decision makers wa technical matters badala ya kuwapa subject matter experts, ndipo tunapotumbukia humo. Hata wabunge, kwa mfano ukiacha wabunge waliochaguliwa na wananchi hebu angalia CV zao, wengi form four, form six, na wengine wana vyeti vya diploma kwenye vyuo ambavyo hata sisi hatuvijui. Tungedhania kuwa basi hawa wa kuteuliwa wangekuwa chachu ktk bunge kwa kuteuliwa watu ambao wana uwezo wa kifikra na sio wa kuumba maneno, nadhani tungepiga hatua.

Pale pia mtu anaponeemeka kwa kuiba hapa bongo anasifiwa kuwa ana akili na ametumia nafasi vizuri. Ingefaa mtu kama huyu afilisiwe kila kitu mpaka kibanda alichojenga kijijini na vyeti vyake kunyang'anywa na serikali na kurudishwa kijijini na kunyimwa uhuru wa kutembea. Ile mali yake itumike kuleta maendeleo kwa wananchi wote na itangazwe. Hawa watu na jamii zao ziogopwe kama ukoma. Nadhani mtu atafikiria sana kabla ya kuboronga kazi yake.

Na si hivyo tu, wale wote walioliingizia taifa hasara hali wakijua wanafanya nini, wachukuliwe hatua ambayo itasaidia kuleta mfano kwa wengine wasirudie wajue cheo ni dhamana na siyo kwa ajili ya kujinufaisha binafsi. Mtu anaruhusu dawa feki au chakula feki kuingia kwenye soko huyu anastahili anyongwe mpaka kufa, mtu anayetumia vibaya fedha za kusaidia wagonjwa wenye magonjwa sugu (fedha za kupitia TACAIDS n.k.) wanyongwe mpaka kufa, polisi wanaosingizia watu kessi na kushuhudia uwongo wawekwe magereza maisha yao yote, polisi wanaokodisha silaha kwa majambazi na kushirikiana nao wanyongwe mpaka kufa na jamii ipate kujua nadhani tutajenge nidhamu katika taifa letu na tutapiga hatua.

Hatuwezi kuwa na demokrasia ya Marekani au Uingereza kwa umri tulionao wa Uhuru wetu wa miaka 48, ni lazima demokrasia iwepo lakini mtu mdhulumaji huyu si mdemokrasia na hahitaji kupewa demokrasi. Ifike wakati tujue sisi ni nani na tunatakiwa kufanya nini na wapi na lini na kwa manufaa ya nani.
 
Tatizo la uwekezaji Tanzania ni upumbavu wa watawala wetu+roho mbaya ya nchi za magharibi kwa afrika.

Kwahiyo Kikwete na Obama ni sawa na Nyani na Ngedele, wote wanaongoza hujuma dhidi ya mali ya mwafrika
 
Kichwa cha habari hii kinapotoka kabisa,habari yenyewe.Ni taarifa muhimu na nzuri,yaelekea Mwandishi amehamasika mno kwa kutaka kutuuzia Gazeti!! Aibu kwa Mwandishi...........................
 
Julius Samwel Magodi

RAIS Barack Obama wa Marekani, wiki hii alifanya mazungumzo na baadhi ya viongozi wa nchi za Afrika, waliokuwa wakihudhuria mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN).

Katika mkutano huo pamoja na mambo mengine, aliwapasulia jibu linalowasumbua viongozi hao kwamba hakuna uwekezaji mzuri katika nchi inayokumbatia ufisadi.

Aliwataka viongozi hao akiwamo Rais Jakaya Kikwete, ambaye alihudhuria hafla hiyo kuondoa ufisadi katika nchi zao ndipo watakapoona manufaa ya uwekezaji.

Alisema mazingira yaliyopo sasa ni kuwa, uwekezaji umeshindwa kuzinufaisha nchi za kiafrika, kutokana na rushwa kutumika kuingiza wawekezaji feki.

Kwa hakika maneno haya ya Obama nilipoyasikia yalinikuna sana, nadhani Rais Kikwete alishtuka sana aliposikia kauli hiyo. Nasema atakuwa alishtuka kutokana na ukweli kwamba onyo hilo lilikuwa likiilenga serikali ya Tanzania.

Ingawa hakuwa akimanisha Tanzania pekee, lakini Obama kama vile mtabiri, kila alichokuwa akikizungumza kilikuwa kikiihusu serikali ya Kikwete.

Hakuna mtu asiyejua kwamba Tanzania sasa, imegeuzwa kuwa shamba la bibi na wawekezaji kutoka nje, ambao wamekuwa wakiingia nchini kuchuma na kuondoka na utajiri mkubwa.

Kuna wakati fulani mwekezaji mmoja kutoka nje aliwahi kusema kwamba,Tanzania ni nchi pekee duniani ambayo unaweza kuingia na kuwekeza ukiwa huna kitu, halafu ukatoka ukiwa miongoni mwa matajiri wakubwa duniani.

Obama alitukumbusha watanzania matatizo makubwa ya mikataba feki ya uwekezaji, ambayo sasa inatutesa na kutufanya tubaki watumwa katika nchi yetu.

Hotuba ya Obama itakuwa ilimkumbusha Rais Kikwete, uwekezaji mbaya ambao mpaka sasa umetutesa, kutokana na maafisa wa serikali kushirikiana na wawekezaji kuiibia nchi.

Mikataba hii ni ile ya Kampuni ya Rites na Shirika la Reli Tanzania (TRC), mikataba ya migodi ya madini, jinsi ambavyo wawekezaji wanachukua madini na kutuachia mashimo. Mgodi wa Mkaa ya mawe ya Kiwira, Richmond, TICTS na mingine mingi.

Hata hivyo Rais Kikwete ambaye kabla ya kuondoka kwenda Marekani, alikaririwa akisisitiza hakuna uchumi wa nchi yoyote duniani unaoweza kukua kwa uwekezaji wa serikali peke yake, bila wawekezaji binafsi.

Aliwataka maofisa wa serikali yake, kuchukua maamuzi ya haraka kutimiza mahitaji ya wawekezaji, mara zinapojitokeza nafasi za wawekezaji kutaka kuja nchini na sio kuwazuia.

Kwa hakika, kama Rais Kikwete anasema uwekezaji ndio njia muhimu ya kuleta maendeleo kwa wananchi, bila ya kutoa onyo kwa watendaji wake wa serikali, kuhusu kuingia mikataba feki ambayo imeipotezea nchi mabilioni ya shilingi, bado tuna matatizo makubwa.

Ni kweli kuwa maendeleo yanaweza kuchangiwa na wawekezaji wa nje. kwa vile wataingiza teknolojia mpya, kupanua ajira na kuongeza mapato ya nchi. Lakini kwa uwekezaji tuliona hapa nchini, wawekezaji kugeuka kuwa milija ya kunyonyea raslimali zetu, bado hawawezi kuwa ni suluhu ya matatizo yetu.

Kitu kibaya ambacho kimejengeka kwa viongozi wetu, ni kuugeuza uwekezaji kuwa miradi yao ya kujipatia utajiri na pengine kutafuatia fedha za CCM, kwa ajili ya uchaguzi mkuu.

Hii ni hatari sana kwa ustawi wa nchi, viongozi wetu wanachekelea kuendelea kuwepo kwa udhaifu wa sheria ya mikataba ya uwekezaji wakijua kwamba, wataendelea kujinufaisha wao au kundi lao.

Leo hii kila mwekezaji ambaye tumeingia naye mikataba feki, nyuma yake yupo kigogo wa serikali au aliyekuwepo katika uongozi wa serikali zilizopita.

Kwa mahesabu ya haraka haraka, mpaka sasa fedha ambazo zinadaiwa kukombwa serikalini kwa njia ya ufisadi, ama kupitia mikataba feki ya uwekezaji na wizi mwingine, ni zaidi ya shilingi trilioni moja, ambazo ni sawa na bajeti za wizara sita kubwa.

Kama viongozi wetu wangekuwa makini ambao hawana ubinafsi, wanaopenda nchi yao, leo fedha hizo zingekuwa ziko salama, zingeweza kujengea barabara na hospitali karibu nchi nzima na hivyo wanachi wakapata maisha bora, kama Rais Kikwete alivyoahidi wakati akiingia madarakani.

Hii ndio Tanzania yetu ambayo inatajwa kuwa moja ya nchi maskini kabisa duniani, ambayo inakosa uongozi madhubuti wa kulinda maliasili zake.

Mwandishi mashuhuri duniani Robin Sharma katika kitabu chake cha 'lead without title' anasema, "kila mtu anaweza kuonyesha tabia za kuwa kiongozi, lakini hiyo haimaanishi kuwa kila mtu anaweza kuwa kiongozi."

Tatizo letu hapa ni kwamba tunao viongozi wengi hususani maafisa waandamaizi na wanasiasa lakini hawana sifa za uongozi kutokana na kujiingiza katika kuifilisi nchi badala ya kulinda rasilimali zetu.

Tatizo tulinalo si wawekezaji, ni sisi wenyewe tunaowaruhusu hao wawekezaji kuchukua faida kubwa katika huo uwekezaji, kwa mikataba feki isiyo na manufaa kwa nchi. Kinachofanyika hapa nchini, ni uporaji wa mali ambao umebarikiwa na viongozi wetu.

Kinachotakiwa sasa tuwe na mapinduzi ya fikra, tutumie uchaguzi ujao kuchagua viongozi ambao wataiongoza nchi, kutufikisha katika nchi ya asali na maziwa badala ya kutupeleka na kutuacha jangwani.

Mwandishi wa safu hii anapatikana kupitia baruapepe; juliusmagodi@yahoo.com
Simu; 0754 304336

source: mwananchi


Prez Obama alikuwa anampigia mbuzi gitaa!!!
 
Kikwete ameshambuliwa vibaya sana kuhusu serikali yake na hali ya Zanzibar ila katika kutaka kujinasua amesema eti serikali yake haihusiki ,kinachohusika ni Chama Chake.
Eti mambo ya Zanzibar yanahusu Vyama sio serikali ,hivi wale wanaotolewa roho kule serikali haihusiki ? Lakini ameonywa na kaahidi kabla ya 2010 atashughulikia nafikiri amewaondoa UN njiani ,jamaa si mkweli.
 
mnae mpigia kelele mwandishi kosa lake nini?

mpaka mtake kumpiga makonzi wengine, sio kila kitu lazima waandike chadema ndio ki-make sense kwa wote humu ndani, ye anaelezea matatizo ambayo matter of fact ndio kila siku mnalia nayo.

Na kwa jinsi nilivyoelewa mimi mpaka the most powerful man in the world kesha yatambua sasa ni nini. Au hajaweka loliondo directly kwenye uwekezaji.

Mijitu mingine kwa lalama tu kiboko.
 
mnae mpigia kelele mwandishi kosa lake nini?

mpaka mtake kumpiga makonzi wengine, sio kila kitu lazima waandike chadema ndio ki-make sense kwa wote humu ndani, ye anaelezea matatizo ambayo matter of fact ndio kila siku mnalia nayo.

Na kwa jinsi nilivyoelewa mimi mpaka the most powerful man in the world kesha yatambua sasa ni nini. Au hajaweka loliondo directly kwenye uwekezaji.

Mijitu mingine kwa lalama tu kiboko.

Mkuu,

Usisumbue kichwa chako bure. Kuna watu kwa sasa wamewekwa tayari tayari kushambulia hoja yoyote inayoonekana kupingana na serikali ya mafisadi inayoletwa hapa JF. Yaani ukisoma terms of reference ya kazi yao ndio hiyo. Eti wanadiriki kumshambulia mwandishi!!! halafu hawasemi ni kipi mwandishi kakosea. Nafikiri they are at the wrong place. Hapa kuna vichwa bwana watu wana uwezo wa kupambanua mambo sio kuleta cheap politics hapa.

Tiba
 
mimi ndio maana huwa siamini magazeti ya home, bora niwe nashinda hapa JF naweza nikapata chochote kuliko magazetini
 
Mkuu,

Usisumbue kichwa chako bure. Kuna watu kwa sasa wamewekwa tayari tayari kushambulia hoja yoyote inayoonekana kupingana na serikali ya mafisadi inayoletwa hapa JF. Yaani ukisoma terms of reference ya kazi yao ndio hiyo. Eti wanadiriki kumshambulia mwandishi!!! halafu hawasemi ni kipi mwandishi kakosea. Nafikiri they are at the wrong place. Hapa kuna vichwa bwana watu wana uwezo wa kupambanua mambo sio kuleta cheap politics hapa.

Tiba

ina make sense sasa asante.
 
Mkuu,

Usisumbue kichwa chako bure. Kuna watu kwa sasa wamewekwa tayari tayari kushambulia hoja yoyote inayoonekana kupingana na serikali ya mafisadi inayoletwa hapa JF. Yaani ukisoma terms of reference ya kazi yao ndio hiyo. Eti wanadiriki kumshambulia mwandishi!!! halafu hawasemi ni kipi mwandishi kakosea. Nafikiri they are at the wrong place. Hapa kuna vichwa bwana watu wana uwezo wa kupambanua mambo sio kuleta cheap politics hapa.

Tiba


safi!!!
 
Mimi naona kichwa cha habari hizi kingekuwa OBAMA AMUUNGA MKONO kIKWETE.

Jinsi JMK alivyo mstari wa mbele na anavyoshughulikia mafisadi na ufisadi systematically, anastahili kila sifa na kuungwa mkono. Obama nna uhakika analijuwa hilo na ndio maana tukaona JMK akiweka rikodi ya kuwa Mkulu wa Kwanza kutoka Africa kukaribishwa na Rais wa kwanza wa USA mwenye asili ya Ki Afrika.

Mwandishi wa hii makala hata aiparaganye vipi kutaka kumponda JMK, haikai.
 
Last edited by a moderator:
tuwe fair hii habari haijatulia ...mimi nilifikiri kamuumbua jk ...kumbe alikuwa anahutubia viongozi waafrika...unajuwa kiongozi wa afrika aliyepewa heshima ya kutoa opening remarks kwenye hiyo luncheon ni kikwete????

ni vema kumpiga jk makonzi lakini yawe ya kweli!!!
 
Waandishi wetu bwana, sometimes unaweza kuwakata makonzi!

umeliona hilo mkuu, pamoja sana

Mkuu kama mko kwenye mawazo yangu; halafu mwisho kajipamba anapatikana vipi....

Kichwa cha habari hii kinapotoka kabisa,habari yenyewe.Ni taarifa muhimu na nzuri,yaelekea Mwandishi amehamasika mno kwa kutaka kutuuzia Gazeti!! Aibu kwa Mwandishi...........................


Guys you need to rethink your ability to critically review things without posing barriers. Content matters a lot!

YeboYebo umekua sasa acheni utoto wa kuleta leta vimajungumajungu visivyojenga! Critical thinking haiko hivi, kama iko hivi basi tumekwisha.

mliyoandika hapo juu is rubbish na yanapatikana tu kwa wale wenye tabia za kitaarabutaarabu! japo taarabu asilia haina umbea na unafiki!

cheers
 
Back
Top Bottom