Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
MBUNGE NOAH SAPUTU - WAZIRI WA ARDHI WANANCHI WANAKUTEGEMEA KUTOA HAKI
"Hii siyo sawa wageni kumiliki Ardhi, haki iliyochelewa ni sawa na haki iliyonyimwa" - Mhe. Noah Lemburis Saputi Mollel, Mbunge wa Arumeru Magharibi.
"Waziri toa tamko kwa makampuni ambayo yamepimia wananchi Ardhi, imepelekea wananchi kupata matatizo makampuni yamekimbia" - Mhe. Noah Lemburis Saputi Mollel, Mbunge wa Arumeru Magharibi.
"Waziri wananchi wanakutegemea kutoa haki, Sheria ya Ardhi na mabaraza yaboreshwe kwani yanamkandamiza mwananchi " - Mhe. Noah Lemburis Saputi Mollel, Mbunge wa Arumeru Magharibi.
"Kwanini tunaendelea kung'ang'ania mabaraza chini ya Wizara? Bora yawekwe chini ya mahakama ili kutoa haki kwa Watanzania" - Mhe. Noah Lemburis Saputi Mollel, Mbunge wa Arumeru Magharibi.