Mwandwanga
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 3,059
- 1,568
Habari wana Ukumbi,
Leo nimekuja hapa barazani kufikisha kero yangu kwa benki ya NMB tawi la Mbalizi road MBEYA.
Mwaka 2013 mwezi wa Nne (04) nilienda kwenye ofisi zao, kwa minajili ya kuomba mkopo. Nilipofika pale nilikutana na Loan officer alijitambulisha kwa jina la Kirungeme.
Katika hatua za awali niliweza pata ushirikiano wa kutosha kwa huyu mfanyakazi. Nilipokamilisha hatua zote ikiwemo ile ya kuja kunitembelea na kuangalia shughuli zangu. Bank iliamua kunipa mkopo wa Tsh. 500,000/- ingawa niliomba Tsh. 1,000,000/-
Kadhia ilianza hapa;
Niliombwa pesa ya mafuta ya gari kwa kuja kunitembelea niliwapa 15,000/- (ilinibidi kutoa maana nilikuwa na shida hasa na ule mkopo)
Akanielekeza kwa mwanasheria atakaye gonga Muhuri na kunitajia kabisa kiwango cha kumlipa (niliambiwa nikamlipe 50,000/-) hili sikulifanya maana, nilienda States attorney nikapigiwa muhuri kwa 10,000/- na kuzirudisha form Bank. Nilipo zikabidhi form za mkopo kwa loan officer huyu alianza kugomba kwanini sijaenda kwa mwanasheria aliyenitajia!
Nilifanikiwa kuchukua mkopo, na kufanya marejesho kila mwezi kama mkataba wetu ulivyokuwa umeelekeza. Baada ya kukamilisha Marejesho, na kufanikiwa kulipa mkopo wote nilienda tena Bank n kukutana na Kirungeme akaniambia yeye kapanda cheo, ila atanikabidhi kwa Mtu mwingine.
Alinikabidhi kwa Mdada anaitwa Alice (ana asili ya kichaga) huyu dada ndio sababu hasa ya kuja kuomba ushauri hapa.
Nilimwambia nahitaji mkopo wa Tsh. 1,500,000/- nilifanya hivi kwakua lengo hasa nilitaka mkopo wa 1M lakini nilijua wanaweza punguza kama walivyonifanyia mwanzo hivyo nikaona niongeze hii 500,000/-
Huyu dada alinizungusha sana, kila nikimpigia simu waje kunitembelea alikuwa haishi Sababu. Nikajua ni walewale wanaohitaji RUSHWA nilimtumia Tsh. 25,000/- ilikuwa ni J3 hiyo siku, wakaja kunitembelea J5.
Kama kawaida akanielekeza kwa Mwanasheria , sikufanya hivyo tena, nikaenda States Attorney. Na huu mkopo nimeumaliza.
Sasa nilipotaka mkopo mwingine nikaona kama kuna kukwepana sana , nikamtuma MKE wangu, yeye ni mtumishi wa Umma. (Mwalimu) nikamwambia aende akope 2M.
Wameomba LAKI TATU ili waweze kutoa huu mkopo. Huyu dada anayeitwa Elice akiwa ni Mmoja wao.
Naomba ushauri Ndugu zangu.
Naomba kuwasilisha.
Leo nimekuja hapa barazani kufikisha kero yangu kwa benki ya NMB tawi la Mbalizi road MBEYA.
Mwaka 2013 mwezi wa Nne (04) nilienda kwenye ofisi zao, kwa minajili ya kuomba mkopo. Nilipofika pale nilikutana na Loan officer alijitambulisha kwa jina la Kirungeme.
Katika hatua za awali niliweza pata ushirikiano wa kutosha kwa huyu mfanyakazi. Nilipokamilisha hatua zote ikiwemo ile ya kuja kunitembelea na kuangalia shughuli zangu. Bank iliamua kunipa mkopo wa Tsh. 500,000/- ingawa niliomba Tsh. 1,000,000/-
Kadhia ilianza hapa;
Niliombwa pesa ya mafuta ya gari kwa kuja kunitembelea niliwapa 15,000/- (ilinibidi kutoa maana nilikuwa na shida hasa na ule mkopo)
Akanielekeza kwa mwanasheria atakaye gonga Muhuri na kunitajia kabisa kiwango cha kumlipa (niliambiwa nikamlipe 50,000/-) hili sikulifanya maana, nilienda States attorney nikapigiwa muhuri kwa 10,000/- na kuzirudisha form Bank. Nilipo zikabidhi form za mkopo kwa loan officer huyu alianza kugomba kwanini sijaenda kwa mwanasheria aliyenitajia!
Nilifanikiwa kuchukua mkopo, na kufanya marejesho kila mwezi kama mkataba wetu ulivyokuwa umeelekeza. Baada ya kukamilisha Marejesho, na kufanikiwa kulipa mkopo wote nilienda tena Bank n kukutana na Kirungeme akaniambia yeye kapanda cheo, ila atanikabidhi kwa Mtu mwingine.
Alinikabidhi kwa Mdada anaitwa Alice (ana asili ya kichaga) huyu dada ndio sababu hasa ya kuja kuomba ushauri hapa.
Nilimwambia nahitaji mkopo wa Tsh. 1,500,000/- nilifanya hivi kwakua lengo hasa nilitaka mkopo wa 1M lakini nilijua wanaweza punguza kama walivyonifanyia mwanzo hivyo nikaona niongeze hii 500,000/-
Huyu dada alinizungusha sana, kila nikimpigia simu waje kunitembelea alikuwa haishi Sababu. Nikajua ni walewale wanaohitaji RUSHWA nilimtumia Tsh. 25,000/- ilikuwa ni J3 hiyo siku, wakaja kunitembelea J5.
Kama kawaida akanielekeza kwa Mwanasheria , sikufanya hivyo tena, nikaenda States Attorney. Na huu mkopo nimeumaliza.
Sasa nilipotaka mkopo mwingine nikaona kama kuna kukwepana sana , nikamtuma MKE wangu, yeye ni mtumishi wa Umma. (Mwalimu) nikamwambia aende akope 2M.
Wameomba LAKI TATU ili waweze kutoa huu mkopo. Huyu dada anayeitwa Elice akiwa ni Mmoja wao.
Naomba ushauri Ndugu zangu.
Naomba kuwasilisha.