Niulize kuhusu mapishi ya futari mbalimbali

Mi naomba unijuze jinsi ya kupika kachori

Mahitaji:
Viazi ,Kitunguu saumu(galic) na Tangawizi iliosagwa,Chumvi,Pilipili ya kusaga kutegemea na unavyoipenda,Ndimu,Mafuta ya kupikia,Unga wa dengu au Ngano Kiasi.


NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Chemsha viazi mpaka viiive, kisha vitoe maganda na uviweka ndani ya bakuli.
2. Vipondeponde kwa mkono mpaka viwe laini(viponde kabla ya kupoa)
3. Saga vitunguu saumu na tangawizi kisha changanya na viazi .
4. Weka chumvi, ndimu na pilipili ya unga kisha uonje, unaweza kuongeza viungo hivi kwa kadri ya mapenzi yako.
5. Tengeneza madonge ya duara uyapange katika tray.
6. Vuruga unga wa dengu au ngano kwa maji uwe mwepesi kidogo.
7. Weka mafuta ya kupikia ndani ya karai na uliweke kwenye moto.
8. Chovya madonge kwenye unga na uyatose kwenye mafuta ya moto. (Uchomaji wake ni kama kuchoma bajia)
9. Wacha kachori zibadilike rangi kuwa ya njano na uzitoe kwenye mafuta.
10. Weka Kachori kwenye sahani zipoe tayari kwa kuliwa na chatne na juice au chai.
 
Naomba unielekeze kupika BIRIANI


Mahitaji
1 kilo mchele wa basmati

1 kilo nyama iwe ya kuku au ng'ombe au mbuzi kata katika umbo dogo la kutosha kula kisha ichemshe na tangawizi na kitunguu swaumu, unga wa binzari (turmeric powder) pili pili manga na chumvi ili kuweka ladha nzuri. Ikisha iva itoe iweke pembeni na mchuzi wake uweke pembeni utautumia baadae.

1 kilo ya vitunguu kata slice ( mviringo)

1 kilo nyanya nyekudu zilizoiva, osha vizuri kisha katakata saizi ndogo ndogo sana

1/2 lita ya mafuta ya kupikia

1/2 kilo ya samli au mafuta yeyote ya kupikia

2 maggi chicken soup cubes

3 kijiko kidogo cha chai unga wa pilipili mwekundu

1/2 kijiko kidogo cha chai unga wa binzari

3 kijiko kidogo cha chai unga wa girigilani (giligilani)

2 kijiko kikubwa cha chakula mchanganyiko wa tangawizi na kitunguu swaumu vilivyosagwa

korosho iliyo kaangwa usizisage zibaki nzima robo kikombe

majani ya girigilani kichanga kimoja

mbegu za nzima ya hiriki kiasi

Pili pili manga nzima kiasi

Chumvi kiasi

Jinsi ya kuanda

Weka mafuta katika sufuria yako iliyo juu ya moto tayari, kisha kaanga nyama yako iliyokwisha chemshwa mpaka iwe na rangi ya kahawia (golden brown)

Kisha itoe nyama hiyo na ichuje mafuta ili mafuta yanayobaki weka kitunguu na endelea kukaanga kwa dakika 7-10 kisha weka unga wa binzali, unga wa pili pili mwekundu, unga wa girigilani, mbegu za hiriki na nusu ya mbegu za pili pili manga.

Changanya vizuri mpaka utapata mchanganyiko mzuri mkavu miminia humo maji uliyotunza baada ya kuchemshia ile nyama yako na kuiweka pembeni ipoe. kisha weka nyanya fresh ndani ya sufuria yako pika mpaka maji yakauke na mafuta yaanze kuoneka kwa juu ndani ya sufuria.

Kisha weka nyama yako ndani ya sufuria pole pole halafu punguza moto acha ijipike kwa muda mpaka mchuzi wako na nyama vikamate ladha pia usisahau kuweka chumvi kulingana na ladha unayopenda.

Chukua sufuria nyingine weka mafuta ya samli na vitunguu ilivyoslice kisha kaanga na majani ya girigilani, korosho funika kwa dakika 10 i, kisha weka mchele wako mkavu uliokwisha oshwa vizuri na uchanganye vizuri ongeza vikombe 5 vya maji na chumvi kidogo mchele ukishaanza kuchemka funika sufuria lako na punguza moto maji yakisha kauka kiasi weka mchanganyiko wa ile nyama yako nusu tu juu ya wali wa basmati acha wali uive kabisa kisha itakua tayari kula na pakua chakula chako kikiwa cha moto
 
Mie nataka kuelewa namna ya kupika sambusa za nyama.

Halafu kwa nini kila ninapopika huwa naugnua sana bana.

Au mikono yangu ina matege.??
Mahitaji

Nyama ya kusaga (minced beef 1/4 kilo)Vitunguu maji vilivyokatwakatwa(diced onion 2 vikubwa )Kitunguu swaum/ tangawizi (garlic and ginger paste 1 kijiko cha chakula)Chumvi (salt)Pilipili iliyokatwakatwa (scotch bonnet 1)Limao (lemon 1/2)Curry powder 1/2 kijiko cha chaiCinnamon powder 1/4 kijiko cha chaiCoriander powder 1/4 kijiko cha chaiCumin powder 1/4 kijiko cha chaiUnga wa ngano (all purpose flour kidogo)Manda za kufungia (spring roll pastry) Giligilani (fresh coriander kiasi)Mafuta ya kukaangia

Matayarisho

Changanya nyama na limao, chumvi, pilipili,kitunguu swaum, tangawizi na spice zote, kisha pika katika moto wa kawaida mpaka nyama iive na maji yote yakauke. Baada ya hapo kabla hujaipua nyama tia vitunguu na giligilani na uvipike pamoja kwa muda wa dakika 2 na uipue weka pembeni na uache viipoe. Baada ya hapo tia unga kidogo katika bakuli nauchanganye na maji kidogo kupata uji mzito kwa ajili ya kugundishia manda. Baada ya hapo tia nyama katika manda na kisha zifunge kwa kugundishia na unga wa ngano.Ukisha maliza kuzifunga zote zikaange mpaka ziwe za brown na uzitoe. Na hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.

7fe2ad603fdb18bc6a71531ac9499d3e.jpg
1c55aff5e0cc37591d0b2d483410bf37.jpg



8a88cde2c4f1c572669cd3f7d6412295.jpg
 
NAOMBA NIELEKEZE JINSI YA KUPIKA TAMBI NZURI ZA RANGI NA HARUFU NZURI.
Mahitaji

Tambi (spaghetti 1/2 ya packet)Mafuta (vegetable oil)Sukari (sugar 1/2 kikombe cha chai)Hiliki (cardamon 1/2 kijiko cha chai)Chumvi (salt 1/2 kijiko cha chai)Tui la nazi (coconut oil 1 kikombe cha chai)Maji kiasi



Matayarisho

Tia mafuta kiasi kwenye sufuria kisha ibandike jikoni (katika moto wa wastani) yakisha pata moto kiasi tia tambi na uanze kuzikaanga kwa kuzigeuzageuza kila mara mpaka zitakapokuwa za yangi ya light brown. baada ya hapo ipua na umwage mafuta ya kwenye tambi (bakiza kidogo sana kwani usipofanya hivyo tambi zitakuwa na mafuta sana) Baada ya hapo zirudishe jikoni na kisha utie hiliki, chumvi, sukari, tui la nazi na maji kiasi. Zifunike kisha ziache zichemke mpaka maji yakauke. Baada ya hapo zigeuze na uzipike mpaka ziive. Nahapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.

1bc08a1a4daeb29683667d1a2fc7c56c.jpg
 
Mie nataka kuelewa namna ya kupika sambusa za nyama.

Halafu kwa nini kila ninapopika huwa naugnua sana bana.

Au mikono yangu ina matege.??
Pole kwa kuungua tumia vitambaa kushiia sufuria
 
Mahitaji:
Viazi ,Kitunguu saumu(galic) na Tangawizi iliosagwa,Chumvi,Pilipili ya kusaga kutegemea na unavyoipenda,Ndimu,Mafuta ya kupikia,Unga wa dengu au Ngano Kiasi.


NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Chemsha viazi mpaka viiive, kisha vitoe maganda na uviweka ndani ya bakuli.
2. Vipondeponde kwa mkono mpaka viwe laini(viponde kabla ya kupoa)
3. Saga vitunguu saumu na tangawizi kisha changanya na viazi .
4. Weka chumvi, ndimu na pilipili ya unga kisha uonje, unaweza kuongeza viungo hivi kwa kadri ya mapenzi yako.
5. Tengeneza madonge ya duara uyapange katika tray.
6. Vuruga unga wa dengu au ngano kwa maji uwe mwepesi kidogo.
7. Weka mafuta ya kupikia ndani ya karai na uliweke kwenye moto.
8. Chovya madonge kwenye unga na uyatose kwenye mafuta ya moto. (Uchomaji wake ni kama kuchoma bajia)
9. Wacha kachori zibadilike rangi kuwa ya njano na uzitoe kwenye mafuta.
10. Weka Kachori kwenye sahani zipoe tayari kwa kuliwa na chatne na juice au chai.
Thank you
 
naomba kujua ile source ya biriani inapikwaje mpk inakua nzito vile plus viungo vyake ni vipii
 
Mahitaji

Tambi (spaghetti 1/2 ya packet)Mafuta (vegetable oil)Sukari (sugar 1/2 kikombe cha chai)Hiliki (cardamon 1/2 kijiko cha chai)Chumvi (salt 1/2 kijiko cha chai)Tui la nazi (coconut oil 1 kikombe cha chai)Maji kiasi



Matayarisho

Tia mafuta kiasi kwenye sufuria kisha ibandike jikoni (katika moto wa wastani) yakisha pata moto kiasi tia tambi na uanze kuzikaanga kwa kuzigeuzageuza kila mara mpaka zitakapokuwa za yangi ya light brown. baada ya hapo ipua na umwage mafuta ya kwenye tambi (bakiza kidogo sana kwani usipofanya hivyo tambi zitakuwa na mafuta sana) Baada ya hapo zirudishe jikoni na kisha utie hiliki, chumvi, sukari, tui la nazi na maji kiasi. Zifunike kisha ziache zichemke mpaka maji yakauke. Baada ya hapo zigeuze na uzipike mpaka ziive. Nahapo zitakuwa tayari kwa kuliwa.

1bc08a1a4daeb29683667d1a2fc7c56c.jpg
My dear, tambi hizi zinaitwa pasta.
Spaghetti ni zile ndefu kama vijiti na mara nyingi zinapikwa za chumvi na mchuzi kama macaroni.
 
Back
Top Bottom