GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 4,839
- 6,573
Mimi ni Mkristo. Niaminivyo, chanzo cha ndoto inaweza ikawa:
1. Ujumbe kutoka kwa Mungu
2. Kazi ya Shetani kwa lengo la kuharibu
3. Uchovu wa mwili na aina ya mawazo uliyokuwa ukiyawaza kabla ya kulala.
Hivi karibuni, nimeota ndoto ambayo mpaka sasa bado sijapata tafsiri yake.
Niliota natembea njiani na vijana wawili, na ghafla , nikaona noti ya sh 1,000/= mbele yangu.
Nilipoiona, nilijisemea kuwa kama nimetegeshewa kichawi, basi itakuwa "imekula" kwao walioitegesha kwa sababu nitaichukua na kuitakasa kwa Jina la Yesu na kuitumia bila madhara yoyote. Niliamua kuchukua, na mara tu baada ya kuiokota, niliziona zingine nyingi, noti za shilingi 1,000/= na za 2,000/=. Niliendelea kuziokota, na nikawaambia vijana wawili niliokuwa nao kuwa na wao waokote.
Baada ya kuiokota kiasi kikubwa, ziliisha na hatimaye tukaendelea na safari kila mmoja akiwa na noti zake. Muda wote nilikuwa makini kuzishikilia huku nikiendelea kuziombea ili kama zilikuwa na nguvu za giza zisiweze kuwa na athari kwangu.
Baada ya kutembea kidogo, tuliwakuta askari watatu wa usalama barabarani wakiwa wamesimama pembezoni mwa barabara. Mmoja wao, akiwa katika sare za kazi, alinifuata na kuniambia hela tuliyoiokota ni ya kwake hivyo nimrudishie.
Kwanza, nilitaka kukataa kumpa. Lakini aliponiambia kuwa walituona tokea tulipokuwa tunaokota hizo fedha, nilipatwa na mshutuko, nikagundua kuwa huyo trafiki si binadamu wa kawaida. Aliwezaje kutuona wakati tulikookotea ni mbali?
Pale pale nilianza kumkemea kwa Jina la Yesu, na ghafla yule trafiki akaanza kubadilika kuanzia sura, umbo mpaka na mavazi.
Mavazi yake ya utrafiki (meupe) yalipoteza uweupe na kufanania kwa mbali sare za wafungwa. Na umbile la huyo askari lilibadilika kutoka wa kiume na kuwa wa kike.
Nilipoendelea kumkemea, alidondoka chini na kuwa kama anayegugumia kwa maumivu.
Vijana wawili niliokuwa nao waliondoka kwa muda na kuniacha peke yangu nikiandelea kupambana na hicho kiumbe. Ni kama vile niliwaagiza kufuata kitu.
Wakati nikiendelea kumkemea, nilimhoji sababu ya kunitegeshea pesa, akasema walinipenda. Nilipomwuliza kama hiyo hela ingewaathiri na hao vijana wawili waliookota, alisema ingewaathiri kama wangekubaliana nao.
Baada ya kusema hivyo, nilikazana kuomba kwa bidii, lengo sasa likiwa hicho kiumbe kipotee kwa kuyeyuka.
Hiyo ndoto inamaanisha nini?
Nini chanzo chake?
Asanteni.
1. Ujumbe kutoka kwa Mungu
2. Kazi ya Shetani kwa lengo la kuharibu
3. Uchovu wa mwili na aina ya mawazo uliyokuwa ukiyawaza kabla ya kulala.
Hivi karibuni, nimeota ndoto ambayo mpaka sasa bado sijapata tafsiri yake.
Niliota natembea njiani na vijana wawili, na ghafla , nikaona noti ya sh 1,000/= mbele yangu.
Nilipoiona, nilijisemea kuwa kama nimetegeshewa kichawi, basi itakuwa "imekula" kwao walioitegesha kwa sababu nitaichukua na kuitakasa kwa Jina la Yesu na kuitumia bila madhara yoyote. Niliamua kuchukua, na mara tu baada ya kuiokota, niliziona zingine nyingi, noti za shilingi 1,000/= na za 2,000/=. Niliendelea kuziokota, na nikawaambia vijana wawili niliokuwa nao kuwa na wao waokote.
Baada ya kuiokota kiasi kikubwa, ziliisha na hatimaye tukaendelea na safari kila mmoja akiwa na noti zake. Muda wote nilikuwa makini kuzishikilia huku nikiendelea kuziombea ili kama zilikuwa na nguvu za giza zisiweze kuwa na athari kwangu.
Baada ya kutembea kidogo, tuliwakuta askari watatu wa usalama barabarani wakiwa wamesimama pembezoni mwa barabara. Mmoja wao, akiwa katika sare za kazi, alinifuata na kuniambia hela tuliyoiokota ni ya kwake hivyo nimrudishie.
Kwanza, nilitaka kukataa kumpa. Lakini aliponiambia kuwa walituona tokea tulipokuwa tunaokota hizo fedha, nilipatwa na mshutuko, nikagundua kuwa huyo trafiki si binadamu wa kawaida. Aliwezaje kutuona wakati tulikookotea ni mbali?
Pale pale nilianza kumkemea kwa Jina la Yesu, na ghafla yule trafiki akaanza kubadilika kuanzia sura, umbo mpaka na mavazi.
Mavazi yake ya utrafiki (meupe) yalipoteza uweupe na kufanania kwa mbali sare za wafungwa. Na umbile la huyo askari lilibadilika kutoka wa kiume na kuwa wa kike.
Nilipoendelea kumkemea, alidondoka chini na kuwa kama anayegugumia kwa maumivu.
Vijana wawili niliokuwa nao waliondoka kwa muda na kuniacha peke yangu nikiandelea kupambana na hicho kiumbe. Ni kama vile niliwaagiza kufuata kitu.
Wakati nikiendelea kumkemea, nilimhoji sababu ya kunitegeshea pesa, akasema walinipenda. Nilipomwuliza kama hiyo hela ingewaathiri na hao vijana wawili waliookota, alisema ingewaathiri kama wangekubaliana nao.
Baada ya kusema hivyo, nilikazana kuomba kwa bidii, lengo sasa likiwa hicho kiumbe kipotee kwa kuyeyuka.
Hiyo ndoto inamaanisha nini?
Nini chanzo chake?
Asanteni.