Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,871
- 155,836
Nimekaa na kuwazua hivi je ni kwanini wachawi ni watu masikini sana na wanaoishi maisha duni yasiyo na mbele wala nyuma?
Nimewaza na kuwazua lakini jibu sijalipata.
Mimi binafsi natamani sana ningekuwa mchawi.
Ningekuwa mchawi ningeifanya mapinduzi ya kisayansi.
Sayansi ya gizani ningeiweka mwangani.
Ungo wangu ningekuwa naupaki pale ubungo,
kipindi cha xmas nauli zikipanda mie navunja bei.
Natangaza nauli elfu tano tu.
Naamini hiyo ingenisaidia sana ku busti kipato cha familia yangu.
Ningewachukua msukule wahandisi wote wakali wa dunia hii na kuwaleta hapa bongo niwatumikishe watujengee viwanda, reli na mitambo kwa gharama ya pumba.
Yaani natamani sana niwe mchawi ili nilikomboe taifa hili maana aliyeliroga kisha kufa,
na sasa tunahitaji mchawi mwenye roho ya uzalendo na taifa letu.
Nimewaza na kuwazua lakini jibu sijalipata.
Mimi binafsi natamani sana ningekuwa mchawi.
Ningekuwa mchawi ningeifanya mapinduzi ya kisayansi.
Sayansi ya gizani ningeiweka mwangani.
Ungo wangu ningekuwa naupaki pale ubungo,
kipindi cha xmas nauli zikipanda mie navunja bei.
Natangaza nauli elfu tano tu.
Naamini hiyo ingenisaidia sana ku busti kipato cha familia yangu.
Ningewachukua msukule wahandisi wote wakali wa dunia hii na kuwaleta hapa bongo niwatumikishe watujengee viwanda, reli na mitambo kwa gharama ya pumba.
Yaani natamani sana niwe mchawi ili nilikomboe taifa hili maana aliyeliroga kisha kufa,
na sasa tunahitaji mchawi mwenye roho ya uzalendo na taifa letu.