Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,528
- 8,187
Leo nimepita shule ya msingi Upendo iliyopo Mbezi Luis jijini Dar es Salaam. Kwanza shule ina wanafunzi wengi kuliko uwezo wa madarasa mpaka wanaingia kwa shift.
Pili shift husika inabeba wanafunzi wengi mpaka wengine wanakaa chini tena sio chini kwenye sakafu, ni chini kwenye mchanga. Unaweza kusema labda wamechelewa kumalizia sakafu kipindi hiki cha kufungua shule, madarasa yamechakaa yakionekana ni ya muda mrefu bila kuwekwa sakafu. Mwalimu hawezi kupata morali ya kufundisha kwenye madarasa hayo na ratiba iliyomzidia.
Hivi ule mkopo wa benki ya dunia ndio walisema wamepeleka kwenye madarasa? Na pesa za Tozo wakasema zinaingia humohumo..
Pichani ni wanafunzi wa darasa la 3C shule ya msingi Upendo iliyopo Mbezi Luis Dar es Saalam wakiendelea na vipindi baada ya shule kufunguliwa
Pili shift husika inabeba wanafunzi wengi mpaka wengine wanakaa chini tena sio chini kwenye sakafu, ni chini kwenye mchanga. Unaweza kusema labda wamechelewa kumalizia sakafu kipindi hiki cha kufungua shule, madarasa yamechakaa yakionekana ni ya muda mrefu bila kuwekwa sakafu. Mwalimu hawezi kupata morali ya kufundisha kwenye madarasa hayo na ratiba iliyomzidia.
Hivi ule mkopo wa benki ya dunia ndio walisema wamepeleka kwenye madarasa? Na pesa za Tozo wakasema zinaingia humohumo..
Pichani ni wanafunzi wa darasa la 3C shule ya msingi Upendo iliyopo Mbezi Luis Dar es Saalam wakiendelea na vipindi baada ya shule kufunguliwa