Nimesikia Misri chini ya Elsisi inatamani Hamas ishindwe lakini wanaiogopa Ikhwanul muslimiin

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,183
10,913
Ikhwanul Muslimiin ni harakati kongwe sana nchini Misri ambayo hatimae iliweza kupenya mataifa kadhaa ya kiislamu.
Upeo wa mafanikio wa Ikhwaan au muslim brotherhood ni pale chama hicho kilipoweza kupanda madarakani mwaka 2012 chini ya raisi Mohammed Morsi.Hiyo ni baada ya vuguvugu lililomuodoa madarakani raisi Hosni Mubarak.
Kiongozi huyo ambaye alikuwa injinia kielimu na aliyesomea na kufundisha nchini Marekani alionekana ni tishio kubwa kwa nchi za magharibi na nchi jirani ya Israel.Baada ya mwaka mmoja tu harakati pinzani dhidi yake zilifanywa na hatimae kupinduliwa na jeshi na kupelekea Elsisi kushika madaraka huku Mohammed Morsi akiwekwa ndani kwa tuhuma kadhaa za kuzushiwa.
Kumpindua Morsi na kukaa madarakani kwa Elsisi kulikuja kwa gharama kubwa sana ya mauwaji ya kikatili kuliko hata yale yaliyofanywa na China kule Tianmen square.
Pamoja na kuendelea kukaa madarakani serikali ya Elsisi imekuwa na hofu kubwa ya kupinduliwa tena na harakati za muslim brotherhood.
Nchini Misri kuna wafuasi wengi sana wa harakati hizo za ikhwaanil muslimiin na wamekuwa wakiwaunga mkono Hamas wakona ni kama muendelezo wa serikali yao iliyopinduliwa Misri.Nguvu kubwa waliyopata Hamas imetokana na kuungwa mkono na watu waliopo Misri ambao baadhi wana nafasi serikalini.
Kwa ujumla viongozi wakuu wa serikali ya Misri wameshindwa kuiunga mkono wazi wazi Hamas wakati huu wa vita kwa vle wanaiona ni muendelezo wa harakati za Ikhawaanul muslimiin.
Kwa upande mwengine serikali hiyo haiwezi kuwakana moja kwa moja kwani kufanya hivyo kutaleta msuguano mkubwa wa waungaji mkono wake ambao ni wengi nchini Misri.
Hiyo ni sababu mojawapo ambayo serikali ya Misri imeweka nia ya kuzuia Israel kudhibiti mpaka wa Rafaha kama ambavyo wametangaza kwani kufanya hivyo kutapelekea machafuko makubwa ndani ya Misri.
 
Ikhwan muslim itarudi. Uislam utashinda na utasimama dunia nzima
Hicho ndicho kinachowaponza mnaonekana ni mawakala wa ibilisi kushabikia machafuko hubirini dini yenu kwa wema na amani watu washashtukia kwamba uislam sio dini ni ideology tu.Kueneza itikadi inabidi uwe na utimamu wa akili.
 
hivi uislam ni chama cha siasa siyo? kuna wakati nawaonea huruma hasa nikiangalia aljazeera. lakini kwa kauli kama hizi alijisemeaga mzee Pinda...
Uislamu sio tu chama cha kisiasa uislam ni kila unalolifanya kuanzia kuamka mpaka kulala siasa uchumi diplomasia burudani nk nk....
 
Hicho ndicho kinachowaponza mnaonekana ni mawakala wa ibilisi kushabikia machafuko hubirini dini yenu kwa wema na amani watu washashtukia kwamba uislam sio dini ni ideology tu.Kueneza itikadi inabidi uwe na utimamu wa akili.
Sisi na papa nani wakala wa ibilisi yaani mtu anaetaka muoane wenyewe kwa wenyewe kwenu ndio malaika
Wakristo mmepotoka sana hakuna sehemu waislam ama uislam unalingania na kusambaza dini bila amani
 
Kwani ukristo ni imani ambayo haijaenea kila nyanja ndg?. Tatizo lenu ni kutoheshimu imani za watu.
Hakuna shaka katika hilo.Tunamuheshimu sana mtume Issa (Yesu) a.s na ni mtume wa Allah aliyepewa miujiza ya aina yake na ambaye ni muislamu
Kwa upande wa ukristo umeenea mabara yote lakini haujaenea kila nyanja ya maisha na huwezi kutetea hilo.Kama umeenea kila nyanja basi habari za ushoga zisingekuwa zinamchanganya mpaka papa Francis.
 
Uislamu sio tu chama cha kisiasa uislam ni kila unalolifanya kuanzia kuamka mpaka kulala siasa uchumi diplomasia burudani nk nk....
Jee wanayo habari kuwa benki ni mfumo ulioanza na uislamu ambao kwa mara ya mwanzo waiengereza waliukopia kutoka nchi za kiislamu hasa wakati wa Ottoman empire.
Ukija kwenye afya na teknolojia za ufundi ndio kabisa hakuna anayeweza kuwabeza waislamu
 
Nyie wafia dini za watu weupe msio na akili hata kidogo , Je mtu anaweza kuishi hapa duniani kwa raha na mafanikio makubwa pasipo hizo dini??? Nyie watu kwanini mnawapambania watu wasio wapenda hata rangi za ngozi zenu?? Nyie mlitakiwa muoneshe kuumizwa na vifo vya waafrica wenzenu kule DRC na Sudan lakn mnajipendekeza kwa Jews na Arabs akili zenu hazina akili .
 
Yan kuna mipumbavu kila siku hizbullah hizbulah Mara IDF IDF sijui na mitakataka gani mingne , fungueni akili nyie mbuzi
 
Hakuna shaka katika hilo.Tunamuheshimu sana mtume Issa (Yesu) a.s na ni mtume wa Allah aliyepewa miujiza ya aina yake na ambaye ni muislamu
Kwa upande wa ukristo umeenea mabara yote lakini haujaenea kila nyanja ya maisha na huwezi kutetea hilo.Kama umeenea kila nyanja basi habari za ushoga zisingekuwa zinamchanganya mpaka papa Francis.
Alwaz, post: 49281052, member: 23239 1. Yesu siyo isa. Msome Yesu wa kwenye Bible achana na vitabu vingine. 2. Yesu hajawahi kuwa muislam huo ni uongo wa ibilisi. 3. Hakuna uhusiano wowote kati ya ukristo na ushoga. Huyo papa ni kiongozi wa dhehebu moja na anapozungumza hausemei ukristo. Ukristo ulishaga kataa ushoga siku nyingi 1 Wakorintho 6:9.. Mambo ya walawi 18:22. Mengine acha ninyamaze.
 
Jee wanayo habari kuwa benki ni mfumo ulioanza na uislamu ambao kwa mara ya mwanzo waiengereza waliukopia kutoka nchi za kiislamu hasa wakati wa Ottoman empire.
Ukija kwenye afya na teknolojia za ufundi ndio kabisa hakuna anayeweza kuwabeza waislamu
Eidha hawajui ama wanajua ila wanataka ukweli usijulikanike
Sababu uislamu na waislam ndio walileta maendeleo ya sayansi elimu technology nk karibu kwa 90%
 
Back
Top Bottom