Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 11,208
- 19,001
Nimeangalia video juu ya tukio la huyu mtu anaetuhumiwa kuua askari, na kuangalia kilichotokea.
Baada ya kuwa amemaliza risazi katika SMG ya pili aliyokuwa nayo na kunyoosha mikono juu, polisi walimpiga risasi ambayo ilimfanya aanguke chini. Hakukuwa na haja tena kuendelea kumpiga risasi mtu ambaye amejeruhiwa kaanguka chini.
Alipokuwa amejeruhiwa na kuanguka chini, Polisi waliendelea kumpiga risasi akiwa amelala chini ambazo nimehesabu na kukuta walimpiga risasi 19. Ajabu ni kwamba kundi lote lile la Polisi walifanikiwa kumpiga pale tu alipoishiwa risasi na kuonyesha wazi alishaamua kufa - maana alijifanya target rahisi sana.
Sasa hili lina maana gani? Ni wazi kwamba polisi wetu hawana weledi katika matukio kama haya, kwa kuwa baada ya kuwa umeona ameishiwa risasi na si tishio tena, jambo la msingi inabidi kuwa ni kumkamata akiwa hai ili kuweza kupata habari zaidi atakapodhibitiwa.
Kwa hiyo Polisi walipaswa kumkaribia kwa umakini katika formation ambayo kunakuwa na askari wanamsogelea wakiwa na silaha tayari, na wengine waanawa-cover askari wanaomsogelea katika kitu tunaita "flanks".
Lakini pia, kuna upande wa pili, kwamba huenda kuna askari walikusudia kumuua ili huyu mtu asitoe taarifa juu ya ugomvi wake na askari, maana mfu haongei!
Kwahiyo kuna conclusion tatu tu hapa, kwamba polisi wetu wako very unprofessional, incompetent, na pia walikusudia huyu mtu asitoke kwenye hili tukio akiwa hai.
Baada ya kuwa amemaliza risazi katika SMG ya pili aliyokuwa nayo na kunyoosha mikono juu, polisi walimpiga risasi ambayo ilimfanya aanguke chini. Hakukuwa na haja tena kuendelea kumpiga risasi mtu ambaye amejeruhiwa kaanguka chini.
Alipokuwa amejeruhiwa na kuanguka chini, Polisi waliendelea kumpiga risasi akiwa amelala chini ambazo nimehesabu na kukuta walimpiga risasi 19. Ajabu ni kwamba kundi lote lile la Polisi walifanikiwa kumpiga pale tu alipoishiwa risasi na kuonyesha wazi alishaamua kufa - maana alijifanya target rahisi sana.
Sasa hili lina maana gani? Ni wazi kwamba polisi wetu hawana weledi katika matukio kama haya, kwa kuwa baada ya kuwa umeona ameishiwa risasi na si tishio tena, jambo la msingi inabidi kuwa ni kumkamata akiwa hai ili kuweza kupata habari zaidi atakapodhibitiwa.
Kwa hiyo Polisi walipaswa kumkaribia kwa umakini katika formation ambayo kunakuwa na askari wanamsogelea wakiwa na silaha tayari, na wengine waanawa-cover askari wanaomsogelea katika kitu tunaita "flanks".
Lakini pia, kuna upande wa pili, kwamba huenda kuna askari walikusudia kumuua ili huyu mtu asitoe taarifa juu ya ugomvi wake na askari, maana mfu haongei!
Kwahiyo kuna conclusion tatu tu hapa, kwamba polisi wetu wako very unprofessional, incompetent, na pia walikusudia huyu mtu asitoke kwenye hili tukio akiwa hai.