Nimegundua wale watu ambao hawanywi pombe ndio wanafiki, wachawi na wambea

Hivi kwanini mkinywa pombe Huwa mnakunja sura?

Kwani Huwa mnakuwa mmelazimishwa?

Kwann Huwa mnakunja sura kama mtu anayedungwa sindano?
 
Iko hivi,

nina marafiki wa kila aina tofauti tofauti, walevi na wasio walevi..mimi binafsi ni mywaji mzuri tu ila sio wa kubebwa.

Sasa siku kadhaa za nyuma hapo nilipata kachangamoto flani ka kimaisha nikaona ngoja niwacheck jamaa zangu(bila kujali ni mlevi au mtakatifu kama wanavyojiita) Wale walevi fresh tu aliyekua nacho chochote kitu basi kwa muda wake aliniwezesha chochote kitu ambae hakua na kitu alinichana tu hana na issue ikaisha.

Sasa hawa wasiokunywa ndio wale nawacheck wananikataa halafu wanaenda huko pembeni wanasema ooh nalewa daily nashindwaje kutatua shida ka hiyo mwenyewe hawajui sie wanywaji kuna wakati unaitwa tu bar na washkaji huna hata Mia na wao ndio wanasimamia show zote.

Sasa leo kuna pimbi ambae sio mnywaji kapatwa na changamoto kama iliyonikuta mimi kipindi kile na yeye alinikataa hakunichangia hata senti tano kanikuta leo niko njema tu, kwanza kanipigia sijapokea coz tuna muda hatujawasliana tangu alivyonikataa ila taarifa zake nazipata toka kwa CIA wangu mmoja hivi, alivyonipa faili lake huyu jamaa nimemkataa kabisa.

Kwa kifupi nimegundua sie wanywaji tunasaidiana sana kuliko hao wanaojiita sijui waimba kwaya.
Endela kunywa mkojo wa Firauni baba.
 
Back
Top Bottom