Kaka elnino nashukuru kwa thread yako lakini tahadhari. Mimi nimelima mwaka huu mvua zimekataa nilikuwa na malengo kama yako lakini kilimo kwanza kimeniponza.nimepeleka mshahara wangu wa miezi minne shambani imekula kwangu.lakini kwa moro nafikiri hali ya hewa ni tofauti na kwetu,wape tahadhari wanaotaka kulima wawe makini wasije kichwakichwa
1. Watafute eneozuri la kulima
2. Wawe na mtaji wa kutosha
3. Wawe tayari kuingia shambani kusimamia [kilimo si mchezo]
4. Wawe tayari kwa matokeo yoyote[kukosa au kupata] wakishakubali tuwakaribishe
Thank you ELININO, but remember life doesn't keep other things constant. If GOD wish you will leave in your dreamz may GOD help you in this plan.JF
Hali ya uchumi ni ngumu sana kwa watu wote hasa tunategemea mwisho wa mwezi. Weekend nilijaribu kupiga hesabu za mishahara yangu in next 10 years....ooooooooooops hazikufika hata 500millions Tshs.
Kwa maneno mengine kama sintantafuta kitu mbadala mbali na mshahara wangu cha kufanya basi nishakufa maskini na sintakuwa na chochote cha kuwaachia wanangu.
Maisha ni magumu sana kadri siku zinavyoenda mbele, sasa nimeamua kuanza kilimo kwa mara ya pili, awamu hii natumia mshahara wangu kama mtaji, nimewaambia kwa mara ya pili sababu kilimo cha kwanza nilifanya pamoja na wazazi wangu hadi nilipomaliza form four miaka hiyo, hicho hakikuwa na manufaa yeyote sababu ya mtaji na ufahamu.
Kwa sasa nimeanza na heka 50 ( 70m by 70m), nipo morogoro - pale Tuliani. Heka zote zimeshalimwa sasa tunapanda - nita expand my project up to 1,000 in next 3 - 5 years.
Makadirioni kwamba kila hekari average ni gunia 30, nitategemea kupata gunia 1500 za mahindi kutokana na hekari zangu za sasa 50. Kila gunia average selling price ni Tshs 60,000. kwa hiyo nitapata average Tshs 90m by July this year.
Running cost itakuwa approx 5m, so super profit ni 85m by July 2010.
Sasa 85m kwa mtu anayepokea sh 1million kwa mwezi ni mshahara wake wa miaka 7 na ushee-- teh teh teh teh
By next year nitaexpand to 200 hektas, nitalipima shamba langu na nijaribu kutafuta mikopo katika mabenki - or mbia toka SA au Zimbabwe. by 2015 wakati Dr Slaa anakuwa Rais wa nchi nitakuwa millionea. sasa ole wenu mseme nimefanya ufisadi.
This is a challenge to you JF- hasa mnaopata less than 5m per month - think twice and join me.
Kumbuka shairi la darasa la nne - Kama mkitaka mali mtayapata shambani - huu ni wosia.
Thank you ELININO, but remember life doesn't keep other things constant. If GOD wish you will leave in your dreamz may GOD help you in this plan.
Yupo shambani jamani. Kuweni na subira.
Heshima kwako El,
Mkuu vipi mahindi yanaendeleaje ?.Mimi nilikuwa Kabuku wiki iliyopita mahindi yameshaanza kukauka naanza kujiandaa na ununuzi wa magunia na dawa za kuzuia wadudu.Hali ya soko la mahindi ni mbaya sana gunia moja la mahindi [debe sita] ni Tshs. 21,000/=,hali itazidi kuwa mbaya kipindi wakulima watakapoanza kuvuna kuanzia mwezi wa tisa na kuendela.Ujanja hapa ni kuhifadhi mpaka hali ya soko itakapokuwa nzuri.
Sijui soko la EAC kama litaweza kutusaidia kupata bei nzuri.