Nilichojifunza uchaguzi wa Arumeru

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Kuna mambo mengi nimejifunza kutokana Kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru, Haya ni baadhi yake.

Tume ya uchaguzi bado haiaminiki na vyama vya Upinzani. Na kadri siku zinavyokwenda ndivyo shaka za tume hiyo kutumiwa kuipa ushindi CCM inavozidi kuongezeka. Na CCM nayo imeanza kuwa na shaka na Tume hiyo.

Vyama vikubwa viwili kwenye kampeni hizo (CHADEMA na CCM) vinatumia mbinu za kuhama na mashabiki wake kutoka sehemu moja kwenda kwingine. Kutokana na Jimbo hilo kuwa karibu na Arusha mashabiki wa vyama hivyo wanaoishi Arusha wanahudhuria kwa wingi kwenye mikutano ya vyama hivyo.

Vyombo vya habari vimeshachukua upande kwenye Kampeni hizi na ili upate ukweli wa hali ya mambo Arumeru ni lazima uwasiliane na watu wasio na upande wowote walioko Arumeru. Vyombo vya habari haviaminiki TENA.

CCM ina uwezo mkubwa sana wa kutumia taasisi za dini kuendeshea kampeni zake kuliko wapinzani wake.

Wapinzani wa CCM wanalalamika CCM inatumia rushwa kwenye kampeni lakini hawaziamini taasisi za kupambana na Rushwa na matokeo yake hawaripoti tuhuma hizo kwenye taasisi hizo zaidi ya kuzisema kwenye majukwaa ya Kampeni.

Lowassa bado ana ushawishi chanya au hasi kwenye siasa za Tanzania, ndiyo maana kila mtu anatamani afanye kampeni Arumeru ili ama "amalizwe" au "awaonyeshe kazi" wapinzani wake.

Kwenye kampeni hakuna ushindani wa sera au ubishani wa tofauti za kutatua matatizo ya wana Arumeru badala yake kumejaa tambo nani atashinda, kuumbuana, kampeni za kifahari, uzushi,kutukanana, kudhalilishana, kutishana, na mwisho wa yote sintofahamu isiyo na lazima.

Nafasi ya mwanamke kwenye Kampeni bado ni kama haipo kwenye siasa za Tanzania. Kwenye Kampeni ya vyama vyote hakuna hata chama kimoja ambacho msemaji wake mkuu ni mwanamke. Wanawake waliopo Arumeru ni wapasha joto Microphone kabla "wenyewe" hawajapanda jukwaani.

Na la mwisho na muhimu,ni kwamba mwaka 2015 mtu atakaye tumia falsafa za Mwalimu kuombea kura ndiye atakayekuwa Rais wetu.
 
Kuna mambo mengi nimejifunza kutokana Kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru, Haya ni baadhi yake.

Tume ya uchaguzi bado haiaminiki na vyama vya Upinzani. Na kadri siku zinavyokwenda ndivyo shaka za tume hiyo kutumiwa kuipa ushindi CCM inavozidi kuongezeka. Na CCM nayo imeanza kuwa na shaka na Tume hiyo.

Vyama vikubwa viwili kwenye kampeni hizo (CHADEMA na CCM) vinatumia mbinu za kuhama na mashabiki wake kutoka sehemu moja kwenda kwingine. Kutokana na Jimbo hilo kuwa karibu na Arusha mashabiki wa vyama hivyo wanaoishi Arusha wanahudhuria kwa wingi kwenye mikutano ya vyama hivyo.

Vyombo vya habari vimeshachukua upande kwenye Kampeni hizi na ili upate ukweli wa hali ya mambo Arumeru ni lazima uwasiliane na watu wasio na upande wowote walioko Arumeru. Vyombo vya habari haviaminiki TENA.

CCM ina uwezo mkubwa sana wa kutumia taasisi za dini kuendeshea kampeni zake kuliko wapinzani wake.

Wapinzani wa CCM wanalalamika CCM inatumia rushwa kwenye kampeni lakini hawaziamini taasisi za kupambana na Rushwa na matokeo yake hawaripoti tuhuma hizo kwenye taasisi hizo zaidi ya kuzisema kwenye majukwaa ya Kampeni.

Lowassa bado ana ushawishi chanya au hasi kwenye siasa za Tanzania, ndiyo maana kila mtu anatamani afanye kampeni Arumeru ili ama "amalizwe" au "awaonyeshe kazi" wapinzani wake.

Kwenye kampeni hakuna ushindani wa sera au ubishani wa tofauti za kutatua matatizo ya wana Arumeru badala yake kumejaa tambo nani atashinda, kuumbuana, kampeni za kifahari, uzushi,kutukanana, kudhalilishana, kutishana, na mwisho wa yote sintofahamu isiyo na lazima.

Nafasi ya mwanamke kwenye Kampeni bado ni kama haipo kwenye siasa za Tanzania. Kwenye Kampeni ya vyama vyote hakuna hata chama kimoja ambacho msemaji wake mkuu ni mwanamke. Wanawake waliopo Arumeru ni wapasha joto Microphone kabla "wenyewe" hawajapanda jukwaani.

Na la mwisho na muhimu,ni kwamba mwaka 2015 mtu atakaye tumia falsafa za Mwalimu kuombea kura ndiye atakayekuwa Rais wetu.
Unategemea kweli kampeni za akina Vicent Nyerere , Lema , Sugu ziwe za kistaarabu kweli?
 
Unategemea kweli kampeni za akina Vicent Nyerere , Lema , Sugu ziwe za kistaarabu kweli?
Immature brain synthesis
D4PeXV3oAAAAABJRU5ErkJggg==
 
1.CCM ina uwezo mkubwa sana wa kutumia taasisi za dini kuendeshea kampeni zake kuliko wapinzani wake.

2.Kwenye kampeni hakuna ushindani wa sera au ubishani wa tofauti za kutatua matatizo ya wana Arumeru badala yake kumejaa tambo nani atashinda, kuumbuana, kampeni za kifahari, uzushi,kutukanana, kudhalilishana, kutishana, na mwisho wa yote sintofahamu isiyo na lazima.

3.Na la mwisho na muhimu,ni kwamba mwaka 2015 mtu atakaye tumia falsafa za Mwalimu kuombea kura ndiye atakayekuwa Rais wetu.

Mkuu nakuunga mkono hapo kwenye namba 2 ila sijakuelewa kwenye namba 1 na 3, singuka zaidi kwa ufafanuzi.
 
Kuna mambo mengi nimejifunza kutokana Kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru, Haya ni baadhi yake.

Tume ya uchaguzi bado haiaminiki na vyama vya Upinzani. Na kadri siku zinavyokwenda ndivyo shaka za tume hiyo kutumiwa kuipa ushindi CCM inavozidi kuongezeka. Na CCM nayo imeanza kuwa na shaka na Tume hiyo.

Vyama vikubwa viwili kwenye kampeni hizo (CHADEMA na CCM) vinatumia mbinu za kuhama na mashabiki wake kutoka sehemu moja kwenda kwingine. Kutokana na Jimbo hilo kuwa karibu na Arusha mashabiki wa vyama hivyo wanaoishi Arusha wanahudhuria kwa wingi kwenye mikutano ya vyama hivyo.

Vyombo vya habari vimeshachukua upande kwenye Kampeni hizi na ili upate ukweli wa hali ya mambo Arumeru ni lazima uwasiliane na watu wasio na upande wowote walioko Arumeru. Vyombo vya habari haviaminiki TENA.

CCM ina uwezo mkubwa sana wa kutumia taasisi za dini kuendeshea kampeni zake kuliko wapinzani wake.

Wapinzani wa CCM wanalalamika CCM inatumia rushwa kwenye kampeni lakini hawaziamini taasisi za kupambana na Rushwa na matokeo yake hawaripoti tuhuma hizo kwenye taasisi hizo zaidi ya kuzisema kwenye majukwaa ya Kampeni.

Lowassa bado ana ushawishi chanya au hasi kwenye siasa za Tanzania, ndiyo maana kila mtu anatamani afanye kampeni Arumeru ili ama "amalizwe" au "awaonyeshe kazi" wapinzani wake.

Kwenye kampeni hakuna ushindani wa sera au ubishani wa tofauti za kutatua matatizo ya wana Arumeru badala yake kumejaa tambo nani atashinda, kuumbuana, kampeni za kifahari, uzushi,kutukanana, kudhalilishana, kutishana, na mwisho wa yote sintofahamu isiyo na lazima.

Nafasi ya mwanamke kwenye Kampeni bado ni kama haipo kwenye siasa za Tanzania. Kwenye Kampeni ya vyama vyote hakuna hata chama kimoja ambacho msemaji wake mkuu ni mwanamke. Wanawake waliopo Arumeru ni wapasha joto Microphone kabla "wenyewe" hawajapanda jukwaani.

Na la mwisho na muhimu,ni kwamba mwaka 2015 mtu atakaye tumia falsafa za Mwalimu kuombea kura ndiye atakayekuwa Rais wetu.

Kwa 99% umenena kweli mkuu.
 
Kuna mambo mengi nimejifunza kutokana Kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru, Haya ni baadhi yake.

Tume ya uchaguzi bado haiaminiki na vyama vya Upinzani. Na kadri siku zinavyokwenda ndivyo shaka za tume hiyo kutumiwa kuipa ushindi CCM inavozidi kuongezeka. Na CCM nayo imeanza kuwa na shaka na Tume hiyo.

Vyama vikubwa viwili kwenye kampeni hizo (CHADEMA na CCM) vinatumia mbinu za kuhama na mashabiki wake kutoka sehemu moja kwenda kwingine. Kutokana na Jimbo hilo kuwa karibu na Arusha mashabiki wa vyama hivyo wanaoishi Arusha wanahudhuria kwa wingi kwenye mikutano ya vyama hivyo.

Vyombo vya habari vimeshachukua upande kwenye Kampeni hizi na ili upate ukweli wa hali ya mambo Arumeru ni lazima uwasiliane na watu wasio na upande wowote walioko Arumeru. Vyombo vya habari haviaminiki TENA.

CCM ina uwezo mkubwa sana wa kutumia taasisi za dini kuendeshea kampeni zake kuliko wapinzani wake.

Wapinzani wa CCM wanalalamika CCM inatumia rushwa kwenye kampeni lakini hawaziamini taasisi za kupambana na Rushwa na matokeo yake hawaripoti tuhuma hizo kwenye taasisi hizo zaidi ya kuzisema kwenye majukwaa ya Kampeni.

Lowassa bado ana ushawishi chanya au hasi kwenye siasa za Tanzania, ndiyo maana kila mtu anatamani afanye kampeni Arumeru ili ama "amalizwe" au "awaonyeshe kazi" wapinzani wake.

Kwenye kampeni hakuna ushindani wa sera au ubishani wa tofauti za kutatua matatizo ya wana Arumeru badala yake kumejaa tambo nani atashinda, kuumbuana, kampeni za kifahari, uzushi,kutukanana, kudhalilishana, kutishana, na mwisho wa yote sintofahamu isiyo na lazima.

Nafasi ya mwanamke kwenye Kampeni bado ni kama haipo kwenye siasa za Tanzania. Kwenye Kampeni ya vyama vyote hakuna hata chama kimoja ambacho msemaji wake mkuu ni mwanamke. Wanawake waliopo Arumeru ni wapasha joto Microphone kabla "wenyewe" hawajapanda jukwaani.

Na la mwisho na muhimu,ni kwamba mwaka 2015 mtu atakaye tumia falsafa za Mwalimu kuombea kura ndiye atakayekuwa Rais wetu.

Recommendations???....................
Hapo kwenye red mkuu ndo vipi hapo?????
 
"Wapinzani wa CCM wanalalamika CCM inatumia rushwa kwenye kampeni lakini hawaziamini taasisi za kupambana na Rushwa na matokeo yake hawaripoti tuhuma hizo kwenye taasisi hizo zaidi ya kuzisema kwenye majukwaa ya Kampeni".
mjomba unataka waripoti nini kwenye taasisi ya rushwa wakati unajua wazi ni kupoteza muda ukitaka kujua sababu uliza ktk uchaguzi wa mwaka 2010 viongozi wangapi wa CCM walikamatwa live wakigawa rushwa mfano mzuri BETTY MACHANGU na MARGARETH SITTA je uliza kati yao wangapi licha kufungwa walifikishwa hata mahakamani ? zero unataka ushahidi gani tena.
 
Recommendations???....................
Hapo kwenye red mkuu ndo vipi hapo?????
Watanzania wengi wanatenda kibepari lakini wanafikiri kwa kijamaa. leo hii watanzania bado wanafikiri wanaweza kuishi kwenye ardhi isiyopimwa na ikaendelea kuwa yao. Kuna kundi kubwa na wasomi wakiwemo ambao wanafikiri ajira ni lazima itoke serikalini. Watu wetu bado wanataka afya zao zitunzwe bure na serikali kwa gharama za kodi zao.

Kwa mantiki hiyo ni mtu atakayewaambia watanzania kwamba yeye akichaguliwa kuwa Rais basi ataishi kijamaa ndiye atakayepata kura nyingi mwaka 2015. Moja ya kauli zilizompa sana Slaa umaarufu mwaka 2010 ni ile aliyosema kwamba yeye akichaguliwa akiingia Ikulu basi atakula Mihogo na kuhakikisha nyumba zote za serikali zilizouzwa zinarejeshwa kwa wenyewe!!

Watanzania wanapenda kuishi kijamaa ingawa matendo yao ni ya kibepari!!
 
Back
Top Bottom