Ni sensa gani kwa watanzania inayotakiwa wafu au wazima??

CAT5

Member
Aug 19, 2012
44
12
Kweli ni jambo la kuhuzunisha kama kweli lengo ilikuwa ni kusimamia zoezi la sensa lisikwamishwe kwa kuzuia mambo ya kisiasa,
hadi kupelekea kifo kwa Mtanzania huyu.
Je ni sensa ipi tunayoitarajia kama Taifa ili tupange maendeleo yetu kama tunavyohubiriwa na viongozi wetu hadi
kuwa na matumizi ya nguvu kubwa ya vyombo vya Dola kwa Watanzania wake ??
Ni ile idadi inayotokana na vifo au ile ya Watanzania waliohai???maake mpaka sasa vifo vya Watanzania vilivyoripotiwa
kusababishwa na zoezi la sensa sasa ni takribani watu wawili na sina hakika na idadi nyingine kupitia vurugu za wanafamilia
waliokataa zoezi hilo?
Vifo vya Watanzania kupitia nguvu za Dola limeniweka njia panda kujua sensa inahitaji Jumla ya idadi gani ya watu,HAI au Wafu???
Kisingizio cha kuua na kudai ni kuzuia mikutano ya kisiasa,hakika DAMU za hao watu zitatupeleka pabaya,
Nawaasa Watanzania wote bila kujali itikadi za Vyama vyetu au kutegemea CHADEMA tuu ikemee mauaji kama haya kutokea TUKEMEE KWA PAMOJA MATUMIZI MABAYA HAYA YA DOLA,kukaa kimya,Waswahili walisema LEO KWANGU KESHO KWAKO.
Uchunguzi unaohitajika ni wa nini kujua kilichotokea wakati kila kitu kipo wazi????????
 
Back
Top Bottom