Hivi kwa nini ukilala mbu huwa anapenda kusogea masikioni na kupiga mluzi wake unaokera sana?
Je kuna maelezo yoyote ya kisayansia yanayoelezea hii tabia mbaya sana ya viumbe hawa?
Mbu wanafata kwenye masikio kwasababu ya Carbon dioxide unayotoa mdomoni, pia kwenye masikio kuna thin skin with superficiall blood vessels. Wanapenda kwenye miguu sababu ya harufu inayotoka huko ni attratact tosha. Need more?
Ushi, ahsante....lakini umenichanganya!
1) Sasa kuna uhusiano gani kati ya Carbondioxide kutoka mdomoni na wao kwenda kupiga kelele masikioni? Kwa nini wasipige kambi mdomoni kabisa? Na ni vipi kwa wale tunaofunga midomo wakati wa kulala? Inakuaje yani?
2) Hiyo thin skin iko ndani ya sikio au nje? Wao wanafaidika vipi wakienda kupiga mdundiko wao masikioni..tena ukiwa umelala?
3) Kiutaratibu watu uoga kabla ya kulala. Sasa sijui miguu hutoa harufu gani hiyo wakati ni misafi? Hata hivyo, huko miguuni sio shida.
mie naomba kuuliza, je mbu anaweza kung´ata hata kiumbe kilicho kufa? maiti ya binadam mathalani.
QM una maswali mazuri sana
1) Mdomoni blood vessel ziko mbali QM, mbu huenda sehemu kufata source ya CO2, sasa husogea karibu na sikio
2) Thin skin ipo nje ya sikio, blood vessel zipo juu mbu inakuwa rahisi kufikia mishipa ya damu na kufyonza damu kwa proboscis (mouth part)
3) Miguu hutoa volatile odour moja wapo ni unsaturated fats ambazo naturally miguu hutoa regardless umeoga ama usafisha hiyo huvutia sana mbu.
Nitakupa mfano Kuku mbu huenda kuuma kwenye combs and wattles, unajua tena kuku ana manyoya na miguu yake ina magamba, its an adaptaion na evolution inafavor hayo...
Hiyo ya miguu imeeleweka kwa ufasaha.....
Turudi masikioni....
...Kutokana na maelezo yako inaonyesha kuwa hawa viumbe upenda masikio kwa sababu ya hizo vessels zipo karibu kuzifikia. Na kwamba huenda kule kufyonza damu. Sawa? Kama ni hivyo, mbona wakifika masikioni upiga kelele tu na sio kung'ata viiile? Kwa nini ukiamka asubuhi unakuta umeng'atwa na kuvimba sana mikononi na miguuni, na sio masikioni? I mean, kutokana na maelezo yako, nilitegemea masikio ndio yangekuwa na majereha mengi sana ya ung'ato wa mbu. Au?
Ushi wa Rombo, maelezo murua, ahsante... nami naomba kuuliza maswali machache.
-- hiyo carbondioxide siyo kuwa ile inayotokea puani kama process ya kupumua, au unamaanisha ile inayotekea mdomoni tu?
--je, mbu hawa detect na kutumia kwa navigation infrared heat emission katika kuvinjari kwao?
--je, concentration ya emission ya infrared heat katika mwili hai correspond na organ za mwili, hivyo kichwani kuwa kuna joto?
Akhsante, ni hayo tu.
SteveD.
mie naomba kuuliza, je mbu anaweza kung´ata hata kiumbe kilicho kufa? maiti ya binadam mathalani.
Juu ya hiyo, aking'ata maiti aliyefariki kwa malaria, kuna uwezekano wowote wa mbu huyo kuambukiza malaria kwa binadamu hai?
Kuna sababu pia ambazo husababisha mbu kuuma zaidi mtu X kuliko Y nitataja kifupi tu, mfano quality ya damu ie Haemoglobin content, iron concetration ambazo hutofautiana watu na watu.
... Mbu hupendelea sehemu zile ambazo mishipa ya damu ipo jirani kurahisisha unyonyaji wa damu.
... Kuna sababu pia ambazo husababisha mbu kuuma zaidi mtu X kuliko Y nitataja kifupi tu, mfano quality ya damu ie Haemoglobin content, iron concetration ambazo hutofautiana watu na watu.
... kama unawalakini uliza
Ushirombo jitahidi kuwa makini na maelezo yako. Wengi wanategemea knowledge hii kuitumia. Si kweli kuwa mbu jike pekee ndiyo anauma. Ila mbu jike ndiyo anahitaji zaidi damu kwa ajili kutaga. Fortunately mbu jike pekee ndiyo ana uwezo wa kubeba na ku-transmit Plasimodium spp. Lakini ikumbukwe si mbu wote wana transmit malaria. Wengine tofauti kabisa. Kuna Anopheline, Culex ,,,, and so
Kuwa updated kuhusu kung'atwa na mbu pitia kidogo hii website. Why some people are prone to mosquito bites - Telegraph
Ushirombo,
Mbu atajuaje kwamba nikimnga'ta mtu X badala Y nitapata damu yenye "Haemoglobin na iron content" bora zaidi kabla hajang'ata ?
Na kama sikio na pua zote zinatoa hewa ya pumzi, tena zaidi pua, na kama kivutio cha sikio hapo ni ukaribu wa mishipa ya damu, sasa mbu atajuaje kwamba nikinga'ta karibu na sikio nitakuta mshipa wa damu kiurahisi kuliko karibu na mfupa wa pua ?