OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 419
- 670
Nchi kadhaa zimekuwa na mijadala juu ya ukomo wa umri ambao rais anatakiwa kutovuka ili kuendelea kutawala. Hata hivyo, baadhi ya marais wamekuwa wakibadili katiba zao ili kuhakikisha wanabaki madarakani. Hii sio shida lakini ni muhimu ukomo wa umri uwepo ili kutokuwa na marais wazee ambao maamuzi yao yanaweza kuathiri taifa kama ilivyotokea kwa nchi kadhaa barani Afrika.
Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 39(1)(b) imeweka kwamba mgombea urais ni lazima awe aliyetimiza miaka 40. Katiba hiyo hiyo haijataja ni je mtu akizidi umri upi hatofaa kugombea urais. Hili jambo ni muhimu sana kuwa nalo.
Kwa sasa Life Expectancy ya mtanzania ni miaka 66, lakini mara nyingine tumechagua watu waliozidi umri huo kwa kuwa hakuna ukomo wa umri wa mgombea urais. Hii sio tu inasema tutakuwa na marais wazee bali pia uzee unaambatana na magojwa na sisi tuna huduma mbovu za awafya ambazo zitatufanya tuwe tunafanya uchaguzi mara kwa mara au kuwafanya watu wengine kuwa marais baada ya wengine kufariki.
Tukiangalia mfano wa waliogombea urais mwaka 2015, wale waliokuwa vinara wagombea urais mwaka 2015, wengi wao walikuwa na miaka zaidi ya 60. Aidha imekuwa ni kama tamaduni sasa kwamba mtu akiwa na miaka isiyozidi 50 akigombea urais akaitwa 'kijana' na inaweza kuwa kikwazo hata kama katiba imeruhusu kugombea. Hebu fikiria Kikwete kuitwa kijana kwa sababu ya umri wake alioingia nao kwenye urais.
Suala la kutokuwa na ukomo wa urais limetengeneza tamaduni isiyoandikwa ya kuwa mtu kugombea urais lazima awe na miaka isiyopungua sitini. Mimi naona ni muhimu katiba iseme Rais asizidi miaka 65. Yaani aingie na miaka ambayo hata akitoka anakuwa hajafikia umri wa ukomo, ili tusije chagua mtu mwenye miaka 65 akakaa madarakani hadi akafika miaka 75, hatari inakuwa ni ile ile.
Nawasilisha.
Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 39(1)(b) imeweka kwamba mgombea urais ni lazima awe aliyetimiza miaka 40. Katiba hiyo hiyo haijataja ni je mtu akizidi umri upi hatofaa kugombea urais. Hili jambo ni muhimu sana kuwa nalo.
Kwa sasa Life Expectancy ya mtanzania ni miaka 66, lakini mara nyingine tumechagua watu waliozidi umri huo kwa kuwa hakuna ukomo wa umri wa mgombea urais. Hii sio tu inasema tutakuwa na marais wazee bali pia uzee unaambatana na magojwa na sisi tuna huduma mbovu za awafya ambazo zitatufanya tuwe tunafanya uchaguzi mara kwa mara au kuwafanya watu wengine kuwa marais baada ya wengine kufariki.
Tukiangalia mfano wa waliogombea urais mwaka 2015, wale waliokuwa vinara wagombea urais mwaka 2015, wengi wao walikuwa na miaka zaidi ya 60. Aidha imekuwa ni kama tamaduni sasa kwamba mtu akiwa na miaka isiyozidi 50 akigombea urais akaitwa 'kijana' na inaweza kuwa kikwazo hata kama katiba imeruhusu kugombea. Hebu fikiria Kikwete kuitwa kijana kwa sababu ya umri wake alioingia nao kwenye urais.
Suala la kutokuwa na ukomo wa urais limetengeneza tamaduni isiyoandikwa ya kuwa mtu kugombea urais lazima awe na miaka isiyopungua sitini. Mimi naona ni muhimu katiba iseme Rais asizidi miaka 65. Yaani aingie na miaka ambayo hata akitoka anakuwa hajafikia umri wa ukomo, ili tusije chagua mtu mwenye miaka 65 akakaa madarakani hadi akafika miaka 75, hatari inakuwa ni ile ile.
Nawasilisha.