Ni muda muafaka Kamanda Mbowe akabidhi chama kwa Tundu Lissu

Vitalis Msungwite

JF-Expert Member
May 11, 2014
3,269
7,775
Tarehe 23 wakati wa ufunguzi wa mikutano ya kisiasa pale Mwanza mheshimiwa mwenyekiti alipwaya Sana. Alionesha ni kwa namna gani anashindwa kutumikia mabwana wawili. Uso wake ulionesha anatamani uanaharakati lakini makubaliano na mama yanamkaba. Alikua anapata shida maana akisifia serikali makamanda hawamuelewi na akimkandia mama hatamuelewa hivyo akabaki kuongea pole pole na Kwa umakini mkubwa kiasi kwamba dakika Moja maneno 10 tu.

Alipowasili makamu mwenyekiti angalau alionesha mwanga Kwa chama kuwa kielekee njia ipi. Ingawa aliweka chumvi Sana kwenye hotuba yake lakini ndio maisha ya siasa. Hata mwenyekiti alibadirika kidogo hiyo siku.

Kutokana na Mbowe kuwa katikati ya pande mbili no Bora kwenye uchaguzi wa mwaka huu asigombee Tena. Hii itamfanya astaafu siasa Kwa heshima kuliko kuja kubezwa mbeleni ma makamanda. Tundu lissu ana amsha amsha na harakati za maana na convincing power ya kutosha ila Kwa mwenyekiti nafikiri hata umri umemtupa mkono apumzike.
 
Je wewe kikao Gani ulishawahi kukiendesha na ukafanikiwa ?
Ulishawahi kusimama mbele za watu kuzungumza Kwa hoja ?
Uloleta mabadiriko yeyote?
Sio Kila eneo unaweza kulitolea njia bali tafakari Kwa kina uje Nini kulikuwa kinamaanishwa
 
Rudisheni kwanzaa mabillioni yake aliyowaambiaa kuwa amepoteza hapa ufipa,Kama hamna basi tulieni ili arudishe mapesa yake yote,Kama Hamtaki Basi ondokeni mumuache na chama chake aendelee kurudisha mtaji wake
 
Chawa naona umeacha zile nyuzi za magazeti yako unakuja kupamia nyuzi za wanaume.
Ukweli ndio huo na mwenye kigoda wenu ameshawaambia wazi kuwa amepoteza mabillioni yake hapo,kwa hiyo subirini akusanye mpaka zitimu ,siyo mnakuja kudandia vyama vya watu njiani halafu mnajifanya kuleta ujuaji wenu
 
Makamanda people's

Iko hivi, mimi naona kwa hapa tulipofikia Mwenyekiti wetu ndugu Mbowe kwa heshima na taadhima akabidhi Uwenyekiti haraka sana kwa kamanda Lissu kabla chama hakijapoteza mvuto kwa wananchi.

Tukubali kuwa wananchi wengi wameshatambua wazi kuwa Mwenyekiti wetu kalamba asali hivyo kuendelea na Mbowe kwenye nafasi hiyo ya Uwenyekiti ni kuzidi kuzamisha jahazi la CHADEMA ambalo tayari linaelekea kuzama kwa kasi kubwa.

Niwatakie usiku mwema makamanda wenzangu.
 
Je wewe kikao Gani ulishawahi kukiendesha na ukafanikiwa ?
Ulishawahi kusimama mbele za watu kuzungumza Kwa hoja ?
Uloleta mabadiriko yeyote?
Sio Kila eneo unaweza kulitolea njia bali tafakari Kwa kina uje Nini kulikuwa kinamaanishwa
Lile kabila litakubali kweli
 
Tarehe 23 wakati wa ufunguzi wa mikutano ya kisiasa pale Mwanza mheshimiwa mwenyekiti alipwaya Sana. Alionesha ni kwa namna gani anashindwa kutumikia mabwana wawili. Uso wake ulionesha anatamani uanaharakati lakini makubaliano na mama yanamkaba. Alikua anapata shida maana akisifia serikali makamanda hawamuelewi na akimkandia mama hatamuelewa hivyo akabaki kuongea pole pole na Kwa umakini mkubwa kiasi kwamba dakika Moja maneno 10 tu.

Alipowasili makamu mwenyekiti angalau alionesha mwanga Kwa chama kuwa kielekee njia ipi. Ingawa aliweka chumvi Sana kwenye hotuba yake lakini ndio maisha ya siasa. Hata mwenyekiti alibadirika kidogo hiyo siku.

Kutokana na Mbowe kuwa katikati ya pande mbili no Bora kwenye uchaguzi wa mwaka huu asigombee Tena. Hii itamfanya astaafu siasa Kwa heshima kuliko kuja kubezwa mbeleni ma makamanda. Tundu lissu ana amsha amsha na harakati za maana na convincing power ya kutosha ila Kwa mwenyekiti nafikiri hata umri umemtupa mkono apumzike.
Kwani chadema bado ipo? Hiki chama kimeishajifia muda. Mnachokiona sasa ni mzimu wake.
 
Nyie mnaoshabikia hiyo hoja mna mpango wa kuiua chadema, sikubaliani nanyi. Mr #dishlimetilt hana akili, hekima, wala uwezo wa kuongoza chama cha siasa.
 
Ili chadema ife haraka siyo?
Kwa taarifa yako Mr #dishlimetilt hana akili, hekima, wala uwezo wa kuongoza chama cha siasa.
 
Mtoa hoja pls rejea katiba ya CHADEMA inasemaje kuhusu nafasi ya Chairman wa Chama, na vema kuishi kwa mujibu wa kisheria, always CHADEMA inajipambanua kutoka vyama vingine kwa up hold katiba.
 
Apana haitawezekana kumpa usukani wa CHADEMA Bw Lissu, Hana Busara na Akili tukivu, amekaa kama mkicha mkicha hivi, inaogopesha akijasirika atakivuruga chama na kukiuwa au kukichoma moto
 
Makamanda people's

Iko hivi, mimi naona kwa hapa tulipofikia Mwenyekiti wetu ndugu Mbowe kwa heshima na taadhima akabidhi Uwenyekiti haraka sana kwa kamanda Lissu kabla chama hakijapoteza mvuto kwa wananchi.

Tukubali kuwa wananchi wengi wameshatambua wazi kuwa Mwenyekiti wetu kalamba asali hivyo kuendelea na Mbowe kwenye nafasi hiyo ya Uwenyekiti ni kuzidi kuzamisha jahazi la CHADEMA ambalo tayari linaelekea kuzama kwa kasi kubwa.

Niwatakie usiku mwema makamanda wenzangu.
Acha lizame.
Wewe linakuhusu?.
 
Back
Top Bottom