Ni kweli kuja kwa Lowassa CHADEMA kumesaidia kitu CHADEMA?

Wana JF.

Kama wachambuzi wengi makini wa siasa walivyotabiri, CHADEMA imeshindwa kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Oktoba2015. Ingawa kushindwa huko kwa CHADEMA kumechangiwa na mambo mengi, lakini kubwa zaidi ni makosa yaliyofanywa na mwenyekiti wake mh. Freeman Mbowe kushinikiza chama kimsimamishe mgombea asiyekubalika.

Ingawa baadhi ya watu wakiangalia juu juu wanaona mgombea aliyeletwa na Mbowe ameleta manufaa, lakini ukiangalia hesabu kwa makini utaona kuwa mgombea huyo hajakinufaisha chama na badala yake amekiletea chama hicho migogoro na kukitenganisha na agenda yake kuu ya ufisadi.Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA mh. Freeman Mbowe alipata asilimia 5.88 ya kura za urais. Mwaka 2010 mgombea Dr. Slaa alipata asilimia 27.05.

Hii ni tofauti ya asilimia 21.17 au ongezeko la asilimia 360 ikilinganishwa na 2005.Vilevile, mwaka 2005 Chadema ilipata majimbo 5. Mwaka 2010 ilipata majimbo 23. Ongezeko hili la majimbo 18 ni sawa na asilimia 360.Mafanikio haya waliyapata CHADEMA bila kuhitaji msaada wa mgombea wa kuazima toka CCM. Kama waliweza wenyewe kufika hapa, ni sahihi kuamini kuwa wangeweza kwenda mbali zaidi.katika uchaguzi wa mwaka huu,CHADEMA wamepata asilimia 39.97. Hii ni tofauti ya asilimia 12.92 ikilinganishwa na matokeo ya chadema ya mwaka 2010.

Hapa utaona kuwa ongezeko aliloleta mgombea "wa kuazima toka CCM" ni dogo kuliko ongezeko aliloleta Slaa la asilimia 21.17.Kwenye ubunge, mwaka huu CHADEMA imepata majimbo 39. Hili ni ongezeko la majimbo 16 ambayo ni sawa na ongezeko la aslimia 69.6. Hapa utaona kuwa mgombea "wa kuazima toka CCM" ameshindwa kuongeza kiasi cha majimbo kama alichoongeza Slaa mwaka 2010.

Ikumbukwe kuwa mgombea wa mwaka huu aliungwa mkono na vyama vinne vya upinzani tofauti na miaka iliyopita ambayo mgombea wa CHADEMA alikuwa anasimama peke yake. Kuungwa mkono huku kulimfanya pia mgombea huyo awe na wabunge wengi wa majimbo (47) wanaompigia kampeni Bara na Visiwani. Dr. Slaa alikuwa na wabunge watano (5) tu waliompigia kampeni.-Pamoja na kuungwa mkono huko lakini bado mgombea hajafanikiwa kuleta mafanikio zaidi ya mwaka 2010.Hitimisho:Woga wa Mbowe umeiponza CHADEMA bure. CHADEMA ilishaanza kujiimarisha kitaasisi na sasa sura ya kitaasisi imebomolewa na kujengwa sura ya kutegemea jina la mtu mmoja.

Kauli za Mbowe na viongozi wengine wa CHADEMA kuwa hawawezi kushinda uchaguzi bila kuchukua kigogo toka CCM itawatafuna siku za usoni na kuwakatisha tamaa wafuasi wao kwenye chaguzi zijazo iwapo hawatapata kigogo wa CCM wa kugombea kupitia CHADEMA.CHADEMA ina jukumu kubwa la kutafuta mtu wa kufidia nafasi ya Dr. Slaa.

Kihesabu hakuna mtu aliyevuna mafanikio makubwa kwa CHADEMA kama Dr. Slaa. Lowassa ameshafikia kilele chake, haongezeki tena nguvu. Kama ameshindwa kufikia level ya Dr. Slaa katika uchaguzi huu, basi hataifikia tena.Uchaguzi huu ni fundisho kwa vyama kuthamini mafanikio ya hatua kwa hatua inayojipatia yenyewe kwa kuheshimu misingi yake kuliko kukimbilia tamaa za kuenda ikulu kwa kubomoa misingi iliyojengwa kwa miaka mingi.

Cc; Zemarcopolo.

Uchakachuzi umekwisha tafuteni kazi mfanye,au kajipangeni kwenye mitaa yenu msubiri zile milioni 50, achaneni na ya Chadema.
 
Poleni sana ccm, kila mtu anajua mlijipanga kupiga kampeni za udini ili kupoteza kura za wale ambao wakisikia neno 'padri' wanapata kizunguzungu. Mlivyoachwa kwenye mataa, mkabaki kujitoa utu, maadili na hata kuachana na imani za dini zenu hadi kumsingizia magonjwa mgombea wa upinzani... Poleni sana nendeni mkatafute toba kwa Muumba wenu maana itakuwa vigumu sana kuachana na laana mliyojiletea juu ya vichwa vyenu katika kipindi chote cha kampeni.
 
NI upuuzi wa hali ya juu kupima ushindi wa vyama chini ya tume ya uchaguzi iliyo chini ya chama tawala, tumeona jinsi matokeo ya wapinzani yalivyo tolewa kwa mbinde... tusipoteze muda kujadili huu ugoro. cha maana majadiliano haya yawepo kama kutakuwa na tume huru, Basi...
 
Katika kitu ambacho huwa nakiona sisi watanzania tunakosa,ni ujasili;yaani hiki kitu hiki kinatutafuna sana,naomba nifafanue kwanini kukosa ujasili;

Siku zote mtu akionekana ana hela,watu hushindwa kabisa kumwambia ukweli hata kama anakosea;yote hayo ni sababu ya pesa. Mfano;mimi katika mtandao wa usokitabu(facebook),niko na friendship na mbunge wa hapa Shinyanga mjini,nadhani wengi mnamfahamu na kwa kiasi kikubwa alihusika sana katika sakata la mwaka jana la wizi wa Bilion 322,ambayo yeye alikuwa naibu waziri wa Nishati husika.

Siku moja nimeamka nika-log in kwa ukurasa wangu wa fb nikakutana na post ya His Excellency The MP,akisema kuwa kafanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuiletea maendeleo Shinyanga na hadi sasa barabara za lami(tarmac roads) zinajengwa karibu kila mtaa;kitu ambacho kwa mkazi wa Shinyanga na anayeifahamu vizuri Shinyanga akiona post ile iliyokuwa inanadi maendeleo hewa,hakika lazima kwa namna moja ama nyingine asingeweza kuvumilia hata kidogo. Kitu ambacho nilijifunza katika post ile ni kwamba,hakika tajiri hupata utukufu kwa ajili ya utajiri wake! Pamoja na kuwa wanashinyanga wanajua kabisa ukweli wa ----- lile,lakini karibu kila comment iliyoandikwa pale ilikuwa ni ya kumpongeza na tukapatikana watu wawili tu ambao ilitubidi tumwamambie makavu na katika kumwambia vile,karibu watu wote wakatugeukia na kuanza kutuchamba eti tunampiga vijembe yule -----,ni kitu ambacho ukikiangalia ni upuuzi wa hali ya juu na ukiangalia na uhalisia wa mkoa wa Shinyanga ulivyo. Mbaya zaidi Mbuge mwenyewe si mzaliwa hata wa Shinyanga;ni moja ya comment ambazo nilimhoji na ndipo kila mmoja akabwatuka eti ningeweza hata kufungwa kwa kumkashfu Mheshimiwa,shame on us! Nilichowajibu ni kwamba,sikuwa naogopa kufungwa,nilichotaka tu awe mkweli kwa wananchi wake na si kuwapa taarifa bandia tena kwenye mitandao ya kijamii ambapo dunia inaona!

Back to the topic! Lowasa ana hela na naomba hilo nikiri kuwa,EL alikuwa na uwezo wa kufanya anachokitaka kwa pesa zake na ndiyo maana alitamani hata kuinunua Ikulu;nadhani wengi mtakumbuka kuna kundi alilianzisha kipindi alikuwa kwenye kile chama cha kijani,kikundi kilichotamba kwa jina la 4U MOVEMENT FRIENDS OF LOWASA ambacho kilimwaga hela ndefu balaa;kwa Shinyanga mtakumbuka kuna watu walihudhuria pale SEREVA LODGE na watu wakapewa ahadi kuwa ilikuwa imeandaliwa YUTONG kuwapeleka ARUSHA siku ya kutangaza nia,yote ni kazi ya pesa!

Kwa hiyo kumwambia LOWASA uchafu wake ilikuwa ni kama kumkashfu MUNGU,maana uatapishana na neema! Hana lolote,tofauti na majivuno ya pesa zake;hakuwahi hata kuzungumzia ufisadi,maana unamgusa sawasawa na kwa walioangalia siku alikuwa anahojiwa na BBC dira ya Dunia juu ya ufisadi,kama moja ya swali aliloulizwa na Zuhura Yunus,alisema tu,"...hilo ni swali gumu...refu..." hakuwa na cha kuzungumza kabisa juu ya suala hilo nyeti la kitaifa kwa sababu linamhusu na ni mhusika mkubwa!

MY INTAKE;kwa CHADEMA,kurudisha hadhi yake tena si leo wala kesho. Mungu saidia kumrudisha DR Slaa,vinginevyo kazi tunayo..badilika ndugu yangu,LOWASA si chochote si lolote katika siasa,ila hela zake tu!
 
Wana JF.

Kama wachambuzi wengi makini wa siasa walivyotabiri, CHADEMA imeshindwa kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwezi Oktoba2015. Ingawa kushindwa huko kwa CHADEMA kumechangiwa na mambo mengi, lakini kubwa zaidi ni makosa yaliyofanywa na mwenyekiti wake mh. Freeman Mbowe kushinikiza chama kimsimamishe mgombea asiyekubalika.

Ingawa baadhi ya watu wakiangalia juu juu wanaona mgombea aliyeletwa na Mbowe ameleta manufaa, lakini ukiangalia hesabu kwa makini utaona kuwa mgombea huyo hajakinufaisha chama na badala yake amekiletea chama hicho migogoro na kukitenganisha na agenda yake kuu ya ufisadi.

Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA mh. Freeman Mbowe alipata asilimia 5.88 ya kura za urais. Mwaka 2010 mgombea Dr. Slaa alipata asilimia 27.05.

Hii ni tofauti ya asilimia 21.17 au ongezeko la asilimia 360 ikilinganishwa na 2005.Vilevile, mwaka 2005 Chadema ilipata majimbo 5. Mwaka 2010 ilipata majimbo 23. Ongezeko hili la majimbo 18 ni sawa na asilimia 360.Mafanikio haya waliyapata CHADEMA bila kuhitaji msaada wa mgombea wa kuazima toka CCM.

Kama waliweza wenyewe kufika hapa, ni sahihi kuamini kuwa wangeweza kwenda mbali zaidi, katika uchaguzi wa mwaka huu, CHADEMA wamepata asilimia 39.97. Hii ni tofauti ya asilimia 12.92 ikilinganishwa na matokeo ya chadema ya mwaka 2010.

Hapa utaona kuwa ongezeko aliloleta mgombea "wa kuazima toka CCM" ni dogo kuliko ongezeko aliloleta Slaa la asilimia 21.17.

Kwenye ubunge, mwaka huu CHADEMA imepata majimbo 35. Hili ni ongezeko la majimbo 16 ambayo ni sawa na ongezeko la aslimia 69.6. Hapa utaona kuwa mgombea "wa kuazima toka CCM" ameshindwa kuongeza kiasi cha majimbo kama alichoongeza Slaa mwaka 2010.

Ikumbukwe kuwa mgombea wa mwaka huu aliungwa mkono na vyama vinne vya upinzani tofauti na miaka iliyopita ambayo mgombea wa CHADEMA alikuwa anasimama peke yake. Kuungwa mkono huku kulimfanya pia mgombea huyo awe na wabunge wengi wa majimbo (47) wanaompigia kampeni Bara na Visiwani.

Dr. Slaa alikuwa na wabunge watano (5) tu waliompigia kampeni.-Pamoja na kuungwa mkono huko lakini bado mgombea hajafanikiwa kuleta mafanikio zaidi ya mwaka 2010.

Hitimisho:Woga wa Mbowe umeiponza CHADEMA bure.

CHADEMA ilishaanza kujiimarisha kitaasisi na sasa sura ya kitaasisi imebomolewa na kujengwa sura ya kutegemea jina la mtu mmoja.

Kauli za Mbowe na viongozi wengine wa CHADEMA kuwa hawawezi kushinda uchaguzi bila kuchukua kigogo toka CCM itawatafuna siku za usoni na kuwakatisha tamaa wafuasi wao kwenye chaguzi zijazo iwapo hawatapata kigogo wa CCM wa kugombea kupitia CHADEMA.CHADEMA ina jukumu kubwa la kutafuta mtu wa kufidia nafasi ya Dr. Slaa.

Kihesabu hakuna mtu aliyevuna mafanikio makubwa kwa CHADEMA kama Dr. Slaa. Lowassa ameshafikia kilele chake, haongezeki tena nguvu. Kama ameshindwa kufikia level ya Dr. Slaa katika uchaguzi huu, basi hataifikia tena.

Uchaguzi huu ni fundisho kwa vyama kuthamini mafanikio ya hatua kwa hatua inayojipatia yenyewe kwa kuheshimu misingi yake kuliko kukimbilia tamaa za kuenda ikulu kwa kubomoa misingi iliyojengwa kwa miaka mingi.

Cc; Zemarcopolo.

Acha kudanganya Umma wa W8atanzania...Hii Asilimia 360..IPO sayari Gani.??....bila shaka wewe ndiye uliyekuwa ukiwapikia NEC..zili data za uongo........Jiulize kwanza nini maana ya Asilimia..
 
mafanikio ya chadema na ukawa yameonekana dhahiri ,kwa mfano CUF wamefanikiwakuongeza idadi wabunge ,chadma imefnikwa kuongeza idadi ya kura za raisi na meya majiji matano.
 
mafanikio ya chadema na ukawa yameonekana dhahiri ,kwa mfano CUF wamefanikiwakuongeza idadi wabunge ,chadma imefnikwa kuongeza idadi ya kura za raisi na meya majiji matano.

ni kweli kuna mafanikio ukawa ukawa lakini haiendani na hiyo inverstment iliyofanyika.
 
Umeongea Pumba tu bila Lowasa UKAWA/CHADEMA ingepigwa vibaya mno. Mbona haoungelei Majimbo aliyoyaleta Upinzani Mh.Lowasa mfano Monduli, Arumeru Magharibi, Simanjiro, Same Magharibi, Moshi vijijini na Siha.
CUF walivyonufaika kule Unguja refer Majimbo aliyoongoza Lowasa na Maalim Seif kaongoza.
Lowasa kapunguza luzuku za CCM mara dufu.
Bila kuongeza hayo majimbo CHADEMA ingeloose sana, Kupoteza VITI kanda ya Ziwa ambako kulikuwa na ngome ya CHADEMA ni ushahidi Kanda ya Ziwa wamebadilika baada ya kuletewa mtu wa kwao, kabila lao na kanda yao. Si rahisi kumsaliti.
Unapotoa Mada uwe unaondoa BIAS ongelea Positive effects AND NEGATIVE EFFECTS za Ujio wa Lowasa CHADEMA na UKAWA otherwise utakuwa unaongelea ushabiki ambao hauna TIJA kwa Taifa.
 
Shehe ponda vipi mambo yake?ccm wamekataa kuwapa haki yao ya kiwanja cha shule future ya waislamu vipiunaweza fafanua hili.


Swissme

Fungulia nyuzi, tutakuja kukujibu.

Mada ya huu uzi, soma kichwa cha habari na utoe majibu kama unayo.
 
Ahsante Carlos Valderrama kwa kufanyia editing, na sasa unasomeka vizuri zaidi.

Mbowe kafanya maamuzi ya kibiashara, kaona mnhh urais hatuupati basi na pesa pia asipate? Kauza utu kwa pesa. Simpo.
 
Last edited by a moderator:
UKAWA umekufa sababu tumewashitukia nyinyi ni wachaga na mmefanya mambo kwa uchaga wenu sasa dawa yenu ipo jikoni tukutane 2020 insaallah tuwaonyeshe watanzania kuwa hatupo tayari kuongozwa na ukoo wa fulani
 
lOWASSA atakuwa na manufaa kwa watanzania kwani amewatia kiwewe CCM na ni lazima wajipange ili kuhakikisha wanarejesha imani kwa watanzania. Pia kwa UKAWA amewasaidia kwani ameibomoa CCM na itaendelea kubomoka siku hadi siku. Ni technical person atakayeendelea kukiimalisha chama kwa mbinu mbadala za uongozi na utendaji!
 
  • Thanks
Reactions: tim
Watu wakiambiwa ukweli wanakuwa wakali bila kuleta hoja za maana. Lowassa imekuwa hasara kwa UKAWA, na hasa CDM.

Kuna watu, mimi mmoja wao, tulikuwa na matumaini sana na CDM. Kitendo cha kumpokea Lowassa kilitufanya tuchague a lesser of the two evils between Lowassa na Magufuli. The lesser evil ni John Pombe Magufuli. Kumchagua Magufuli hakuwezi kuwa sawa na kuipenda CCM katika suala hili.

Muda peke yake ndiyo utatuambia kama ujio wa Lowassa ulikuwa mwema kwa CDM. Chama lazima kiwe na misingi yake. Bila kufuata misingi hiyo, sio chama bali ni kundi la wahuni wanaofuata upepo tu.
 
Poor analysis....! Unafikiria waTanzania wa leo ni wa mwaka 47?

Unataka kufanananisha watanzania Watanzania ya 2010, na 2015?

Pumba kabisa......

Kama hujui kusoma, hata picha huoni?
 
Back
Top Bottom