mkongo
Member
- Nov 21, 2009
- 19
- 9
Nakuja tena na video kuonyesha msisitizo. Najua baadhi yetu mtakuwa mmeshaangalia video hizi za Unyanyasaji wa polisi wa tanzania (FFU). Ni kwamba elimu yao haiwatoshi? au viongozi wao waliowatuma pamoja na waziri wa wakati huo nao ni hivi hivi. Unaona kabisa mtu habishi kukamatwa lakini wanatembeza mkong'oto utafikiri wanapiga mnyama. Haya ni matumizi ya nguvu yasiyo na lazima. Lawama hizi ziwaeendee Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar. Nasema tena NAWACHUKIA SANA. Sijui mnajionaje mnapoamka asubuhi na Kuvaa Suti na kujitokeza mbele za watu. Sijui mnafikiri nini mnapotoa amri mambo haya yatokee au hata kuyaona na kukaa kimya. Jaribu kujibadilisha kidogo na kufikiri kama ungekuwa mmoja wa hawa wanaofanyiwa hivi vitendo vya unyanyasaji. Bonyeza kwenye linki zifuatazo kujionea mwenyewe [ame]http://www.youtube.com/watch?v=8vTs4Ue2cPs[/ame] [ame]http://www.youtube.com/watch?v=P1-YuxjdcvU&feature=related[/ame]