Ni habari lakini hazifunguki - Sakata

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Denti wa Mama JK ajazwa mimba

Mhe. Mungai alipuliwa

Sorce Ippmedia 22/11/2008

Kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting
 
Denti wa Mama JK ajazwa mimba

Mhe. Mungai alipuliwa

Sorce Ippmedia 22/11/2008

Kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting


Denti wa Mama JK akijazwa mimba nayo ni breaking news? Kwa hiyo ukiwa denti wa mama JK ni marufuku kuzaa? Maana huwezi kuzaa kama hujapata mimba!

Hizi alasiri news.
 
Denti wa Mama JK ajazwa mimba

Mhe. Mungai alipuliwa

Sorce Ippmedia 22/11/2008

Kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting

Denti wa Mama JK akijazwa mimba nayo ni breaking news? Kwa hiyo ukiwa denti wa mama JK ni marufuku kuzaa? Maana huwezi kuzaa kama hujapata mimba!

Hizi alasiri news.

Da nilizani wamepita na kuvuluga kwa Mh.laisi kumbe ni mfazili tu,hawa waandishi wanazidi kukosa adabu.
 
Mhe. Mungai alipuliwa

2008-11-22 16:55:39
Na Emmanuel Lengwa, Jijini

Wakati vuguvugu la kufichua watu wanaojihusisha na ufisadi nchini limepamba moto, mbunge mmoja wa CCM, amejikuta akilipuliwa kwa kudaiwa kuwa naye ni fisadi mkubwa.

Mheshimiwa aliyerushiwa kombora hilo la kufungia mwaka, ni Bw. Joseph Mungai ambaye ni mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini.

Tuhuma hizo za kifisadi dhidi ya Bw. Mungai zimetolewa na Bw. Renatus Mkinga wakati akichangia mada kwenye kipindi cha Kipimajoto, kilichorushwa `live` na kituo cha luninga cha ITV jana usiku.

Akizungumza kwa kujiamini, Bw. Mkinga alidai kuwa wakati Bw. Mungai akiwa Waziri wa Elimu na Utamaduni wa serikali ya awamu ya tatu, ulitokea wizi wa fedha zaidi ya shilingi bilioni tatu , mali ya wizara hiyo.

Akadai punde tu wizi huo ulipotokea, mfanyakazi mmoja wa Wizara hiyo ambaye Bw. Mkinga hakumtaja jina, aligundua na kutoa taarifa kwa Mungai ili hatua zaidi zichukuliwe.

Bw. Mkinga alizidi kudai kuwa badala ya Waziri Mungai kufuatilia taarifa hizo, alikanusha vikali kuwa hakuna wizi uliotokea na kuchukua hatua kali za kumtimua kazi mfanyakazi huyo aliyebaini upotevu wa fedha.

Akadai kuwa hata hivyo ukaguzi wa kina ulipofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, ikagundulika kuwa fedha hizo zaidi ya shilingi bilioni tatu zilikuwa zimeibwa wizarani hapo.

Bw. Mkinga alidai kuwa anashangaa kuwa licha ya ukweli huo kubainika, Waziri Mungai hadi sasa bado hajakamatwa na wala mfanyakazi aliyefukuzwa kazi kwa kutoa taarifa hizo za upotevu wa fedha hajarejeshwa kazini.

``Naomba nitumie fursa hii kuiomba Serikali imrejeshe kazini kijana huyo, na kumchukulia hatua Mungai, nadhani hata yeye ni fisadi,`` akasema Bw. Mkinga.

Kipindi hicho ya Kipimajoto kinachorushwa na ITV `live` kila Ijumaa, jana kilikuwa kikijadili mada ya nini kifanyike kupata suluhu ya migomo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu.

SOURCE: Alasiri
 
Denti wa Mama JK ajazwa mimba

Mhe. Mungai alipuliwa

Sorce Ippmedia 22/11/2008

Kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting
Khaa. huna mpya. Umerishai!!!!!!!
 
Mi naona nyuzi hii ipelekwe kuleee kwenye Jokes na utani......


Utani ni nini?

Kama habari hii ni utani, nadhani kila kitu tunachoongea ni utani.
Kuna masawali mengi ya msingi ya kujiuliza kuhusu tuhuma hizi kuliko kutoa maoni ya kuipeleka habari kwenye utani.

Labda sielewi, utani kwenye habari hii uko wapi? Naomba nielekezwe.
 
Utani ni nini?

Kama habari hii ni utani, nadhani kila kitu tunachoongea ni utani.
Kuna masawali mengi ya msingi ya kujiuliza kuhusu tuhuma hizi kuliko kutoa maoni ya kuipeleka habari kwenye utani.

Labda sielewi, utani kwenye habari hii uko wapi? Naomba nielekezwe.
Kama utasoma kichwa habari na muandishi mwenyewe alivyoanza ndio utaona, au kama ukii-edit na kuweza kuiweka kwenye hadhi ya kujadilika seriously then itastahili kuwa hapa.....Hebu wewe angalia mwenyewe muanzishaji alivyoandika...
 
denti wa mama jk ajazwa mimba

mhe. Mungai alipuliwa

sorce ippmedia 22/11/2008

kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting

leo nimeamini kweli wewe ni mwiba.......................
 
Mi naona nyuzi hii ipelekwe kuleee kwenye Jokes na utani......

Jokes? Utani? ur serious? Mtu kasema ukweli kafukuzwa kazi. Two Billion zimeliwa na ikathibitishwa hivyo na Mhusika mkuu bado anapeta mtaani, Wanafunzi wetu shida kila kukicha acha hizo bwana Mizengwe
 
Mhe. Mungai alipuliwa

2008-11-22 16:55:39
Na Emmanuel Lengwa, Jijini

Wakati vuguvugu la kufichua watu wanaojihusisha na ufisadi nchini limepamba moto, mbunge mmoja wa CCM, amejikuta akilipuliwa kwa kudaiwa kuwa naye ni fisadi mkubwa.

Mheshimiwa aliyerushiwa kombora hilo la kufungia mwaka, ni Bw. Joseph Mungai ambaye ni mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini.

Tuhuma hizo za kifisadi dhidi ya Bw. Mungai zimetolewa na Bw. Renatus Mkinga wakati akichangia mada kwenye kipindi cha Kipimajoto, kilichorushwa `live` na kituo cha luninga cha ITV jana usiku.

Akizungumza kwa kujiamini, Bw. Mkinga alidai kuwa wakati Bw. Mungai akiwa Waziri wa Elimu na Utamaduni wa serikali ya awamu ya tatu, ulitokea wizi wa fedha zaidi ya shilingi bilioni tatu , mali ya wizara hiyo.

Akadai punde tu wizi huo ulipotokea, mfanyakazi mmoja wa Wizara hiyo ambaye Bw. Mkinga hakumtaja jina, aligundua na kutoa taarifa kwa Mungai ili hatua zaidi zichukuliwe.

Bw. Mkinga alizidi kudai kuwa badala ya Waziri Mungai kufuatilia taarifa hizo, alikanusha vikali kuwa hakuna wizi uliotokea na kuchukua hatua kali za kumtimua kazi mfanyakazi huyo aliyebaini upotevu wa fedha.

Akadai kuwa hata hivyo ukaguzi wa kina ulipofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, ikagundulika kuwa fedha hizo zaidi ya shilingi bilioni tatu zilikuwa zimeibwa wizarani hapo.

Bw. Mkinga alidai kuwa anashangaa kuwa licha ya ukweli huo kubainika, Waziri Mungai hadi sasa bado hajakamatwa na wala mfanyakazi aliyefukuzwa kazi kwa kutoa taarifa hizo za upotevu wa fedha hajarejeshwa kazini.

``Naomba nitumie fursa hii kuiomba Serikali imrejeshe kazini kijana huyo, na kumchukulia hatua Mungai, nadhani hata yeye ni fisadi,`` akasema Bw. Mkinga.

Kipindi hicho ya Kipimajoto kinachorushwa na ITV `live` kila Ijumaa, jana kilikuwa kikijadili mada ya nini kifanyike kupata suluhu ya migomo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu.

SOURCE: Alasiri



Anayedhani watanzania ni wakimya au hawana ujasiri, na afikiri tena. Hicho kipindi cha Kipimajoto kilikuwa moto sana. Big up kwa mzee Renatus Mkinga. Nakuombea uzima, naamini huko uliko uko salama salmin. Bila shaka huenda tukakusikia tena wakati mwingine - utushushie DATA zaidi.







.
 
Back
Top Bottom