Denti wa Mama JK ajazwa mimba
Mhe. Mungai alipuliwa
Sorce Ippmedia 22/11/2008
Kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting
Denti wa Mama JK ajazwa mimba
Mhe. Mungai alipuliwa
Sorce Ippmedia 22/11/2008
Kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting
Denti wa Mama JK akijazwa mimba nayo ni breaking news? Kwa hiyo ukiwa denti wa mama JK ni marufuku kuzaa? Maana huwezi kuzaa kama hujapata mimba!
Hizi alasiri news.
Da nilizani wamepita na kuvuluga kwa Mh.laisi kumbe ni mfazili tu,hawa waandishi wanazidi kukosa adabu.
Unamaanisha nini unapoandika
1. Nilizani
2. Kuvuluga
3. Laisi
4. Mfazili
Khaa. huna mpya. Umerishai!!!!!!!Denti wa Mama JK ajazwa mimba
Mhe. Mungai alipuliwa
Sorce Ippmedia 22/11/2008
Kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting
Mi naona nyuzi hii ipelekwe kuleee kwenye Jokes na utani......
Kama utasoma kichwa habari na muandishi mwenyewe alivyoanza ndio utaona, au kama ukii-edit na kuweza kuiweka kwenye hadhi ya kujadilika seriously then itastahili kuwa hapa.....Hebu wewe angalia mwenyewe muanzishaji alivyoandika...Utani ni nini?
Kama habari hii ni utani, nadhani kila kitu tunachoongea ni utani.
Kuna masawali mengi ya msingi ya kujiuliza kuhusu tuhuma hizi kuliko kutoa maoni ya kuipeleka habari kwenye utani.
Labda sielewi, utani kwenye habari hii uko wapi? Naomba nielekezwe.
denti wa mama jk ajazwa mimba
mhe. Mungai alipuliwa
sorce ippmedia 22/11/2008
kama kuna mtu ameweza kupata makala hayo na kuyasoma atuwekee ili tujue yaliyojiri katika habari hizo ukienda kwenye ippmedia utaona hazifunguki, very interesting
Mi naona nyuzi hii ipelekwe kuleee kwenye Jokes na utani......
Mhe. Mungai alipuliwa
2008-11-22 16:55:39
Na Emmanuel Lengwa, Jijini
Wakati vuguvugu la kufichua watu wanaojihusisha na ufisadi nchini limepamba moto, mbunge mmoja wa CCM, amejikuta akilipuliwa kwa kudaiwa kuwa naye ni fisadi mkubwa.
Mheshimiwa aliyerushiwa kombora hilo la kufungia mwaka, ni Bw. Joseph Mungai ambaye ni mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini.
Tuhuma hizo za kifisadi dhidi ya Bw. Mungai zimetolewa na Bw. Renatus Mkinga wakati akichangia mada kwenye kipindi cha Kipimajoto, kilichorushwa `live` na kituo cha luninga cha ITV jana usiku.
Akizungumza kwa kujiamini, Bw. Mkinga alidai kuwa wakati Bw. Mungai akiwa Waziri wa Elimu na Utamaduni wa serikali ya awamu ya tatu, ulitokea wizi wa fedha zaidi ya shilingi bilioni tatu , mali ya wizara hiyo.
Akadai punde tu wizi huo ulipotokea, mfanyakazi mmoja wa Wizara hiyo ambaye Bw. Mkinga hakumtaja jina, aligundua na kutoa taarifa kwa Mungai ili hatua zaidi zichukuliwe.
Bw. Mkinga alizidi kudai kuwa badala ya Waziri Mungai kufuatilia taarifa hizo, alikanusha vikali kuwa hakuna wizi uliotokea na kuchukua hatua kali za kumtimua kazi mfanyakazi huyo aliyebaini upotevu wa fedha.
Akadai kuwa hata hivyo ukaguzi wa kina ulipofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, ikagundulika kuwa fedha hizo zaidi ya shilingi bilioni tatu zilikuwa zimeibwa wizarani hapo.
Bw. Mkinga alidai kuwa anashangaa kuwa licha ya ukweli huo kubainika, Waziri Mungai hadi sasa bado hajakamatwa na wala mfanyakazi aliyefukuzwa kazi kwa kutoa taarifa hizo za upotevu wa fedha hajarejeshwa kazini.
``Naomba nitumie fursa hii kuiomba Serikali imrejeshe kazini kijana huyo, na kumchukulia hatua Mungai, nadhani hata yeye ni fisadi,`` akasema Bw. Mkinga.
Kipindi hicho ya Kipimajoto kinachorushwa na ITV `live` kila Ijumaa, jana kilikuwa kikijadili mada ya nini kifanyike kupata suluhu ya migomo ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu.
SOURCE: Alasiri